Taasisi ya Nyaraka na Kumbukumbu Zanzibar

Taasisi ya Nyaraka na Kumbukumbu Zanzibar Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Taasisi ya Nyaraka na Kumbukumbu Zanzibar, Government Organization, Kilimani, Zanzibar, Stone Town.

Katika kuadhimisha Juma la Nyaraka , Taasisi ya Nyaraka na Kumbukumbu Zanzibar imeandaa Jukwaa la Nyaraka lililowakutani...
04/06/2026

Katika kuadhimisha Juma la Nyaraka , Taasisi ya Nyaraka na Kumbukumbu Zanzibar imeandaa Jukwaa la Nyaraka lililowakutanisha wataalamu mbalimbali kujadili nafasi ya nyaraka na kumbukumbu katika kuimarisha uwajibikaji, haki za wananchi na utawala bora.

Jukwaa hilo ni miongoni mwa matukio muhimu ya wiki ya maadhimisho, likilenga kuongeza uelewa kuhusu mchango wa nyaraka katika maendeleo ya jamii.

Jopo la majadiliano liliwahusisha Moza Z. Mohamed -Mkuu wa Idara ya Nyaraka na kumbukumbu, Fuad A. Mohamed - Mkuu Idara ya kumbukumbu tuli, Anwar Yunus Yahya- Mkuu wa kitengo cha sheria pamoja na Afisa kumbukumbu Ndg Zainab Hassan kutoka Arahma Hospital.

Wataalamu hao wamejadili kwa kina umuhimu wa nyaraka katika utoaji wa ushahidi wa kisheria, kulinda haki za wananchi na kuimarisha uwajibikaji.

Aidha, walisisitiza umuhimu wa kuimarisha mifumo ya usimamizi wa kumbukumbu ili kuhakikisha upatikanaji wa taarifa sahihi na za kuaminika kwa wakati.



TAASISI YA NYARAKA NA KUMBUKUMBU ZANZIBAR YAPOKEA UGENI KUTOKA ALGERIATaasisi ya Nyaraka na Kumbukumbu Zanzibar imepokea...
03/06/2026

TAASISI YA NYARAKA NA KUMBUKUMBU ZANZIBAR YAPOKEA UGENI KUTOKA ALGERIA

Taasisi ya Nyaraka na Kumbukumbu Zanzibar imepokea ugeni kutoka Kurugenzi ya Nyaraka za Taifa ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Algeria kwa lengo la kubadilishana uzoefu na kuimarisha ushirikiano katika masuala ya usimamizi wa nyaraka na kumbukumbu.

Ujumbe huo ulijumuisha Bw. Rida Ben Laksira (Mkurugenzi wa Uboreshaji na Uhaulishaji wa Nyaraka Kidijitali), Bw. Zakaria Alfarouk Guettouch (Naibu Mkurugenzi wa Ushirikiano), Bi. Djouhra Malek (Naibu Mkurugenzi wa Teknolojia za Usimamizi wa Nyaraka) na Bi. Samia Ben Ali (Mhifadhi Mkuu wa Nyaraka).

Ujumbe huo uliambatana na viongozi kutoka Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa Tanzania, akiwemo Bw. Firimin Mbua Msiangi, Mkurugenzi Mkuu wa Idara hiyo, pamoja na Bw. Gasper J. Kileo, Mkurugenzi wa Usimamizi wa Nyaraka.

Aidha wageni walipata fursa ya kujionea shughuli na huduma mbalimbali zinazotekelezwa na Taasisi, ikiwemo ukusanyaji, uhifadhi, uhaulishaji na uhuishaji wa nyaraka za kihistoria na za kiutawala.

Aidha, ujumbe huo ulipongeza juhudi zinazofanywa na Taasisi katika ukusanyaji, uhifadhi na uchambuzi wa nyaraka pamoja na matumizi ya mifumo ya kisasa katika usimamizi wa kumbukumbu. Pia jube huo ulisisitiza umuhimu wa kuendelea kuharakisha mchakato wa uhaulishaji wa nyaraka ili kuongeza upatikanaji na matumizi yake kwa kizazi cha sasa na kijacho.

Taasisi ya Nyaraka na Kumbukumbu Zanzibar itaendelea kuthamini na kuimarisha ushirikiano wa kitaaluma na taasisi mbalimbali za ndani na nje ya nchi kwa lengo la kuendeleza sekta ya nyaraka na kumbukumbu.

Taasisi ya Nyaraka na Kumbukumbu Zanzibar itawakutanisha wadau mbalimbali kwa ajili yaΒ  majadiliano kuhusu umuhimu wa ny...
02/06/2026

Taasisi ya Nyaraka na Kumbukumbu Zanzibar itawakutanisha wadau mbalimbali kwa ajili yaΒ  majadiliano kuhusu umuhimu wa nyaraka na kumbukumbu katika haki, utamaduni hiatoria na maendeleo ya jamii.

