14/03/2025
Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mpanda inaendelea na zoezi la kugawa na kutoa vifaa vya maunganisho mapya ya huduma ya majisafi ambapo leo tarehe 14/3/2025 imekabidhi vifaa kwa wateja 51 ambao wamekamilisha malipo yao katika maeneo mbalimbali katika Manispaa ya Mpanda.
Aidha kupitia zoezi hilo elimu mbalimbali zimeendelea kutolewa ikiwemo utunzaji wa miundombinu ya maji, matumizi sahihi ya maji na njia rasmi za malipo ya kiserikali, njia za mawasiliano na huduma nyingine zitolewazo na Muwasa.
Kwa msaada wasiliana nasi kupitia namba ya huduma kwa wateja namba 0800110124 (Bure) MUWASA