04/06/2026
Katika kuadhimisha Juma la Nyaraka , Taasisi ya Nyaraka na Kumbukumbu Zanzibar imeandaa Jukwaa la Nyaraka lililowakutanisha wataalamu mbalimbali kujadili nafasi ya nyaraka na kumbukumbu katika kuimarisha uwajibikaji, haki za wananchi na utawala bora.
Jukwaa hilo ni miongoni mwa matukio muhimu ya wiki ya maadhimisho, likilenga kuongeza uelewa kuhusu mchango wa nyaraka katika maendeleo ya jamii.
Jopo la majadiliano liliwahusisha Moza Z. Mohamed -Mkuu wa Idara ya Nyaraka na kumbukumbu, Fuad A. Mohamed - Mkuu Idara ya kumbukumbu tuli, Anwar Yunus Yahya- Mkuu wa kitengo cha sheria pamoja na Afisa kumbukumbu Ndg Zainab Hassan kutoka Arahma Hospital.
Wataalamu hao wamejadili kwa kina umuhimu wa nyaraka katika utoaji wa ushahidi wa kisheria, kulinda haki za wananchi na kuimarisha uwajibikaji.
Aidha, walisisitiza umuhimu wa kuimarisha mifumo ya usimamizi wa kumbukumbu ili kuhakikisha upatikanaji wa taarifa sahihi na za kuaminika kwa wakati.