Mada kuu ya Jukwaa la Nyaraka ni: "Umuhimu wa Nyaraka katika Uwajibikaji na Haki."

πŸ—“οΈ 03 Juni 2026
πŸ•˜ Saa 3:00 Asubuhi
πŸ“ Taasisi ya Nyaraka na Kumbukumbu Zanzibar

02/06/2026
MKUTANO NA WAANDISHI WA HABARI.
01/06/2026

MKUTANO NA WAANDISHI WA HABARI.

29/05/2026

Katika kuadhimisha Juma la Nyaraka, Taasisi ya Nyaraka na Kumbukumbu Zanzibar inavikaribisha vyuo na taasisi za sheria kushiriki katika maonesho maalum ya nyaraka za kisheria yatakayofanyika katika Taasisi ya Nyaraka na Kumbukumbu Zanzibar.

Kupitia video hii, Mkuu wa Kitengo cha Sheria, Ndugu Anwar Yunus Yahya, anatoa mwaliko rasmi kwa wadau wa sekta ya sheria kuhudhuria maonesho hayo yatakayowawezesha washiriki kujionea nyaraka mbalimbali za kisheria zenye thamani ya kihistoria na kitaaluma katika maendeleo ya sheria, utawala na uhifadhi wa kumbukumbu Zanzibar.

Maonesho haya yanalenga kuimarisha uelewa kuhusu umuhimu wa nyaraka za kisheria katika kuhifadhi historia ya taifa pamoja na kuimarisha misingi ya utawala bora na utoaji wa haki.

πŸ“ Taasisi ya Nyaraka na Kumbukumbu Zanzibar
πŸ“… 8 Juni 2026
⏰ Asubuhi

29/05/2026

The Zanzibar Institute of Archives and Records warmly invites the public to attend the World Archives Day Celebrations on 9 June 2026 at the Peace Memorial Museum, Mnazi Mmoja – Zanzibar.

This year’s celebrations will feature a special exhibition of rare Islamic and Arabic manuscripts preserved in Zanzibar, offering visitors a unique opportunity to witness historical handwritten documents that reflect the rich religious, educational, and cultural heritage of the Zanzibar community.

The event will also include the performance of: -
β€’ Traditional Maulid (maulid ya homu)
β€’ Zikr sessions
β€’ Traditional foods and their medicinal value and more traditional culture tents.

This exhibition is organized in collaboration with the Museum of Cultural History, University of Oslo, the University of Bergen, and the Royal Norwegian Embassy in Dar es Salaam.

Join us in celebrating and preserving our documentary heritage for future generations.
πŸ“ Peace Memorial Museum, Mnazi Mmoja – Zanzibar
πŸ“… 9 June 2026

CulturalHeritage DocumentaryHeritage

Bodi na Wafanyakazi wa Taasisi ya Nyaraka na Kumbukumbu Zanzibar inawatakia wote kheri na baraka za Eid el Adhaa..
26/05/2026

Bodi na Wafanyakazi wa Taasisi ya Nyaraka na Kumbukumbu Zanzibar inawatakia wote kheri na baraka za Eid el Adhaa..

Taasisi ya Nyaraka na Kumbukumbu Zanzibar imepokea ugeni kutoka Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere (The Mwalimu Nyer...
18/05/2026

Taasisi ya Nyaraka na Kumbukumbu Zanzibar imepokea ugeni kutoka Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere (The Mwalimu Nyerere Memorial Academy) , katika ziara iliyolenga kutangaza na kutoa maelezo kuhusu programu mbalimbali zinazotolewa na chuo hicho katika ngazi za Cheti (Certificate), Stashahada (Diploma), Shahada (Degree) pamoja na Shahada ya Uzamili (Master).

Ugeni huo uliongozwa na Afisa Udahili, Mr. Sharif Othman Juma, akifuatana na Bw. Frank Akile kutoka Kitengo cha Uhusiano pamoja na Bi. Zaituni Tawakal** kutoka Idara ya Utawala. Walieleza kuhusu fursa mbalimbali za masomo zinazotolewa na chuo hicho, taratibu za udahili pamoja na mchango wa chuo katika kuendeleza elimu bora na kukuza maendeleo ya taifa.

Aidha, wafanyakazi wa Taasisi waliohudhuria kikao hicho walipata fursa ya kuuliza maswali mbalimbali yaliyohusiana na programu za masomo, sifa za kujiunga pamoja na huduma zinazotolewa na chuo hicho.

Taasisi ya Nyaraka na Kumbukumbu Zanzibar inathamini ushirikiano huu na itaendelea kushirikiana na taasisi mbalimbali za elimu kwa lengo la kukuza maarifa na kuimarisha huduma kwa jamii.



Ijumaa kareem
08/05/2026

Ijumaa kareem

Address

Kilimani, Zanzibar
Stone Town

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Taasisi ya Nyaraka na Kumbukumbu Zanzibar posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share