03/06/2026
Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) imechangia uzoefu wake katika mjadala wa kujenga Mfumo wa Mawasiliano ya Serikali wenye dira moja, sauti moja na uratibu wa pamoja kwenye "Dira2050", ikiwa ni sehemu ya Mkutano Mkuu wa Maafisa Mawasiliano wa Serikali unaofanyika jijini Mwanza.
Mkutano huo umefunguliwa rasmi tarehe 2 Juni 2026, na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mohamed Mtanda, na kuhudhuriwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa.
Akizungumza katika mkutano huo, Mwenyekiti wa Chama cha Maafisa Mawasiliano wa Serikali (TAGCO), Karim Meshaki, alieleza mipango ya chama hicho katika kuongeza weledi wa wanachama wake, kuimarisha mifumo ya uendeshaji wa shughuli za chama kupitia TEHAMA, pamoja na maandalizi ya utekelezaji wa mradi mkubwa wa ujenzi wa Makao Makuu ya TAGCO jijini Dodoma.
Katika mkutano huo, Sarah Reuben, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Hifadhi Hati - NIDA, alishiriki uzoefu wake katika sekta ya mawasiliano kupitia mada ya โOne Nation, One Vision: Building a Whole-of-Government Communication System for Vision 2050,โ ambapo alisisitiza umuhimu wa taarifa sahihi, uratibu wa pamoja na mawasiliano ya Serikali yanayomfikia mwananchi kwa wakati na kwa lugha inayoeleweka.
Kupitia ushiriki huo, NIDA imeonesha dhamira yake ya kuendelea kuboresha mawasiliano ya kitaasisi katika kuelimisha wananchi kuhusu usajili, utambuzi na matumizi ya Kitambulisho cha Taifa k**a nyenzo muhimu ya kupata huduma mbalimbali za kijamii na kiuchumi.