BRELA Tanzania

BRELA Tanzania The Business Registrations and Licensing Agency deals with Business Names,Trade Marks,Industrial License, and Patents.

BRELA is a Government Executive Agency established under the Government Executive Agencies Act No. 30 of 1997. It was established on the 28th of October, 1999 by Government Notice No. 294 A published on the 8th October, 1999 and it was officially inaugurated on the 3rd December, 1999. AIM, ROLE AND STRATEGIC OBJECTIVES

AIM
-The aim of the Agency is to ensure that businesses operate in accordance

with the laid down regulations and sound commercial principles. ROLES
-The specific roles include the following:
-To administer companies and business names laws.
-To regulate business by administering business and industrial licensing laws.
-To administer intellectual property laws.
-To encourage and facilitate local and foreign business investment.
-To stimulate scientific and technological inventiveness and innovation and encourage technology transfer.
-To protect the development of creativity in artistic, literary works, and expression of folklore by protecting such work in conjunction with rights owners. STRATEGIC OBJECTIVES
The Strategic Objectives of the agency are :
-Ensuring that businesses comply with the laid down regulations to the satisfaction of the Government and the business community.
-Improving service delivery by the adoption of modern business practices.
-Building an efficient and effective workforce by adopting modern Human Resource Management policies.
-Achieving financial self-sufficiency and generate surplus of income that supports the implementation of other strategic objectives.

WANAWAKE FANI YA SAYANSI, TEKNOLOJIA, UHANDISI NA HISABATI WASISITIZWA KULINDA BUNIFU ZAOWakala wa Usajili wa Biashara n...
10/06/2026

WANAWAKE FANI YA SAYANSI, TEKNOLOJIA, UHANDISI NA HISABATI WASISITIZWA KULINDA BUNIFU ZAO

Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) imeendelea kusisitiza umuhimu wa ulinzi wa Miliki Ubunifu kupitia ushirikiano na wanawake wa fani za Sayansi, Teknolojia, Uhandisi na Hisabati hatua inayolenga kuongeza uelewa kuhusu haki za Miliki Ubunifu ili kuhakikisha bunifu za watanzania zinalindwa, zinathaminiwa na zinachangia kikamilifu katika maendeleo ya jamii na kutatua changamoto zilizoizunguka jamii kwenye maisha yao ya kila siku.

Hayo yamebainishwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa BRELA, Bw. Godfrey Nyaisa leo tarehe 09 Juni 2026 wakati akifungua warsha ya Miliki Ubunifu kwa wanawake katika fani za Sayansi, Teknolojia, Uhandisi pamoja na Hisabati (STEM) iliyofanyika katika ukumbi wa Tume ya Ushindani jijini Dar es salaam.

Akizungumza katika hotuba yake, Bw. Nyaisa alisema kuwa warsha hiyo ni muendelezo wa utekelezaji wa mkakati wa BRELA kuwafikia wabunifu waka kada na fani zote ili kuwaelezea umuhimu wa ulinzi na ubiasharishaji wa bunifu zao.

“Kwa kutambua umuhimu wa fani za Sayansi, Teknolojia, Uhandisi na Hisabati katika uvumbuzi BRELA imeona ni vyema kuandaa warsha hii ili kuwapa ninyi nafasi ya kujifunza masuala ya Miliki Ubunifu pamoja na urasimishaji wa biashara zinazotokana na bunifu mnazozifanya,” alisema Bw. Nyaisa.

Awali akimkaribisha Afisa Mtendaji Mkuu Bw. Godfrey Nyaisa, Kaimu Mkurugenzi wa Miliki Ubunifu Bw. Seka Kasera alisema idadi ya wanawake katika fani za Sayansi, Teknolojia, Uandisi na Hisabati kwa sasa imezidi kuongezeka na kwamba warsha hiyo itasaidia wanawake wengi kwenye fani ya Sayansi, Teknolojia, Uhandisi na Hisabati kulinda bunifu zao.

Kwa upande wao baadhi ya washiriki wa warsha hiyo walieleza kuwa warsha hiyo imebadilisha kwa kiasi kikubwa mtazamo wao kuhusu masuala ya Miliki Ubunifu hasa kwenye kulinda kazi ambazo wanabuni kwenye kada yao ya STEM.

Pumzika kwa Amani 🕯️
08/06/2026

Pumzika kwa Amani 🕯️

“Bwana alitoa, na Bwana ametwaa; jina la Bwana lihimidiwe.” (Ayubu 1:21)
07/06/2026

“Bwana alitoa, na Bwana ametwaa; jina la Bwana lihimidiwe.” (Ayubu 1:21)

BRELA KUENDELEA KUWAELIMISHA WAJASIRIAMALI JUU YA ULINZI WA ALAMA ZA BIASHARANaibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. D...
05/06/2026

BRELA KUENDELEA KUWAELIMISHA WAJASIRIAMALI JUU YA ULINZI WA ALAMA ZA BIASHARA

Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dennis Londo, amesema kuwa Sheria ya Alama za Biashara na Huduma, Sura ya 326, inampa mmiliki wa alama ya biashara haki ya kipekee ya kuitumia na kumwezesha kuchukua hatua za kisheria dhidi ya mtu yeyote atakayeitumia bila idhini yake.

