BRELA Tanzania

BRELA Tanzania The Business Registrations and Licensing Agency deals with Business Names,Trade Marks,Industrial License, and Patents.

BRELA is a Government Executive Agency established under the Government Executive Agencies Act No. 30 of 1997. It was established on the 28th of October, 1999 by Government Notice No. 294 A published on the 8th October, 1999 and it was officially inaugurated on the 3rd December, 1999. AIM, ROLE AND STRATEGIC OBJECTIVES

AIM
-The aim of the Agency is to ensure that businesses operate in accordance with the laid down regulations and sound commercial principles. ROLES
-The specific roles include the following:
-To administer companies and business names laws.
-To regulate business by administering business and industrial licensing laws.
-To administer intellectual property laws.
-To encourage and facilitate local and foreign business investment.
-To stimulate scientific and technological inventiveness and innovation and encourage technology transfer.
-To protect the development of creativity in artistic, literary works, and expression of folklore by protecting such work in conjunction with rights owners. STRATEGIC OBJECTIVES
The Strategic Objectives of the agency are :
-Ensuring that businesses comply with the laid down regulations to the satisfaction of the Government and the business community.
-Improving service delivery by the adoption of modern business practices.
-Building an efficient and effective workforce by adopting modern Human Resource Management policies.
-Achieving financial self-sufficiency and generate surplus of income that supports the implementation of other strategic objectives.

Je, una ubunifu ambao haujaulinda? Wahi sasa na ulinde leo kwa manufaa yako na Taifa kwa ujumla
18/09/2026

Je, una ubunifu ambao haujaulinda? Wahi sasa na ulinde leo kwa manufaa yako na Taifa kwa ujumla

Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Mhe. Modest Mkude, amewapongeza wajasiriamali hususan wanawake wa Arusha kwa ubunifu na juhudi...
18/09/2026

Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Mhe. Modest Mkude, amewapongeza wajasiriamali hususan wanawake wa Arusha kwa ubunifu na juhudi wanazofanya katika kuanzisha na kuendeleza shughuli za kiuchumi, huku akiwataka kutumia fursa zilizopo kurasimisha na kukuza biashara zao ili kuongeza mchango wao katika uchumi wa taifa.

Mhe. Mkude alitoa pongezi hizo leo tarehe 17 Septemba 2026 katika Viwanja vya Ngarenaro, Jijini Arusha, alipokiwa akizungumza na wajasiriamali na wadau walioshiriki katika Kliniki ya Biashara na Viwanda iliyoandaliwa na Wizara ya Viwanda na Biashara kwa kushirikisha taasisi mbalimbali za Serikali zinazotoa huduma kwa wafanyabiashara na wajasiriamali ikiwemo BRELA.

“Wajasiriamali wanapaswa kutumia fursa zinazopatikana, kuendelea kuwa wabunifu na kuhakikisha biashara zao zinarasimishwa ili waweze kunufaika na fursa mbalimbali zinazotolewa na Serikali,” alisema Mhe. Mkude.

Alisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya Serikali, taasisi zake na sekta binafsi katika kujenga mazingira wezeshi kwa wafanyabiashara na wajasiriamali, akieleza kuwa upatikanaji wa elimu na huduma kwa wakati ni sehemu muhimu ya kuwawezesha wafanyabiashara kuendesha shughuli zao kwa ufanisi.

Kwa upande wake, Afisa Leseni kutoka Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), Bw. Rajab Chambega, alibainisha kuwa BRELA imeshiriki katika kliniki hiyo kwa lengo la kusogeza huduma na elimu ya urasimishaji wa biashara karibu zaidi na wafanyabiashara na wajasiriamali.

Aidha, alieleza kuwa kupitia kliniki hiyo, wafanyabiashara wamepata fursa ya kupata maelezo kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa na BRELA, ikiwemo usajili wa majina ya biashara, usajili wa kampuni, utoaji wa Leseni za Biashara Kundi A, leseni za viwanda pamoja na usajili wa alama za biashara na huduma.

“Lengo letu ni kuhakikisha mfanyabiashara anapata elimu sahihi kuhusu hatua anazopaswa kuchukua ili kurasimisha biashara yake, kuilinda na kuitengenezea mazingira ya kukua,” alisema Chambega.

