Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi Zanzibar

Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi Zanzibar Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi Zanzibar, Government Official, ZURA BUILDING, MAISARA, Zanzibar City.

WANANCHI WAPATA ELIMU NA TAARIFA KUHUSU UCHUMI WA BULUUWananchi wanaotembelea banda la Sekta ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi...
17/09/2026

WANANCHI WAPATA ELIMU NA TAARIFA KUHUSU UCHUMI WA BULUU
Wananchi wanaotembelea banda la Sekta ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi katika Mkutano wa Kitaifa wa Uchumi wa Kijani (Green Summit) unaofanyika Mlimani City, Dar es Salaam, wamepata elimu na maelezo kuhusu fursa mbalimbali za kiuchumi zinazotokana na rasilimali za bahari.

Elimu hiyo inaeleza namna Uchumi wa Buluu na Uvuvi endelevu unavyoweza kuchangia ajira, uwekezaji, kuongeza kipato na kukuza maendeleo endelevu.

Lengo kuu la Mkutano ni kujadili na kutafuta fursa za kiuchumi zinazotokana na hatua za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, pamoja na kuimarisha mwelekeo wa Tanzania kuelekea uchumi wa kijani endelevu.

Katika muktadha huo, Sekta ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi ina nafasi muhimu katika kuibua fursa na kuhakikisha rasilimali za bahari zinatumika kwa tija na kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar  itaendelea kuweka mazingira wezeshi kwa wananchi wanaojishughulisha na shughuli za uvuvi...
14/09/2026

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar itaendelea kuweka mazingira wezeshi kwa wananchi wanaojishughulisha na shughuli za uvuvi na kilimo cha Mwani, ikiwa ni sehemu ya kuongeza fursa za ajira na kuinua kipato cha wananchi.

Akizungumza katika uzinduzi wa Diko la Samaki Fumba, Naibu Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mwanasha Khamis Juma amesema uwekezaji katika sekta ya uvuvi ni muhimu katika kukuza uchumi wa wananchi na kuimarisha matumizi endelevu ya rasilimali za bahari huku akiwataka wananchi kua na mashirikiano katika utekelezaji wa kazi zao za kujiingizia kipato

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Uchumi wa Buluu, Mheshimiwa Mboja Ramadhan Mshenga, amesema Serikali inalenga kuhakikisha changamoto zinazowakabili wananchi katika shughuli za uvuvi na kilimo cha Mwani zinapatiwa ufumbuzi ili shughuli hizo ziweze kuleta tija zaidi huku amewataka Wananchi wa eneo hilo kutunza miundombinu na rasilimali za bahari, pamoja na kuzitumia kwa uangalifu ili ziendelee kuwa na manufaa kwao na vizazi vijavyo.

Sheha wa Shehia ya Fumba, Mohammed Suleiman Mohammed, pamoja na Mratibu wa Diko, wameishukuru Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kutekeleza ahadi wakisema diko na boti walio patiwa Wakulima zitasaidia kuwaongezea wananchi uwezo wa kufanya shughuli zao za Uvuvi wa Mwani kwa ufanisi zaidi.

Pumzika Kwa Amani
07/09/2026

Pumzika Kwa Amani

Mradi wa TASFAM utaleta mabadiliko Makubwa katika Sekta za Uchumi wa Buluu na Uvuvi visiwani Zanzibar.Ameyasema hayo Afi...
01/09/2026

Mradi wa TASFAM utaleta mabadiliko Makubwa katika Sekta za Uchumi wa Buluu na Uvuvi visiwani Zanzibar.

Ameyasema hayo Afisa Mdhamin wa Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi Dkt. Salim Mohamed Hamza wakati akizungumza na Wadau katika Mkutano wa Wadau wa Mradi wa Kuimarisha usimamizi Endelevu wa Uvuvi na Ufugaji wa Mazao ya Baharini Tanzania TASFAM, huko Chakechake Pemba.

Mdhamin amesema, mipango na mikakati ya TASFAM ikiwemo Ujenzi wa Madiko makubwa ya Kisasa inaonesha namna Mradi utakua na Matokeo chanya Kwa Wananchi hususan wale wote wanaojishughulisha na shughuli za kiuchumu Kupitia Bahari.

Dkt. Salim amewaomba Wananchi na Wadau kutoa mashirikiano Kwa watendaji wa Mradi ili waweze kufanya kazi kwa ufanisi na kufikia malengo.

"Uchumi wa Buluu Kwa Maendeleo Endelevu"

Watendaji wa Mradi wa Kuimarisha Uvuvi Endelevu na Mazao ya Baharini Tanzania TASFAM wametakiwa kuhakikisha Wananchi wan...
26/08/2026

Watendaji wa Mradi wa Kuimarisha Uvuvi Endelevu na Mazao ya Baharini Tanzania TASFAM wametakiwa kuhakikisha Wananchi wanashirikishwa vyema katika utekelezaji wa Mradi ili kuleta ufanisi.

Ameyasema hayo Katibu Mkuu Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi Zanzibar. Kepteni Hamad Bakar Hamad wakati akifunga Mkutano wa Kwanza wa Wadau wa Sekta za Uchumi wa Buluu wa kutambulisha kazi, malengo na matarajio ya mradi kwa muda wa miaka mitano ili kuleta maendeleo katika Sekta za Uchumi wa Buluu. Mkutano huo umefanyika katika Ukumbi wa Zanzibar Ocean View Hotel.

Mradi wa Kuimarisha Uvuvi Endelevu na Mazao ya Baharini Tanzania TASFAM umeandaa mkutano na wadau wa sekta za Uchumi wa ...
26/08/2026

Mradi wa Kuimarisha Uvuvi Endelevu na Mazao ya Baharini Tanzania TASFAM umeandaa mkutano na wadau wa sekta za Uchumi wa Buluu wa kutambulisha kazi, malengo na matarajio ya mradi wa muda wa miaka mitano ili kuleta maendeleo katika sekta za Uchumi wa Buluu.

