ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Urambo

ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Urambo Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Urambo, Public & Government Service, Urambo.

MCHONGO NI AFYA YAKO, ZINGATIA UNACHOKULA.Mkuu wa Wilaya Ya Urambo Dkt.Khamis Athumani Mkanachi amesema Watu wa Urambo k...
30/10/2024

MCHONGO NI AFYA YAKO, ZINGATIA UNACHOKULA.

Mkuu wa Wilaya Ya Urambo Dkt.Khamis Athumani Mkanachi amesema Watu wa Urambo kubadilisha mfumo wa Chakula ili kuimarisha afya zao.

Dkt.Khamis Mkanachi amesema hayo wakati akizungumza katika kilele cha maadhimisho ya Wiki ya Lishe iliyofanyika katika viwanja vya Kata ya Ussoke Tarafa ya Ussoke leo tarehe 30.10.2024.

DC. Mkanachi amesema vyakula vinavyohitajika kwa afya zetu vinalimwa katika maeneo yetuz hivyo tutumie vyakul hivyo kuimarisha afya zetu.

Hata hivyo Mhe. Mkuu wa Wilaya amesisitiza kwa kusema ulaji unaohitajika unatufanya tufanye kazi kwa bidii ili kujiletea maendeleo.

Aidha ameendelea kuwaelekeza wadau wa Lishe kuongeza nguvu kwani Takwimu zinaonyesha bado hali siyo nzuri kwa watu wengi ambao wamepimwa hawana lishe bora.

Baada ya kuhitimisha pamoja na maelekezo aliyoyatoa Mhe.Dkt Mkanachi aliongoza zoezi la kuchangia Damu Salama akiwa pamoja na Diwani wa Kata ya Ussoke Wakifuatiwa na baadhi ya Watumishi na Wanannchi.

Zoezi la uchangiaji limekuja baada ya Mhe. Dkt Khamis kutembelea banda la uchangiaji Damu Salama nakuelezwa kuwa hali ya uchangiaji hairidhishi na uhitaji wa Damu salama ni mkubwa sana.

Amesisitiza kwamba liwe zoezi endelevu kwani kumekuwa na uhitaji kwenye maeneo ya huduma za afya hasa kwa Wanawake wanaojifungua, watu wanaopata ajali na wengine kupungukiwa damu hivyo basi Watu wajitokeze kwa wingi kuchangia Damu Salama.

"Mchongo ni Afya , Zingatia unachokula"



Mkuu wa Wilaya ya Urambo Dkt.Khamis Athumani Mkanachi amewaaka TAWA kuwajibika kufuatilia malipo ya Migambo na (VGS) Vil...
29/10/2024

Mkuu wa Wilaya ya Urambo Dkt.Khamis Athumani Mkanachi amewaaka TAWA kuwajibika kufuatilia malipo ya Migambo na (VGS) Village Games Scout's ili kuwezesha ulinzi wa Hifadhi ya WMA.

Dkt.Khamis amesema hayo leo tarehe 29.10.2024 wakati akiwa katika ziara yake ya kutembelea hifadhi ya Wanyapori WMA kwenye kikao kabla ya kuingia kwenye Eneo la Hifadhi iliyopo Katika Kata ya Uyumbu.

DC Mkanachi ameongozana na k**ati Ya Ulinzi na Usalama pamoja Timu ya Halmashauri ikiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji Bi Grace Quintine, na Viongozi wa ngazi zote wa WMA.

Aidha DC Mkanachi amesema wajumbe wawakilishi wa wananchi kweny bodi ya Jumuiya kutimiza wajibu wao wa uwakilishi kwa Wananchi.

Pamoja na kutoa maelekezo hayo amemsimamisha kazi Afisa Mahusiano WMA Bwana Samora Wilium nakuagiza Uongozi wa Taasisi zinazohusika kumtafuta Mtumishi Mwingine atakayefanya kqzi hiyo kwani Samora Wilium alikuwa akilalamikiwa kwa kutofanya vizuri kweye majukumu yake.

Hata hiyo amewataka watumishi wa WMA pamoja na Viongozi wa Jumuiya kutojiingiza katika ujangili wa aina yoyote uwe wa Magogo wala wa Wanyama,huku akiwataka bajeti ya Jumuiya ipitishwe kwa Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri na siyo kupeleka tu Hundi ya malipo.

Katika ombi la Jumuiya ya kuongezewa Gari ns Silaha amewahakikishia silaha na Gari kila kitu kitakuwa sawa.