Vile vile alisema kuwa urasimishaji wa biashara ni hatua muhimu katika kujenga biashara yenye msingi imara, kwa kuwa humwezesha mfanyabiashara kutambulika kisheria na kutumia fursa mbalimbali zinazohitaji biashara kuwa imesajiliwa na kuwa na

BRELA: VIJANA RASIMISHENI VIKUNDI KUNUFAIKA NA FURSA ZA KIUCHUMIWakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) umewahim...
17/09/2026

BRELA: VIJANA RASIMISHENI VIKUNDI KUNUFAIKA NA FURSA ZA KIUCHUMI

Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) umewahimiza wanafunzi na wahitimu wa Vyuo Vikuu Nchini kuanzisha, kujiunga na kurasimisha vikundi vyao vya ujasiriamali ili kuongeza uwezo wa kunufaika na fursa mbalimbali za kiuchumi, ikiwemo mikopo, zabuni na huduma nyingine zinazolenga kuwawezesha vijana.

Wito huo umetolewa leo, Septemba 17, 2026, jijini Dar es Salaam na Afisa Mtendaji Mkuu wa BRELA, Bw. Godfrey Nyaisa, alipokuwa akitoa wasilisho maalum katika Kongamano la CEO Mindset 2026 lililoandaliwa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) na kufanyika katika Ukumbi wa Confucius Institute wa Chuo hapo.

Kongamano hilo lililenga kuwaandaa wanafunzi na wahitimu wapya kuwa viongozi na wasimamizi wenye uwezo wa kuanzisha na kuendesha taasisi, kampuni na biashara zao kwa ufanisi iliwakutanisha wanafunzi 33 kutoka Ndaki ya Biashara (UDBS), Ndaki ya Elimu (UDSoE), pamoja na Ndaki ya Kilimo na Sayansi ya Chakula (CoAF).

Akizungumza katika kongamano hilo, Bw. Nyaisa alisema urasimishaji wa vikundi ni hatua muhimu kwa vijana wanaotaka kujenga biashara endelevu na kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi badala ya vijana kufanya shughuli zao mmoja mmoja, kuunda na kurasimisha vikundi kunaweza kuwawezesha kuwa na nguvu ya pamoja katika kutafuta mitaji, fursa za biashara pamoja na zabuni mbalimbali zinazotolewa na Serikali.

“Vijana mnapaswa kuanza kufikiria zaidi ya mtu mmoja mmoja. Mkiwa katika vikundi vilivyorasimishwa mnaweza kujenga nguvu ya pamoja na kuwa katika nafasi nzuri zaidi ya kutafuta fursa za kiuchumi, usajili na urasimishaji wa biashara ni hatua muhimu katika safari ya kijana kutoka kuwa na wazo la biashara hadi kuwa mjasiriamali mwenye shughuli inayotambulika” alisema Bw. Nyaisa

Bw. Nyaisa alisema elimu ya urasimishaji inapaswa kuanza mapema, hususan katika vyuo vikuu, ili wanafunzi waelewe taratibu za kuanzisha na kusimamia biashara kabla ya kuhitimu huku akiwasisitiza walimu na wahadhiri wa masomo ya biashara Chuoni hapo, kutenga muda katika ratiba zao kwa ajili ya kuwaunganisha wanafunzi na wataalamu wa BRELA kwa lengo la kuwawezesha wanafunzi kupata elimu kuhusu usajili wa ka

17/09/2026

Kuelekea CCEOs Forum 2026.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), atashiriki katika Mkutano wa Wenyeviti na Wakuu wa Taasisi za Umma (C-CEOs Forum 2026), unaotarajiwa kuanza Septemba 28 hadi 30, 2026, katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Arusha (AICC).



-CEOsForum2026

Sogea karibu na Radio yako tutakuwa mubashara kupitia TBC FM Radio
17/09/2026

Sogea karibu na Radio yako tutakuwa mubashara kupitia TBC FM Radio

WIZARA NA BRELA ZAFANYA TATHMINI YA KATAZO LA BIASHARA 15 KWA WAGENIKatibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Mhe. B...
16/09/2026

WIZARA NA BRELA ZAFANYA TATHMINI YA KATAZO LA BIASHARA 15 KWA WAGENI

Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Mhe. Balozi Waziri Rajab Salum, leo tarehe 16 Septemba 2026 amefanya kikao kazi na taasisi wezeshi kwa biashara ikiwemo BRELA, TISEZA, TANTRADE, FCC, TPA, TASAC, Idara ya Uhamiaji, Idara ya Kazi na Ajira kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Wizara ya Uchukuzi pamoja na Halmashauri za Dar es Salaam na Mwanza kwa lengo la kujadili na kufanya maboresho katika utekelezaji wa katazo la biashara 15 ambazo haziruhusiwi kwa wageni nchini.

Akizungumza katika kikao hicho, Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara Mhe. Balozi Waziri alisema hatua hiyo imekuja kufuatia maoni na malalamiko kutoka kwa wadau mbalimbali, hivyo Wizara imeona umuhimu wa kuyafanyia tathmini ili kubaini maeneo yanayohitaji maboresho na kuhakikisha utekelezaji unazingatia malengo yaliyokusudiwa.

