21/08/2026
ZIARA YA MHE: RIDHIWANI-TAKUKURU MOROGORO
Mhe. Ridhiwani Kikwete, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ameipongeza TAKUKURU kwa kazi nzuri na inayoendelea kuzitekeleza na kuipa taasisi heshima inayostahili.
Ameyasema hayo wakati wa ziara yake katika jengo jipya la Ofisi za TAKUKURU Mkoa wa Morogoro Agosti 20, 2026 ambapo pamoja na mambo mengine alizungumza na watumishi na kusisitiza yafuatayo:
📌Msingi mkubwa wa kazi zetu za kila siku ni kuhakikisha wananchi wanapata maendeleo wanayostahili bila kuwepo kwa vitendo vya rushwa, hivyo tufanye kazi kwa wekedi mkubwa.
📌Endeleeni kusimamia fedha mnazopewa za majengo ili thamani ya fedha izidi kuonekana.
📌Jitahidini kuzingatia muda katika chunguzi zenu, ni vizuri chunguzi zisichukue muda mrefu kukamilika.
📌Endeleeni kufanya kazi vizuri kwani Mhe: Dkt. Samia Suluhu Hasan, Raisxwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, anawategemea sana.
TAKUKURU - Morogoro Agosti 20, 2026