Hata hivyo Mwekezaji wa Jumuiya ya WMA Ndugu Hilary leo amekabidhi pikipiki mpya kwa Jumuiya nakuahidi kuongeza gari ndani ya Mwezi moja ili kuwasaidia Walinzi wa Hifadhi kufanya kazi kwa weledi mkubwa.
"Serikali za Mitaa, Sauti ya Wananchi, Jitokeze kushiriki Uchaguzi"



ya maliasili

"Serikali za Mitaa, Sauti ya Wananchi, Jitokeze kushiriki Uchaguzi"
23/10/2024

"Serikali za Mitaa, Sauti ya Wananchi, Jitokeze kushiriki Uchaguzi"



Mkuu wa Wilaya ya Urambo Dkt Khamis Mkanachi ameongoza Kamati ya Ulinzi na Usalama kupitia Nyumba kwa Nyumba kuwahamasis...
16/10/2024

Mkuu wa Wilaya ya Urambo Dkt Khamis Mkanachi ameongoza Kamati ya Ulinzi na Usalama kupitia Nyumba kwa Nyumba kuwahamasisha na kutoa Elimu kwa Wananchi kujiandikisha katiķa Daftari la orodha ya Wapiga Kura kwa ajili ya Uchaguzi wa serikali za Mitaa utakaofanyika Novemba 27, 2024.

DC Mkanachi amewaeleza Wananchi aliozungumza nao kwamba wakajiandikishe ili wachague viongozi wao yaani Wenyeviti wa Vijiji, Vitongoji/ Mitaa, pampja na Wajumbe wa Serikali hizo ili waweze kuwaletea maendeleo wanayoyataka.

Zoezi la Kuhamasisha Wananchi kuhusu Kujiandikisha limefanyika leo tarehe 16.10.2024 katika Mitaa na Vijiji Mbalimbali katika Wilaya ya Urambo.

Aidha DC Mkanachi amesema kwamba Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Kipalata (Kitambulisho cha Mpiga Kura) hakitotumika bali Wapiga kura wanajiandikisha/ kujiorodhesha kwenye Daftari la orodha ya wapiga kura ili kupata kibali cha kuchagua viongozi.

Amewasisitiza Wananchi kujiandikisha kila mtu kwenye Kitongoji chake ili achague kuongozi kutoka katika kitongoji/ Mtaa anaotoka Mwananchi.

Mhe. Mkuu wa Wilaya ya Urambo Dkt. Khamis Athumani Mkanachi pia amepita katika maeneo ya makazi na Biashara za Wananchi huku akizungumzia umuhimu wa Kujiandikisha lengo kuu likiwa ni kuwa Kila mwananchi wa Urambo ashiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024.

Pamoja na hayo amesisitiza kwamba Kipalata(Kadi ya Mpiga Kura) itatumika kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu ambapo Wananchi watawachagua Waheshimiwa Madiwani, Waheshimiwa Wabunge na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 2025.

Hivyo basi kila Mwananchi atumie muda huu uliobaki kwa ajili ya kujiandikisha ili kupata haki ya kuchagua viongozi ifikapo Novemba 27.2024.

Mkuu wa Wilaya Dkt. Khamis Mkanachi amesema Serikali za Mitaa ni viongozi ambao tunaishi nao kwenye maeneo yetu na ni vyema kufanya uchaguzi sahihi.

"Serikali za Mitaa, Sauti ya Wananchi, Jitokeze kushiriki Uchaguzi"





@

DC NA DED URAMBO WAJIANDIKISHA KWENYE DAFTARI LA MAKAZI KITONGOJI CHA SHIMONI.Mapema leo tarehe 12.10.2024 Mkuu wa Wilay...
12/10/2024

DC NA DED URAMBO WAJIANDIKISHA KWENYE DAFTARI LA MAKAZI KITONGOJI CHA SHIMONI.

Mapema leo tarehe 12.10.2024 Mkuu wa Wilaya ya Urambo Mhe. Dkt. Khamis A. Mkanachi aliambatana Kamati ya Ulinzi na Usalama na Mkurugenzi Mtendaji ambaye pia ni Msimamizi Mkuu wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa Halmashauri ya Wilaya ya Urambo Bi. Grace Quintine na kujiandikisha katika daftari la orodha ya wapiga kura ikiwa ni maamdalizi kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika tarehe 27.11.2024.

Aidha baada ya Kujiandikisha Mhe.Dkt Mkanachi amepata fursa ya kuzungumza na Wananchi waliojitokeza kujiandikisha nakuwaasa kwamba kila mtu awe balozi wa Mwenzake na jirani yake kuhamasisha watu kujitokeza kwenye zoezi hili Muhimu.

Amesisitiza kuwa kujiandikisha ndiyo kigezo cha kupiga kura hivyo basi kila Raia mwenye Sifa ya kujiandikisha afike kwenye kituo cha kujiandikisha kwenye kitongoji chake ajiorotheshe kwenye Daftari la Makazi.

Dkt. Mkanachi amehimiza wananchi wa Urambo kujitokeza kwa Wingi kujiandikisha ili kuweza kufikia lengo la wapiga kura zaidi ya 104,500 wanaopaswa kujiandikisha katika Daftari hilo.

Aidha Mhe. Dkt. Mkanachi amewaomba viongozi wa vyama vya Siasa Urambo kushiriki kikamilifu kuwahamasisha wananchi kujiandikisha kwa maslahi mapana ya Wilaya ili wapate fursa ya kuchagua viongozi wanaowaona wao wanafaa kuliko kuchaguliwa na wachache.

