04/10/2024
;
; Usiogope(2)
------------------------------------
5. Kwa sababu Muumba wako ni mume wako;
BWANA wa majeshi ndilo jina lake; na mtakatifu wa Israel ndiye mkombozi wako;
Yeye ataitwa Mungu wa dunia yote.
6. Maana BWANA amekuita k**a mke aliyeachwa na kuhuzunishwa rohoni,
k**a mke wakati wa ujana, atupwapo, asema Mungu wako.
7. Kwa kitambo kidogo nimekuacha;
lakini kwa rehema nyingi nitakukusanya.
8. Kwa ghadhabu ifurikayo nalikuficha uso wangu ktk dakika moja;
lakini kwa fadhili za milele nitakurehemu, asema BWANA, Mkombozi wako.
{ 54-5}
.
----------------------
Haleluja watu wa Mungu.
Neno la Mungu kupitia kinywa cha nabii Isaya linasema kuwa "kwa sababu Muumba wako ni mume wako; BWANA wa majeshi ndilo jna lake;"
Kwa hiyo kusema kwamba Mungu pia ni mume wa wajane na ni mtetezi wao.
41;14
Usiogope, Yakobo uliyemdudu, nanyi watu wa Israel; mimi nitakusaidia,
asema BWANA, na mkombozi wako ni mtakatifu wa Israel.
Kwa hiyo Mungu huyu anayesema na nabii Isaya, ni Mungu wa wote wenye mwili asiye na ubaguzi
wala hangalii wewe umeolewa au mjane.
Neno la Mungu linaendelea kwa kusema "Yeye ni Mungu wa dunia yote"
Wakati wanadamu wanapofikiri wamekuacha, na kukutenga mbali nawe.
Na kufananishwa na mke aliyeachwa na mumewe na kuhuzunishwa rohoni, na kuwa mwenye dhiki na kukata tamaa.
2Kori 4;17
Maana dhiki yetu nyepesi, iliyo ya muda wa kitambo tu, yatufanyia utukufu wa milele uzidio kuwa mwingi sana.
Haleluya watu wa Mungu, kwa hiyo wakati unapihisi umeachwa na kuwa na dhiki, shida na taabu.
Mungu anayaachilia ili pale utakapoona umeaibika vya kutosha mbele za wanadamu, ndipo Mungu anakuinuwa na kukuweka mahala pa juu na kukuondolea aibu yako yote.
Na ndiyo maana kichwa cha somo tukapewa "USIOGOPE"
Maana pale utakspoogopa ndipo adui yako anachukuwa nafasi ktk maisha yako.
Kwa sbabu hiyo basi, haijarishi itakutesa kuasi gani, lakini neno moja ulishike ni hili .
31;3
BWANA alinitokea alinitokea zamani, akisema, Naam nimekupenda kwa upendo wa milele,
ndiyo maana nimekuvuta kwa fadhili zangu.
Hakika Bwana Mungu umetuita na kutupenda kwa fadhili za milele, hivyo tusiogope, wewe u pamoja nsi daima.
Mbarikiwe nyote