24/04/2023
*Taarifa Kutoka Ofisi ya Mbunge Jimbo la Rungwe 24/04/2023*
*ISYONJE-ISONGOLE*
Katibu wa Mbunge Jimbo la Rungwe Gabriel Mwakagenda amemwakilisha Mbunge wa Jimbo la Rungwe *Mhe; Anton Mwantona* kwenye hafla ya Uzinduzi wa *Zahanati ya Kijiji Cha Isyonje* Kata ya *Isongole*.
Zahanati hiyo iliyoanzishwa kwa nguvu za Wananchi imezinduliwa Leo na Mkuu wa Wilaya ya Rungwe *Mhe; Jaffar Haniu* kufuatia michango ya wadau Mbalimbali wa Maendeleo, Kisha Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kutoa Fedha za ukamilishaji pamoja na Vifaa Tiba.
Akitoa salam za Mhe; Mbunge; Katibu amesema katika kuunga Mkono Juhudi za wananchi wa Isyonje katika kufanikisha Ujenzi wa Zahanati hiyo Mhe; Mbunge alijitolea *Madirisha (Alminium) 18 yenye thamani ya Tsh 6,200,000* pamoja na gharama za kufunga ikiwa ni Ahadi aliyoitoa wakati wa Kampeni za Uchaguzi mwaka 2020.
Pia Katibu amewasihi Wananchi kuendelea kujitolea na kushiriki katika shughuli Mbalimbali za Maendeleo huku wakiendelea kuiunga Mkono Serikali inayoongozwa na Mhe; Rais wetu *Dkt; Samia Suluhu Hassan* ili kufanikisha lengo la Serikali katika kusogeza Huduma za kijamii karibu na Wananchi.
* #*