Kampuni ya Meli Tanzania

Kampuni ya Meli Tanzania KAMPUNI YA MELI TANZANIA (TASHICO) ilijulikana k**a MSCL ilianzishwa rasmi tarehe 8/12/1997 baada ya kutenganishwa kutoka katika shirika la reli nchini(TRC).

TASHICO ni Kampuni ya Serikali inayosafirisha abiria na mizigo katika Maziwa Makuu.

27/05/2026
25/05/2026
Ziara ya Naibu Waziri wa Mambo ya Nje Makao Makuu ya TASHICO - Mwanza.  Kampuni ya Meli Tanzania (TASHICO) Jumatano ya M...
20/05/2026

Ziara ya Naibu Waziri wa Mambo ya Nje Makao Makuu ya TASHICO - Mwanza.


Kampuni ya Meli Tanzania (TASHICO) Jumatano ya Mei 20,2026 imepokea ugeni wa ziara ya Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. James Kinyasi Millya.

Ugeni huo ulipokelewa jijini Mwanza na Mkurugenzi Mtendaji wa TASHICO, Ndg. Eric Benedict Hamissi, pamoja na menejimenti ya TASHICO katika Ofisi zilizopo eneo la Bandari ya Mwanza Kaskazini.

Mhe. Millya aliambatana na viongozi waandamizi akiwepo Balozi Saidi Shaibu M***a ambaye ni Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki , pamoja na Mhandisi Abdillah Mataka ambaye ni Mkurugenzi wa Uchumi, Miundombinu na Huduma za Kijamii.

Awali, Mkurugenzi Mtendaji wa TASHICO Ndg. Eric Hamissi alitoa maelezo mafupi kuhusu Kampuni akisema kuwa TASHICO kuwa na meli zinazounganisha Tanzania na mataifa mengine ni ashirio la moja kwa moja la uhitaji wa msaada wa Wizara ya mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki katika mukhtadha wa uhusiano na urahisi wa msaada kwa meli za Serikali pindi zinapo kuwa nje ya nchi.

Miongoni mwa meli hizo ni MV New Mwanza Meli mpya yenye sifa zote zinazostahili katika ukanda wa maziwa yote makuu.

"Tunaona ni fursa kutembelewa na timu hii inayoongozwa na Mhe. Naibu Waziri, sisi TASHICO kupitia meli zetu zinazo kwenda nje ya nchi , kwetu fursa hii ni muhimu sana kupenyeza mambo ambayo tunaona yanaweza kurahisisha katika baadhi ya maeneo ambayo yana changamoto kidogo katika utoaji huduma zetu tunapokuwa nje ya nchi" - Alisema Eric .

Kwa upande wake Naibu Waziri Mhe. Millya ameelekeza kuundwa kwa timu ndogo ya uwakilishi wa taasisi husika za Tanzania ili kuzungumza na wahusika katika nchi jirani kupitia Wizara hii ambayo itakuwa ni kiungo cha mazungumzo hayo.

Aidha amampongeza Mkurugenzi Mtendaji wa TASHICO Ndg Eric Benedict Hamissi kwa maelezo yake mazuri yanayo onyesha uhusika na usimamizi mzuri wa malengo ya Serikali lakini maono yake kuhusu Kampuni yanayoonyesha picha na taswira nzuri ya mafanikio ya TASHICO na Serikali kwa ujumla.

13/05/2026

BAJETI YA WIZARA YA UCHUKUZI BUNGENI DODODMA
Leo tarehe 13 Mei 2026

SERIKALI YATENGA SHILINGI BILIONI 171 KUTEKELEZA MIRADI YA TASHICO Serikali kupitia Wizara ya Uchukuzi imetenga jumla ya...
13/05/2026

SERIKALI YATENGA SHILINGI BILIONI 171 KUTEKELEZA MIRADI YA TASHICO

Serikali kupitia Wizara ya Uchukuzi imetenga jumla ya Shilingi bilioni 171 katika mwaka wa fedha 2026/27 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya ujenzi na ukarabati wa meli chini ya Kampuni ya Meli Tanzania (TASHICO).

Akisoma Bajeti ya Wizara ya Uchukuzi bungeni mjini Dodoma leo tarehe 13.5.2026, Waziri wa Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa alisema kuwa fedha hizo zitatumika kuimarisha usafiri wa njia ya maji katika maziwa makuu pamoja na kuongeza uwezo wa biashara na usafirishaji nchini.

"Fedha hizo zitaelekezwa katika utekelezaji wa miradi mikubwa ikiwemo ujenzi wa meli mpya ya mizigo yenye uwezo wa kubeba tani 3,500 katika Ziwa Tanganyika pamoja na kuanza ujenzi wa meli mbili za mafuta zenye uwezo wa kubeba lita 600,000 kila moja katika ziwa hilo," Prof. Mbarawa alisema

Aidha, Serikali imepanga kuanza ujenzi wa meli mpya yenye uwezo wa kubeba abiria 600 na mizigo tani 400 katika Ziwa Tanganyika pamoja na meli mpya ya mizigo yenye uwezo wa kubeba tani 3,000 katika Ziwa Victoria.

