08/10/2020
UHAMILISHAJI WA NGURUWE (PIG ARTIFICIAL INSEMINATION) ni njia ya kisasa ya kuboresha wanyama wako (nguruwe) kwa kuwapandisha na mbegu za kisasa zaidi kwa kutumia teknolojia ya mirija.
Hii ni njia mbadala na rahisi kwa wewe (mfugaji) kupandisha wanyama wako bila kuhitaji kumiliki madume (BOARS) shambani kwako. Unaweza kutumia njia hii kupandisha wanyama wengi kwa wakati mmoja bila uwepo wa dume la kupanda.
Zaidi ya hapo, inakupa wewe mfugaji uwezo wa kuchagua mbegu za dume unayetaka kulingana na mahitaji ya mradi wako.
Njia hii imekuwa inatumika kwa wanyama k**a “NGOMBE, MBUZI, KONDOO NA MBWA” na imeleta mafanikio makubwa sana hapa nchini na hata nchi zilizoendelea.
*FAIDA ZA UHAMILISHAJI*
1. URAHISI
Uhamilishaji unakurahisishia wewe mfugaji kupandisha wanyama wengi kwa mara moja bila kuhitaji madume wengi. Mchakato huu hutumia muda mfupi na nguvu chache ukilingianisha na matumizi ya dume la mbegu amabayo huhitaji matumizi ya muda na nguvu nyingi.
2. UPATIKANAJI WA MBEGU BORA.
Mfugaji anaweza kupata mbegu bora muda wowote pale atakapohitaji.
3. UWEZO WA KUCHAGUA MBEGU
Matumizi ya uhamilishaji unakupa nafasi wewe mfugaji kuchagua mbegu bora na ambayo unahitaji kwa malengo husika. Mara kwa mara, mfugaji huhitaji kujaribu mbegu tofauti tofauti na hii huwa ngumu au ya gharama k**a utakuwa unamiliki madume yote. Mbegu za mirija zinakupa uwezo wewe mfugaji kuwa na uchaguzi wa mbegu za aina mbalimbali.
4. GHARAMA NAFUU
Uhamilishaji ni njia nafuu sana kifedha kwa wafugaji wadogo wadogo wanaotaka kuanza kufuga kisasa na kukuza mradi wao wa nguruwe.
Mchakato huu unapunguza uhitaji wa kununua na kumiliki dume la mbegu la kisasa ambao huuzwa kwa bei kubwa, ukizingatia kwamba dume huyo hutumika mara chache sana.
5. MAGONJWA
Pale unapoingiza nguruwe mgeni (iwe dume au jike) kwenye shamba lako, unahatarisha sana wanyama wako kwani mnyama huyo huweza kuja na magonjwa ambayo yanaweza kuambukiza shamba lako zima. Matumizi ya uhamilishaji huepusha uwezekano wa kupatwa na magonjwa hayo yanayotoka shamba moja kwenda lingine.
K**a una maswali ya ziada, unaweza wasiliana basi kupitia:
[email protected]
+255-755-361-904