Ikumbukwe kuwa zoezi la kujiandikisha katika daftari la Orodha ya wapiga kura kwa ajili ya uchaguzi wa Serikali za Mitwa litafanyika kuanzia tarehe 11.10.2024 na kutamatika ifikapo tarehe 20.10.2024 ili Watanzania wote walenye vigezo vya kujiandikisha waweze kupata haki yao ya kikatiba ya kumchagua kiongozi wanayemtaka katika uchaguzi wa Serikali za mitaa.

Kwa upande wake Msimamizi Mkuu wa Uchaguzi ambaye pia Mkurugenzi Mtendaji Bi.Grace Quintine amesema zoezi linaenda vizuri nakusisitiza wananchi wasisubiri siku za mwisho ili kuepuka usumbufu bali watumie siku hizi za Mwanzo kujiandikisha.

"Serikali za Mitaa, Sauti ya Wananchi, Jitokeze kushiriki Uchaguzi"



MATOKEO YA USAILI WA VIJANA WALIOOMBA NAFASI KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA JKT 2024 WILAYA YA URAMBO, HATUA INAYOFU...
10/10/2024

MATOKEO YA USAILI WA VIJANA WALIOOMBA NAFASI KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA JKT 2024 WILAYA YA URAMBO, HATUA INAYOFUATA NI NGAZI YA MKOA.

WACHEZESHA MICHEZO YA KUBAHATISHA MAFURUKU KUINGIA NDANI YA MNADA WILAYANI URAMBO.Mkuu wa Wilaya ya Urambo Dkt.Khamis At...
10/10/2024

WACHEZESHA MICHEZO YA KUBAHATISHA MAFURUKU KUINGIA NDANI YA MNADA WILAYANI URAMBO.

Mkuu wa Wilaya ya Urambo Dkt.Khamis Athumani Mkanachi ameagiza kwamba wachezesha michezo ya kubahatisha ( Betting) wasiingie ndani ya mnada Wilayani Urambo bali wafanyie shughuli zao nje ya Mnada.

DC Mkanachi ametoa kauli hiyo leo ofisini kwake Tarehe 10.10.2024 wakati akizungumza na Wafanyabiashara wa Mifugo waliofika kwake kulalamika kughaiwa na wachezesha Michezo ya Kubahatisha Minadani.

Aidha Dkt Khamis Mkanachi amewataka wafanyabiashara hao kufanya biashara na kuepukana na michezo ya kubahatisha kwani hakuna aliyefanikiwa kwa kucheza michezo hiyo zaidi ya kufilisika.

Hata hivyo DC Dkt.Mkanachi amesema Serikali ya Wilaya itafuatilia kwa kila hatua kuona namna bora zaidi kwa sasa hawataingia kwenye uzio wa mnada bali watafanya Michezo yao nje ya mnada na k**a kuna mtu atawafuata nje na kucheza itakuwa ni jukumu lake kwani kazi ya Serikali ni kuwalinda raia na mali zao.

08/10/2024
Taarifa kwa Umma!
08/10/2024

Taarifa kwa Umma!

TUBADILISHE FIKRA ZETU TUTUMIE FURSA ZILIZOPO AMAZO ZINATOLEWA NA SERIKALI.TK MOVEMENT WAFUNDWA.
06/10/2024

TUBADILISHE FIKRA ZETU TUTUMIE FURSA ZILIZOPO AMAZO ZINATOLEWA NA SERIKALI.

TK MOVEMENT WAFUNDWA.

Katibu Tarafa wa Tarafa ya Urambo Ndugu Hamadi Muya kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Urambo ametoa Pongezi nyingi Idara ya...
04/10/2024

Katibu Tarafa wa Tarafa ya Urambo Ndugu Hamadi Muya kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Urambo ametoa Pongezi nyingi Idara ya Elimu Msingi na Sekondari Wilayani Urambo kwa Juhudi kubwa zinazofanyika kuhakikisha elimu ya Watu wazima inaendelea.

Ndugu Hamadi Muya ametoa Pongezi hizo katika maadhimisha ya Wiki ya Elimu ya Watu wazima ambapo kiwilaya imefanyika leo katika Viwanja vya Mwananchi Square Urambo tarehe 04.10.2024 yenye kauli mbiu isemayo ""UJUMUISHI KATIKA ELIMU BILA KIKOMO KWA UJUZI, USTAHIMILIVU, AMANI, NA MAENDELEO"

Ndugu Hamadi Muya amewapongeza wote wakiwemo Wajasiriamali, waalimu wa Elimu ya watu wazima, Wanafunzi kwani imeonekana kuna Wanannchi wengi hawajui kusoma na kuandika.

Hivyo ameendelea kuishauri Idara ya Elimu Halmashauri ya Wilaya ya Urambo kuhakikisha watoto wanasoma vyema na kwa waliochelewa kuanza ni vyema wakaanza kusomwa elimu ya watu wazima.

Kwa upande wake Afisa Elimu Sekondari Halmashauri ya Wilaya ya Urambo Mwalimu Sarah amesema mpango wa Serikali ni kuweka mazingira salama kwa watoto ili watoto wote wasome asikosekane hata moja kukosa Elimu.

"Serikali za Mitaa, Sauti ya Wananchi, Jitokeze kushiriki Uchaguzi"



Address

Urambo

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Urambo posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share