Katika hatua nyingine, Serikali itaendelea kukamilisha upembuzi yakinifu utakaoiwezesha TASHICO kufanya biashara katika Bahari ya Hindi. Sambamba na hilo, Serikali imepanga kuendelea na ujenzi wa kiwanda cha kujengea meli katika Ziwa Tanganyika chenye uwezo wa kuhudumia meli zenye uzito wa tani 5,000.

Prof. Mbarawa alieleza kuwa miradi mingine itakayotekelezwa ni pamoja na ukarabati mkubwa wa meli ya MV. Mwongozo na kumalizia ukarabati wa meli ya MV. Liemba katika Ziwa Tanganyika ambayo ina asilimia 70 ya utekelezaji.

Pia, Serikali itaendelea na ukarabati wa meli za MT. Nyangumi na MV. Clarias katika Ziwa Victoria pamoja na ununuzi wa mabehewa ya kubeba mizigo kwa ajili ya meli ya MV. Umoja.

Miradi mingine iliyotajwa ni pamoja na ununuzi wa boti za uokoaji katika maziwa makuu, uboreshaji wa mifumo ya TEHAMA kwa ajili ya ukusanyaji wa mapato na ukarabati wa meli ya MV. Songea inayohudumia Ziwa Nyasa.

Hatua hiyo inaelezwa kuwa sehemu ya jitihada za Serikali za kuimarisha sekta ya usafiri wa majini nchini, kuongeza usalama wa usafiri na kuchochea ukuaji wa biashara na uchumi kupitia usafirishaji wa majini.

NI LEO HII 13.5.2026. USIKOSE
13/05/2026

NI LEO HII 13.5.2026. USIKOSE

Alhamisi hii ya Mei 14,2025 meli ya MV New Mwanza itakuwa kwenye mzunguko wa ratiba za meli kutoka Mwanza kwenda Bukoba ...
12/05/2026

Alhamisi hii ya Mei 14,2025 meli ya MV New Mwanza itakuwa kwenye mzunguko wa ratiba za meli kutoka Mwanza kwenda Bukoba na kurudi.

MV New Mwanza itasafiri badala ya meli ya MV Victoria ikiwa ni muendelezo wa ratiba za safari za meli kutoka Mwanza kwenda Bukoba.

Muda wa kuondoka ni saa 3: 00 usiku kutoka Bandari ya Mwanza Kusini kupitia Kemondo.

Bajeti ya Wizara ya Uchukuzi itasomwa tarehe 13.05.2026
12/05/2026

Bajeti ya Wizara ya Uchukuzi itasomwa tarehe 13.05.2026

Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Meli Tanzania (TASHICO) Mej. Jen (Mstaafu) John Julius Mbungo leo amefanya mazungumzo n...
04/05/2026

Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Meli Tanzania (TASHICO) Mej. Jen (Mstaafu) John Julius Mbungo leo amefanya mazungumzo na Mwenyekiti wa Bodi ya Lignes Maritimes Congolaises SA (LMC) Mhe. Mende Omalanga Lambert jijini Kinshasa, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), ikiwa ni sehemu ya ziara rasmi ya kikazi ya TASHICO nchini humo.

Mazungumzo hayo yaliyohudhuriwa na Mkurugenzi Mtendaji wa TASHICO Ndg Eric B Hamissi, Katibu Mtendaji wa Wakala wa Uwekezaji Usafirishaji Ushoroba wa Kati (CCTTFA) Wakili Flory Okandju na Balozi wa Tanzania nchini DRC Mhe. Said Juma Mshana, yalilenga kuimarisha ushirikiano wa kimkakati kati ya taasisi hizi mbili za serikali katika sekta ya usafirishaji wa njia ya maji hususan katika kukuza biashara ya kikanda na kuongeza ufanisi wa huduma za usafiri kati ya Afrika Mashariki, Kati na Ukanda wa Maziwa Makuu.

Ziara hii inatarajiwa kuhitimishwa kwa kusainiwa kwa Hati ya Makubaliano (Memorandum of Understanding - MoU) kati ya TASHICO na LMC, ambayo itaweka msingi wa ushirikiano katika maeneo muhimu ikiwemo uendeshaji wa pamoja wa meli, kubadilishana uzoefu wa kitaalam, maendeleo ya biashara ya mizigo kwenye Bahari ya Hindi pamoja na Ziwa Tanganyika, na kuimarisha mnyororo wa usafirishaji kwa faida ya nchi zetu na Ukanda wa Maziwa Makuu.

Ushirikiano huu ni hatua muhimu katika kufungua fursa mpya za biashara, kuongeza ushindani wa bandari zetu, na kuifanya Tanzania kuwa lango kuu la usafirishaji katika ukanda huu.

RegionalIntegration

Address

Tanzania Shipping Company Ltd
Mwanza
33000

Opening Hours

Monday 07:30 - 17:30
Tuesday 07:30 - 17:30
Wednesday 07:30 - 17:30
Thursday 07:30 - 17:30
Friday 07:30 - 17:30
Saturday 07:30 - 17:30
Sunday 07:30 - 17:30

Telephone

+255739606600

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kampuni ya Meli Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Kampuni ya Meli Tanzania:

Share