Mhe. Londo ameyasema hayo leo, Juni 5, 2026, Bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Janeth Mahawanga, ambaye alihoji hatua zinazochukuliwa na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) kulinda bidhaa za wanawake dhidi ya wizi wa nembo na mawazo ya ubunifu.

Amesema kuwa Wizara ya Viwanda na Biashara kupitia BRELA imeendelea kutoa elimu kwa wanawake wajasiriamali kuhusu umuhimu wa kulinda na kusajili bunifu zao. Kwa mwaka 2025 pekee, zaidi ya wanawake 1,000 walifikiwa kupitia mafunzo yaliyotolewa katika mikoa 13 ya Tanzania Bara ambayo ni Shinyanga, Morogoro, Songwe, Ruvuma, Lindi, Mtwara, Pwani, Dodoma, Geita, Simiyu, Manyara na Mara.

Aidha, ameeleza kuwa BRELA kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo ya Viwanda Vidogo (SIDO) imekuwa ikiendesha mafunzo kwa wajasiriamali nchini kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kulinda bunifu zao na kuwahamasisha kusajili alama za biashara ili kuimarisha ushindani wa bidhaa zao sokoni na kuzuia matumizi yasiyoidhinishwa ya alama hizo.

“BRELA imekuwa ikishiriki matukio mbalimbali k**a Sabasaba, NaneNane na maonesho ya taasisi mbalimbali kwa kutoa elimu kwa wajasiriamali katika maeneo tofauti ya nchi. Pia imekuwa ikitoa huduma za usajili hapo kwa papo, na shughuli hiyo imeendelea kufanyika katika maeneo mbalimbali nchini,” amesema Mhe. Londo.

Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), kwa kushirikiana na Shirika la Miliki Ubunifu Duniani (WIPO) na Taasisi...
01/06/2026

Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), kwa kushirikiana na Shirika la Miliki Ubunifu Duniani (WIPO) na Taasisi washirika imefanya uzinduzi wa Mradi wa upatikanaji wa teknolojia rahisi itakayotumika kutengeneza chakula cha mifugo na mbolea kwa kutumia mabaki ya chakula na zao la Parachichi leo, Juni 01, 2026, Jijini Dar es Salaam.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa Mradi huo, Mkurugenzi wa Miliki Ubunifu kutoka BRELA Bi. Loy Mhando, alieleza kuwa, BRELA inajukumu la kulinda Miliki Ubunifu nchini na imekuwa ikifanya kazi kwa karibu na Shirikika la Miliki Ubunifu Duniani (WIPO). Kupitia ushirikiano wa kimkakati, BRELA iliwasilisha ombi la kutafuta teknolojia sahihi na madhubuti itakayosaidia kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii nchini kutoka katika kanzidata ya WIPO ili ziweze kutumika kwa maendeleo katika jamii.

“BRELA ndio ofisi kiungo wa Miliki Ubunifu Tanzania Bara, na inafanya kazi kwa karibu na WIPO ambapo kutokana na ushirikiano huo tulifanya mawasiliano na tukaona umuhimu wa kwenda mbali zaidi ya kulinda Miliki Ubunifu kwa kuangalia ni namna gani tunatumia Miliki Ubunifu kwa maendeleo ya jamii, ndipo matokeo ya Mradi huu ambao unazinduliwa leo. Mradi huu unalenga kutafuta teknolojia rahisi itakayowezesha uzalishaji wa chakula cha mifugo na mbolea kwa kutumia mabaki ya vyakula” alisema Bi. Mhando.

Bi. Mhando alibainisha kuwa Mradi huo utaanza kutekelezwa kwa majaribio katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini ikihusisha mikoa ya Mbeya, Iringa, na Njombe kwa lengo la kuwanufaisha moja kwa moja wakulima na wafugaji nchini.

Aliendelea kusema kuwa mradi huu utatafuta na kuleta teknolojia ambayo itatumia mabaki ya vyakula kuzalisha bidhaa nyingine. Hatua hii haitainua tu jamii kiuchumi, bali pia itapunguza kwa kiasi kikubwa mzigo wa Serikali na wafanyabiashara kuagiza vyakula vya mifugo kutoka nje ya nchi.

BRELA YATOA MAFUNZO KUHUSU DHANA YA MILIKI MANUFAA ARUSHADhana ya Miliki Manufaa (Beneficial Ownership) iliyoanza kutumi...
30/05/2026

BRELA YATOA MAFUNZO KUHUSU DHANA YA MILIKI MANUFAA ARUSHA

Dhana ya Miliki Manufaa (Beneficial Ownership) iliyoanza kutumika rasmi mwaka 2022, imeendelea kuwa nguzo muhimu katika mfumo wa usajili wa kampuni nchini Tanzania, ikilenga kuongeza uwazi katika umiliki wa biashara na kudhibiti mianya ya utakatishaji fedha pamoja na udanganyifu wa kifedha.

