Tanzania Railways Corporation

Tanzania Railways Corporation Tanzania Railways Corporation(TRC) is a state corporation created with the core mandate of providing Ukurasa rasmi wa Facebook wa Shirika la Reli Tanzania.

Shirika linalotoa huduma ya Usafiri wa abiria na mizigo na kusimamia miundombinu ya Reli Tanzania.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC), Mha. Machibya Shiwa, amekuwa sehemu ya jopo  kwenye Mkutano wa 10 wa ...
15/09/2026

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC), Mha. Machibya Shiwa, amekuwa sehemu ya jopo kwenye Mkutano wa 10 wa Uhandisi Afrika unaoendelea katika Ukumbi wa JNICC, jijini Dar es Salaam, leo Septemba 15, 2026.

Mjadala kwenye jopo hilo umejikita katika maeneo mbalimbali ikiwemo umuhimu wa Ufadhili wa Miundombinu; Upatikanaji wa Nishati kupitia Mpango wa Mission 300, Uendelezaji wa Viwanda, Mabadiliko ya Kidijitali na Ushirikiano wa Kikanda.

Awali Mkurugenzi Mkuu, alipokea tuzo kutoka kwa Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla, kwa kutambua mchango wa TRC katika kufanikisha Wiki ya Uhandisi na Mkutano wa 10 wa Uhandisi barani Afrika.

15/09/2026

AFRIKA KUUNGANISHWA NA RELI 2063

14/09/2026

TRC inashiriki Wiki ya 12 ya Uhandisi Afrika na Mkutano wa 10 wa Uhandisi Afrika unaofanyika JNICC, Dar es Salaam, tarehe 14–17 Septemba 2026.

14/09/2026

Wahandisi Wanawake TRC wang'arisha Wiki ya 12 ya Uhandisi na Mkutano wa 10 wa Uhandisi Afrika

Wanawake wahandisi kutoka Shirika la Reli Tanzania (TRC) wameshiriki kwa wingi katika Jukwaa la 9 la Wanawake Wahandisi ...
14/09/2026

Wanawake wahandisi kutoka Shirika la Reli Tanzania (TRC) wameshiriki kwa wingi katika Jukwaa la 9 la Wanawake Wahandisi Afrika (9th African Women Engineering Forum) linalofanyika leo, Septemba 14, 2026, katika ukumbi wa JNICC, Dar es Salaam.

Jukwaa hili ni sehemu ya Wiki ya 12 ya Uhandisi Afrika (12th Africa Engineering Week) na Mkutano wa 10 wa Uhandisi Afrika (10th Africa Engineering Conference) unaofanyika tarehe 14–17 Septemba 2026, wenye kaulimbiu “Kujenga Afrika yenye mustakabali jumuishi, bunifu na endelevu” (Engineering Africa’s Inclusive, Innovative and Sustainable Future).

Ushiriki wa wanawake katika uhandisi ni muhimu katika kuleta mitazamo bunifu, usawa wa fursa na suluhisho endelevu zinazokidhi mahitaji ya jamii. Kupitia utaalamu na ubunifu wao, wanawake wanaendelea kuwa sehemu muhimu ya kujenga miundombinu imara na kuchochea maendeleo ya Afrika.

Jumatatu njema...!!
14/09/2026

Jumatatu njema...!!

Sehemu ya wahitimu wa elimu ya msingi Septemba 10, 2026 nchini,  katika Shule ya msingi Itigi reli, wakiwa katika picha ...
12/09/2026

Sehemu ya wahitimu wa elimu ya msingi Septemba 10, 2026 nchini, katika Shule ya msingi Itigi reli, wakiwa katika picha ya pamoja katika mahafali ya 32 ya shule ya msingi Itigi reli Septemba 12, 2026.

Shule ya msingi Itigi Reli ilianzishwa mwaka 1987 ikiwa na lengo la kutoa elimu kwa watoto wa wafanyakazi wa TRC wanaohudumu katika maeneo yasiyo na shule za msingi au ziko mbali na maeneo yao ya kazi (magengeni). Shule hii ilizinduliwa rasmi Aprili 04, 1993 na Rais Mstaafu wa awamu ya pili Hayati Alhaji Ali Hassan Mwinyi na hadi sasa inamilikiwa na TRC.

12/09/2026

Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) Bi. Irene Ungani Robert, kwa niaba ya Mkurugenzi mkuu wa TRC Mhandisi Machibya Shiwa, akizungumza na wahitimu wa elimu ya msingi ( hawapo pichani), katika mahafali ya 32 ya shule ya msingi Itigi reli, Septemba 12, 2026.

12/09/2026

Ni vipaji kutoka kwa wanafunzi wa darasa la kwanza na la pili wa Shule ya msingi Itigi reli wakati wa mahafali ya 32 ya shule ya msingi Itigi Reli Septemba 12, 2026

12/09/2026

Wazazi na wanafunzi waliohitimu elimu ya msingi Septemba 10, 2026 sambamba na wageni waalikwa, wakicheza na kufurahia pamoja wakati wa mahafali ya 32 ya Shule ya msingi Itigi reli Septemba 11, 2026.

Address

Railway Street
Dar Es Salaam
P.OBOX76959

Opening Hours

Monday 08:00 - 16:30
Tuesday 08:00 - 16:30
Wednesday 08:00 - 16:30
Thursday 08:00 - 16:30
Friday 08:00 - 16:30
Saturday 08:00 - 12:30

Telephone

+255800110042

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Tanzania Railways Corporation posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Tanzania Railways Corporation:

Shortcuts

Share