Mhe. Balozi Waziri alisema mapendekezo ya kikao na tathmini itawasilishwa kwa Waziri wa Viwanda na Biashara kwa hatua zaidi za na kutoa mwelekeo wa utekelezaji wake huku akisisitiza kuwa Serikali, kupitia Wizara inalenga kulinda na kuimarisha sekta ya biashara nchini kwa kuweka misingi imara ya kiuchumi na kujenga mazingira wezeshi yatakayowawezesha Watanzania kunufaika na fursa za biashara

Aidha, Balozi Waziri alisisitiza umuhimu wa kuzingatia utu katika utekelezaji wa katazo hilo, akibainisha kuwa pamoja na wajibu wa Serikali kusimamia na kutekeleza sheria, utekelezaji wake unapaswa kufanyika kwa kuzingatia utu na kuepusha usumbufu usio wa lazima kwa wahusika.

Baada ya kukamilika kwa tathmini na majadiliano, kikao hicho kilifikia hatua ya kupitisha mapendekezo yaliyofanyiwa maboresho, ambayo sasa yanawasilishwa kwa Waziri wa Viwanda na Biashara kwa ajili ya kutoa mwelekeo wa mwisho kuhusu hatua zinazofuata katika utekelezaji wa katazo hilo.

Hatua hiyo inalenga kuhakikisha kuwa utekelezaji wa katazo la biashara 15 unakwenda sambamba na sera, sheria na taratibu za Serikali, huku ukizingatia maslahi ya Taifa na mazingira wezeshi kwa Watanzania kushiriki kikamilifu katika shughuli za biashara.

Sogea karibu na redio yako kupitia Safina radio FM
16/09/2026

Sogea karibu na redio yako kupitia Safina radio FM

Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) umewataka wananchi wa Mikoa ya Arusha, Kilimanjaro na Manyara kujitokeza...
16/09/2026

Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) umewataka wananchi wa Mikoa ya Arusha, Kilimanjaro na Manyara kujitokeza kwa wingi katika Viwanja vya Ngarenaro, Jijini Arusha, ili kupata elimu na huduma mbalimbali zinazotolewa na Wakala huo.

Wito huo umetolewa leo tarehe 15 Septemba 2026 wakati wa Maonesho ya Viwanda Business Clinic yaliyoandaliwa na Wizara ya Viwanda na Biashara ambayo yanayoendelea katika viwanja hivyo.

Awali, akizungumza katika banda la BRELA, Afisa Leseni wa Wakala huo, Bw. Rajabu Chambega, amesema BRELA imeshiriki katika maonesho hayo mahsusi kwa lengo la kusogeza huduma karibu na wananchi.

“Tumefika hapa Arusha kushiriki katika kliniki hii iliyoandaliwa na Wizara ya Viwanda na Biashara kwa lengo la kuwafikia wakazi wa Arusha na maeneo jirani ili waweze kupata huduma zetu kwa urahisi zikiwemo usajili wa majina ya biashara, usajili wa makampuni na utoaji wa leseni,” alisema Bw. Chambega.

Aidha, Bw. Chambega aliwasisitiza wamiliki wa makampuni hususan yanayojihusisha na masuala ya utalii, hoteli na viwanda kuhakikisha wanafuata sheria kwa kusajili na kuhuisha biashara zao kwa wakati.

Katika hatua nyingine, Bw. Chambega, aliwataka wananchi kuchangamkia fursa hiyo kupata elimu kuhusu masuala ya Miliki Ubunifu, Alama za Biashara pamoja na Hataza ili kupata fursa mbalimbali za kibiashara na mikopo.

Maonesho ya Viwanda Business Clinic yanahusisha Taasisi mbalimbali zilizo chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara zikitoa huduma kwa wananchi wa Kanda ya Kaskazini kwa pamoja.

Radio Five 🎧📻
16/09/2026

Radio Five 🎧📻

Arusha tumekufikia sasa, karibu katika Kliniki ya Viwanda na Biashara tukuhudumie
15/09/2026

Arusha tumekufikia sasa, karibu katika Kliniki ya Viwanda na Biashara tukuhudumie

Address

BRELA HOUSE, Plot No. 23, , Block No. 20, , Shaaban Rober Street/Sokoine Drive
Dar Es Salaam
P.O.BOX9393

Opening Hours

Monday 08:30 - 15:30
Tuesday 08:30 - 15:30
Wednesday 08:30 - 15:30
Thursday 08:30 - 15:30
Friday 08:30 - 15:30

Telephone

+255222212800

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when BRELA Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to BRELA Tanzania:

Shortcuts

Share