Kwa mujibu wa Meneja wa Kampuni kutoka Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), Harvey Kombe, wakati wa mafunzo ya Miliki Manufaa yaliyofanyika jijini Arusha, alisema bado kuna changamoto kubwa ya usahihi wa taarifa zinazowasilishwa kwenye mfumo wa usajili wa kampuni. Alibainisha kuwa takribani asilimia 95 ya maombi yanayowasilishwa katika mfumo huo huwa na makosa, hali inayotokana na kutofuatwa kwa taratibu sahihi za ujazaji wa taarifa za miliki manufaa.

Katika mazingira hayo, imekuwa ikisisitizwa kuwa mawakili na wahasibu wana nafasi muhimu ya kuhakikisha taarifa za wamiliki halisi wa kampuni zinakaguliwa kwa umakini kabla ya kuwasilishwa, ili kupunguza kiwango cha makosa yanayojitokeza katika mfumo.

Mafunzo hayo hufanyika katika mikoa mbalimbali yenye shughuli kubwa za kiuchumi na mwitikio mkubwa wa usajili wa kampuni, ambapo Arusha ni miongoni mwa maeneo ambayo BRELA hupokea maombi mengi ya Miliki Manufaa.

Kwa ujumla, hatua hiyo ni sehemu ya jitihada zinazoendelea za kuboresha mfumo wa usajili wa kampuni nchini, huku msisitizo ukiwekwa katika kuhakikisha taarifa za miliki manufaa zinakuwa sahihi, zenye uhalisia na zinazoweza kusaidia kuimarisha uwazi na uwajibikaji katika sekta ya biashara.

Mafunzo hayo yamekuwa na matokeo chanya kwa taasisi na wadau wake, kwani yamechangia kuongeza uelewa, kuboresha usahihi wa taarifa zinazowasilishwa, na kupunguza makosa katika mfumo wa usajili wa kampuni.

Hongera kwa kurasimisha biashara
30/05/2026

Hongera kwa kurasimisha biashara

*BRELA YAPONGEZWA KUSAIDIA WAFANYABIASHARA JIJINI MBEYA*Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi ...
30/05/2026

*BRELA YAPONGEZWA KUSAIDIA WAFANYABIASHARA JIJINI MBEYA*

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhandisi Maryprisca Mahundi, ameipongeza Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) kwa kuendeleza mkakati kusaidia na kuwawezesha wafanyabiashara vijana, hususan jijini Mbeya kupitia huduma za papo kwa papo.

Mhandisi Mahundi ametoa pongezi hizo alipotembelea banda la BRELA katika maonesho ya Mbeya City Expo 2026 yanayoendelea mkoani humo ambapo alipata pia fursa ya kuona jinsi Wakala inavyotoa huduma za usajili wa papo kwa papo, hatua inayookoa muda na gharama kwa wafanyabiashara wadogo na wakati.

“Nawapongeza sana BRELA kwa kusogeza huduma hizi karibu na wananchi wa Mbeya, kutoa huduma za papo kwa papo na kukabidhi vyeti hapa hapa kunawawezesha wafanyabiashara hasa vijana na wanawake kuchangamkia fursa ya kurasimisha biashara zao na kuingia kwenye mfumo rasmi wa kiuchumi,” alisema Naibu Waziri Mhandisi Mahundi.

Aidha, akiwa bandani hapo, Naibu Waziri Mhandisi Maryprisca Mahundi alipata pia fursa ya kipekee ya kukabidhi cheti cha usajili wa Jina la Biashara kwa mteja aliyekamilisha mchakato wa urasimishaji wa biashara yake papo hapo.

Nao baadhi ya washiriki na wajasiriamali waliotembelea banda la BRELA walieleza kufurahishwa kwao na huduma ya papo kwa papo inayoendelea kwenye maonyesho hayo, wakisema kuwa imewapunguzia urasimu na kuwapa nafasi ya kulinda nembo na majina ya biashara zao kwa urahisi zaidi.

Maonyesho hayo ya siku kumi yanatarajiwa kuhitimishwa Mei 30, 2026 ambapo BRELA imekuwa ikitoa huduma za Usajili wa Jina la Biashara, Kampuni, Alama za Biashara na Huduma, Leseni za Biashara Kundi A pamoja na elimu ya urasimishaji biashara.

TAARIFA KWA UMMA
28/05/2026

TAARIFA KWA UMMA

Address

BRELA HOUSE, Plot No. 23, , Block No. 20, , Shaaban Rober Street/Sokoine Drive
Dar Es Salaam
P.O.BOX9393

Opening Hours

Monday 08:30 - 15:30
Tuesday 08:30 - 15:30
Wednesday 08:30 - 15:30
Thursday 08:30 - 15:30
Friday 08:30 - 15:30

Telephone

+255222212800

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when BRELA Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to BRELA Tanzania:

Share