Zanzibar Electricity Corporation

Zanzibar Electricity Corporation Shirika la Umeme Zanzibar ni Shirika lenye jukumu la kusimamia uzalishaji, usambazaji na ugawaji ume

Mkutano huo wa 67 wa Jumuiya ya Kusini mwa Afrika ya Nishati ya Umeme — SAPP, umewakutanisha viongozi na wataalamu kutok...
11/09/2026

Mkutano huo wa 67 wa Jumuiya ya Kusini mwa Afrika ya Nishati ya Umeme — SAPP, umewakutanisha viongozi na wataalamu kutoka nchi wanachama kwa ajili ya kujadili masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya umeme.

Mkutano huo umehudhuriwa pia na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO), Mhandisi Haji Haji, pamoja na viongozi na wafanyakazi wa Shirika hilo, kwa lengo la kufuatilia kwa karibu majadiliano na utekelezaji wa masuala yanayohusu sekta ya umeme katika ukanda huo.

Mkutano wa 67 ulifunguliwa tarehe 7 Septemba 2026 na Mkurugenzi Mkuu wa ZECO, Mhandisi Haji Haji, ambapo wajumbe walifanya majadiliano kuhusu masuala mbalimbali ya ushirikiano katika sekta ya umeme.

Mkutano huo umefikia kilele leo, tarehe 11 Septemba 2026, ambapo kikao cha viongozi wa Jumuiya hiyo kimefungwa na Naibu Waziri wa Maji, Nishati na Madini wa Zanzibar, Mheshimiwa Seif Kombo Pandu.

Mkutano huo wa SAPP umeandaliwa na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO), ukiwa umejikita katika kuimarisha ushirikiano wa nchi wanachama katika sekta ya umeme, ikiwemo uzalishaji, usafirishaji na biashara ya nishati.

Ushirikiano huo unalenga kuhakikisha nchi wanachama zinakuwa na mifumo imara ya umeme, pamoja na uwezo wa kusaidiana pale zinapokabiliwa na changamoto za upatikanaji wa nishati.

Akizungumza wakati wa kufunga mkutano huo, Naibu Waziri wa Maji, Nishati na Madini Zanzibar, Mheshimiwa Seif Kombo Pandu, amesema Zanzibar ni miongoni mwa maeneo yanayoshiriki kikamilifu katika jitihada za kuimarisha sekta ya umeme, akieleza kuwa kupitia mkutano huo wanatarajia malengo yaliyowekwa yatafanikiwa.

Kwa upande wake, Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Usafirishaji wa Umeme kutoka TANESCO, Mhandisi Zakaria Mgarama, amesema mkutano huo umeweka msisitizo katika ushirikiano wa nchi mbalimbali katika sekta ya umeme, jambo litakalosaidia kuongeza usalama wa nishati na kuwezesha nchi wanachama kusaidiana pale zinapokabiliwa na changamoto za umeme.
# #

               #               #
11/09/2026

# #

SALAMU ZA POLE KWA MHE: SAMIA SULUHU HASSAN               #               #
07/09/2026

SALAMU ZA POLE KWA MHE: SAMIA SULUHU HASSAN
# #

TAARIFA YA KUKOSA UMEME
07/09/2026

TAARIFA YA KUKOSA UMEME

TAARIFA YA KUKOSA UMEME               #               #
06/09/2026

TAARIFA YA KUKOSA UMEME
# #

UJUMBE wa Benki ya Dunia (WB) umefurahishwa na maendeleo ya utekelezaji wa mradi wa Mabadiliko ya Sekta ya Nishati na Up...
04/09/2026

UJUMBE wa Benki ya Dunia (WB) umefurahishwa na maendeleo ya utekelezaji wa mradi wa Mabadiliko ya Sekta ya Nishati na Upatikanaji wa Umeme Zanzibar (ZESTA).

Kiongozi Mkuu wa ujumbe huo Bi. Rhonda Jordan amesema licha ya baadhi ya changamoto zilizojitokeza na ambazo wameziona katika ziara yao ya ukaguzi lakini bado ana matumaini ya kukamilika kwa mradi huo.

Ameeleza hayo wakati wa kikao cha kuhitimisha ziara yao ya Ukaguzi wa maendeleo ya mradi huo kilichofanyika ukumbi wa ZURA, Maisara ambacho kimewakutanisha watendaji wa ZESTA na Ujumbe wa Benki hiyo.

Naye Katibu Mkuu Wizara ya Maji Nishati na Madini Zanzibar amewataka watendaji wa mradi huo kuzishughulikia changamoto zilizobainishwa ili kukamilisha mradi huo ndani ya wakati husika.

Kikao hicho kinahitimisha ziara ya ujumbe huo ambao upo Zanzibar tokea tarehe 31 Agosti, 2026 kujionea maendeleo ya utekelezaji wa mradi wa ZESTA.

SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Wizara ya Maji Nishati na Madini inatekeleza mradi wa Mabadiliko ya Sekta ya N...
02/09/2026

SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Wizara ya Maji Nishati na Madini inatekeleza mradi wa Mabadiliko ya Sekta ya Nishati na Upatikanaji wa Umeme Zanzibar (ZESTA) ambao mbali na mambo mengine unajihusisha na mradi wa ujenzi wa kituo cha kuzalisha umeme kupitia nishati ya jua huko Makunduchi, Mkoa Kusini Unguja.

Mradi huo unaotekelezwa kwa ufadhili wa Benki ya Dunia ambao unasimamiwa na ZECO upo katika hatua za Mwishoni kukamilika kwake.

Kiwango cha megawati 18MW za umeme zinatarajiwa kuzalishwa kupitia kituo hicho ambazo zitaingizwa katika gridi.

Ujumbe huo umekagua kituo cha kusafirishia umeme kinachojengwa Welezo, minara ya njia ya kusafirishia umeme na kituo cha kuzalishia umeme Makunduchi.

Ujumbe huo upo Zanzibar kwa muda wa wiki moja kufanya ufuatiliaji wa miradi inayoyekelezwa kupitia WB


TAARIFA YA MATENEGENEZO               #               #
01/09/2026

TAARIFA YA MATENEGENEZO
# #

MRADI wa Mabadiliko ya Sekta ya Nishati na Upatikanaji wa Umeme Zanzibar (ZESTA - Project) ni mradi unaotekelezwa na Wiz...
31/08/2026

MRADI wa Mabadiliko ya Sekta ya Nishati na Upatikanaji wa Umeme Zanzibar (ZESTA - Project) ni mradi unaotekelezwa na Wizara ya Maji Nishati na Madini Zanzibar kupitia Benki ya Dunia (WB). Mbali na mambo mengineyo Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO) ni miongoni mwa watekelezaji wa mradi huu ambao unakusudia kujenga kituo cha kuzalishia umeme kwa kutumia nishati ya jua chenye uwezo wa kuzalisha megawati 18MW eneo la Makunduchi, Mkoa Kusini Unguja.

ZECO
31/08/2026

ZECO

Address

Zanzibar

Opening Hours

Monday 08:00 - 17:00
Tuesday 08:00 - 17:00
Wednesday 08:00 - 17:00
Thursday 08:00 - 17:00
Friday 08:00 - 17:00
Saturday 08:00 - 12:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Zanzibar Electricity Corporation posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Zanzibar Electricity Corporation:

Shortcuts

Share