BAHI DC

BAHI DC Tuna tekeleza ila ya chama cha mapinduzi kwa kuwatumikia wanachanchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

WILAYA YA BAHI YAPONGEZWA KWA UTEKELEZAJI MZURI WA MIRADI YA MAENDELEO‎‎Viongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2026 w...
03/06/2026

WILAYA YA BAHI YAPONGEZWA KWA UTEKELEZAJI MZURI WA MIRADI YA MAENDELEO

‎Viongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2026 wakiongozwa na Ndugu Wazo Michael Mwang'onda wameipongeza Wilaya ya Bahi kwa mafanikio makubwa katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo pamoja na kutekeleza maelekezo mbalimbali ya Serikali kwa ufanisi

‎Akizungumza wakati wa ziara ya Mwenge wa Uhuru wilayani humo , kiongozi wa mbio hizo amesema kuwa Wilaya ya Bahi imekuwa ya kwanza miongoni mwa Wilaya zote walizozitembelea kwa kufanikiwa kusajili vikundi vingi vya wananchi, ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan hatua ambayo imeonesha dhamira ya halmashauri katika kuwawezesha wananchi kiuchumi na kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo

‎Viongozi hao pia wamepongeza usimamizi mzuri wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa wilayani humo, wakisema miradi hiyo imekamilishwa kwa ubora na kuwahimiza wananchi kuendelea kushiriki katika miradi ya maendeleo ili kuunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan

‎Sambamba na hayo, viongozi wa Mwenge wa Uhuru wamesisitiza umuhimu wa kulinda amani na utulivu wa nchi, wakieleza kuwa amani ndiyo msingi wa maendeleo endelevu na ustawi wa wananchi

‎Katika hatua nyingine, wameipongeza Wilaya ya Bahi kwa kuhamasisha matumizi ya nishati safi na salama kwa vitendo na wamewataka wananchi kuacha ukataji holela wa miti unaochangia uharibifu wa mazingira na badala yake kutumia nishati safi na kuacha matumizi ya  mifuko ya lambo  ili kuhifadhi mazingira kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo

‎Vilevile, viongozi hao wamepongeza jitihada za halmashauri katika kusajili vikundi vingi vya wananchi na kufikia na kuvuka malengo yaliyowekwa na serikali Wamesema mafanikio hayo yameufurahisha Mwenge wa Uhuru na Serikali kwa ujumla, kwani yanaonesha utekelezaji mzuri wa maelekezo ya Serikali na dhamira ya kuwainua wananchi kiuchumi

‎Mwenge wa uhuru umetembelea, na kukagua Miradi 7 katika wilaya ya Bahi na kukabidhiwa na Kaimu mkuu wa wilaya ya Bahi Dkt. Sophia Kizigo ambaye ni mkuu wa wilaya ya Mpwapwa Tarehe 3 Juni 2026 katika wilaya ya Kondoa dc.

01/06/2026

VIJANA PLATFORM waukarikibisha Mwenge wa Uhuru Wilayani Bahi kupitia Ufunguzi wa kongamano la vijana

VIJANA PLATFORM WAMECHAFUA MJI WA BAHI.Vijana kwa umoja wao ujulikanao k**a "Vijana Platform" wamefanya jogging na kutan...
01/06/2026

VIJANA PLATFORM WAMECHAFUA MJI WA BAHI.

Vijana kwa umoja wao ujulikanao k**a "Vijana Platform" wamefanya jogging na kutanda ndani ya Mji wa Bahi kuonyesha bashasha yao na shauku ya ukaribisho wa Mwenge wa Uhuru Wilaya ya Bahi 02 Juni 2026.

‎VIJANA WAHIMIZWA KUWA WAZALENDO NA KUTUMIA FURSA ZA MAENDELEO‎‎Vijana wa Wilaya ya Bahi wamehimizwa kuwa wazalendo, kul...
01/06/2026

‎VIJANA WAHIMIZWA KUWA WAZALENDO NA KUTUMIA FURSA ZA MAENDELEO

‎Vijana wa Wilaya ya Bahi wamehimizwa kuwa wazalendo, kulinda amani na kutumia fursa mbalimbali za maendeleo zinazotolewa na Serikali ili kujikwamua kiuchumi na kuchangia maendeleo ya taifa

‎Wito huo umetolewa leo tarehe 1 Juni 2026 katika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi wakati wa Kongamano la Vijana na Uzinduzi wa Jukwaa la Vijana (Youth Platform) la Wilaya ya Bahi, lililowakutanisha vijana kutoka maeneo mbalimbali ya wilaya hiyo lililobeba kaulimbiu isemayo "Vijana Tuyajenge, Tanzania ni Yetu Sote", sambamba na kaulimbiu ya Mwenge wa Uhuru ya mwaka 2026 isemayo "Tanzania ni Yetu Sote, Tushik**ane kwa Pamoja Kuleta Maendeleo"

‎Akifungua kongamano hilo kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Afisa Maendeleo ya Jamii Bi. Jane Ng'ondi, amewataka Vijana kuzingatia Maadili ya Taifa, kuunda vikundi, kujisajili na kuanzisha miradi mbalimbali ili kunufaika na fursa zinazotolewa na Serikali

‎"Vijana ni kioo cha taifa letu, tujiepushe na vurugu kwani vurugu zinaharibu amani yetu , tulinde amani ya nchi yetu na tuwe wazalendo," alisema Bi. Ng'ondi

‎Aidha, Bw. Omari Abdullah Pumzi kutoka k**ati ya Vijana Wazalendo, alipokuwa akifafanua kuhusu Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Vijana, amewahimiza vijana kutumia Tekinolojia na mitandao ya kijamii kutafuta taarifa na fursa mbalimbali za maendeleo

‎"Wizara zote zinatutegemea sisi vijana Usigombane na watu wewe ng'ang'ania fursa, Fursa haikufuati nyumbani; ifuate mtandaoni, katika ofisi za maendeleo ya jamii na sehemu nyingine zinazotoa huduma za maendeleo," alisema Punai

‎Lengo la kongamano hilo lilikuwa kuchagua viongozi wa Jukwaa la Vijana la Wilaya ya Bahi na kuwawezesha vijana kutambua fursa mbalimbali zilizopo katika halmashauri likiambatana na mafunzo kuhusu elimu ya uraia na uzalendo, ujasiriamali, usimamizi wa biashara, elimu ya fedha, upatikanaji wa mikopo na fursa za uwezeshaji wa vijana, pamoja na ushiriki wa vijana katika shughuli za maendelo

Mada hizo zimewasilishwa na wataalamu kutoka taasisi mbalimbali akiwemo Dkt. Samson Msilu, Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo cha Serikali za Mitaa; CPSP Scholastica Nyabweke kutoka Hombolo(lgti)

31/05/2026
31/05/2026
25/05/2026

Tanzania ni yetu sote tushik**ane kwa pamoja kuleta maendeleo.

Address

Info@bahidc. Go. Tz
Dodoma
SLP2993

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00
Saturday 09:00 - 17:00
Sunday 09:00 - 17:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when BAHI DC posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to BAHI DC:

Shortcuts

Share