Mradi huo unategemewa kuleta mapinduzi katika sekta ya Uvuvi kwa kuweka miundombinu Bora ikiwemo kujenga madiko ya kisasa, vyumba vya kuhifadhia samaki pamoja na vifaa mbali mbali vya Uvuvi.

Pamoja na mambo mengine mkutano huu umekusudia kuwashirikisha wadau mbali mbali ili kutoa ushirikiano kwa watekelezaji wa mradi na wadau wote kwa ujumla.

Mashirika na Taasisi za kimataifa  zinazoshughulikia masuala ya uhifadhi na uendelezaji wa bahari ya Hindi zimefanya mku...
26/08/2026

Mashirika na Taasisi za kimataifa zinazoshughulikia masuala ya uhifadhi na uendelezaji wa bahari ya Hindi zimefanya mkutano wa siku tatu wa kuandaa na kuweka mikakati na itifaki juu ya anuai ya viumbehai vya Baharini.

Mkutano huo umefunguliwa na Naibu Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi Mheshimiwa Mboja Ramadhan Mshenga katika Hoteli ya Verde ambapo amesema nchi zilizozungukwa na bahari sio tu kuwa bahari ni sehemu ya Uchumi wao lakini bahari ndio utambulisho wa maisha na injini ya Uchumi wa nchi hizo.

Ameongeza kuwa mikakati hiyo itakayoafikiwa katika mkutano huo itatilia mkazo na kuweka ahadi ya pamoja ya kukuza ushirikiano katika uhifadhi na uendelezaji wa matumizi ya bahari na maisha ya viumbe bahari.

Mapema Mkuu wa kitengo Cha Mfumo wa Ikolojia ya bahari wa Shirika la Umoja wa Mataifa kuhusu Mazingira UNEP Sinikinesh Beyene Jimma amesema wanaendelea na mipango ya kuwajengea uwezo wadau wa Mazingira ya bahari, usimamizi mzuri wa Rasilimali za Baharini, kubadilishana taaluma, mlinganisho wa sera ili kuifanya bahari kuwa endelevu na himilivu kwa wakaazi na watumiaji WOTE wa bahari.

SERIKALI YASAINI MKATABA WA UNUNUZI WA MELI ZA UVUVI WA BAHARI KUU.Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (SMT) pam...
24/08/2026

SERIKALI YASAINI MKATABA WA UNUNUZI WA MELI ZA UVUVI WA BAHARI KUU.

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (SMT) pamoja na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) zimesaini mkataba wa ununuzi wa meli tatu (3) za uvuvi wa Bahari Kuu, ikiwa ni hatua muhimu inayolenga kuimarisha sekta ya uvuvi na kukuza Uchumi wa Buluu.

Meli hizo zinatarajiwa kutengenezwa na kukamilika ndani ya kipindi cha miezi tisa (9), na zitasaidia kuongeza uwezo wa uvuvi katika Bahari Kuu pamoja na kuleta fursa zaidi za kiuchumi kwa wananchi.

Upatikanaji wa meli hizo ni utekelezaji wa Mradi wa AFDP kwa ufadhili wa IFAD, ikiwa ni sehemu ya jitihada za Serikali katika kuendeleza uvuvi wa kisasa, kuongeza uzalishaji na kuhakikisha wananchi wananufaika zaidi na Rasilimali za Bahari.

"Uchumi wa Buluu Kwa Maendeleo Endelevu"

Taasisi za Serikali na binafsi zimeshauriwa kufanya utafiti na kuweka taarifa sahihi za sayansi ya bahari hali itakayosa...
17/08/2026

Taasisi za Serikali na binafsi zimeshauriwa kufanya utafiti na kuweka taarifa sahihi za sayansi ya bahari hali itakayosaidia kuifanya bahari kuwa salama na endelevu.

Akifungua mafunzo ya kuwajengea uwezo wataalamu wa ukusanyaji wa taarifa za bahari, Naibu Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi Mheshimiwa Mboja Ramadhan Mshenga amesema utafiti wa kisayansi ndio unaotoa dira ya matumizi sahihi na kuweka mazingira salama ya bahari na viumbe vyake.

Balozi Mkaazi wa China nchini Li Qianghua amesema bahari ya Zanzibar Ina upekee hivyo wataalamu wake wakipata mafunzo ya ukusanyaji wa taarifa za sayansi ya bahari itakuwa ni nyenzo muhimu ya uhifadhi wa bahari na ukuaji wa Uchumi katika sekta za Uchumi wa Buluu.

Ameongeza kuwa mafunzo hayo ambapo wataalamu wa wa Zanzibar watafaidika na mambo kadhaa kutoka kwa wenzao wa China ikiwemo kubadilishana uzoefu wa kitaalamu na kupata mbinu Bora za kisasa hali itakayosaidia kukuza Uchumi wa wananchi wa kawaida.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi na Rasilimali za Baharini Dkt. Zakaria Ali Khamis amesema mafunzo hayo ya siku 14 kwa wataalamu wa bahari kutoka Taasisi na Idara mbali mbali za Serikali yanayotolewa na wataalamu kutoka Jamhuri wa Watu WA China yatasaidia watumiaji.wa bahari kuitumia bahari kwa usahihi na kuisimamia ili itoe matokeo chanya kwa Taifa.

"Uchumi wa Buluu Kwa Maendeleo Endelevu"
16/08/2026

"Uchumi wa Buluu Kwa Maendeleo Endelevu"

Address

ZURA BUILDING, MAISARA
Zanzibar City

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi Zanzibar posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share