Taasisiyaelimutanzania

Taasisiyaelimutanzania Taasisi ya Serikali yenye mamlaka kisheria ya kuandika na kuandaa vitabu vya kiada, mihtasari na mitaala.

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) Dkt. Aneth Komba amesema kuwa, Shindano la Taifa la Stadi za Ufundish...
08/06/2026

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) Dkt. Aneth Komba amesema kuwa, Shindano la Taifa la Stadi za Ufundishaji kwa walimu wa Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari Tanzania Bara linaunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan za kuhakikisha wanafunzi wanamudu Stadi za kusoma, kuandika na kuhesabu (K*K) wanapofika darasa la tatu.

Aliyasema hayo Juni 6, 2026 katika hafla ya tuzo ya Taifa ya stadi za ufundishaji kwa walimu wa Awali, Msingi na Sekondari lililofanyika katika ukumbi wa maktaba mpya UDSM.

“Lengo la shindano hili ni kusaidia kutatua changamoto za ufundishaji na ujifunzaji wa stadi za Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (K*K) ili kuhakikisha wanafunzi wanazimudu stadi hizo muhimu wanapofikia Darasa la Tatu." Alisema

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) Dkt. Aneth Komba amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe kutoka Uba...
08/06/2026

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) Dkt. Aneth Komba amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe kutoka Ubalozi wa Jamhuri ya Korea nchini  Tanzania kujadili namna ya kushirikiana katika kuboresha Elimu nchini.

Dkt. Komba amekutana na ugeni huo ulioongozwa na Naibu Mkuu wa misheni wa Ubalozi huo nchini Bi. Daeun Kim leo Juni 8, 2026 katika ofisi za TET makao makuu Jijini Dar es Salaam ambapo pamoja na kujadili uboreshaji wa elimu nchini ujumbe huo kutoka Korea umeahidi kuchangia vitabu vya hadithi vitavyosaidia ujifunzaji na ufundishaji kwa wanafunzi.

07/06/2026

Mgeni rasmi wa hafla ya shindano la Taifa la Stadi za Ufundishaji kwa walimu wa Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari Tanzania Bara Prof. Riziki Shemdoe akiongea na walimu walioshiriki katika hafla ya hiyo iliyofanyika Juni 6,2026 katika ukumbi wa maktaba mpya UDSM

Hafla hiyo ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa kimataifa, kitaifa, mkoa na wilaya

Mgeni rasmi wa hafla ya shindano la Taifa la Stadi za Ufundishaji kwa walimu wa Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari Tanz...
07/06/2026

Mgeni rasmi wa hafla ya shindano la Taifa la Stadi za Ufundishaji kwa walimu wa Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari Tanzania Bara Prof. Riziki Shemdoe akitoa zawadi kwa washindi wa kwanza katika kila kipengele cha shindano hilo lililofanyika Juni 6,2026 katika ukumbi wa maktaba mpya UDSM.

Hafla hiyo ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa kimataifa, kitaifa, mkoa na wilaya

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo, Husna Sekiboko, amesema mafanikio katika sekta y...
06/06/2026

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo, Husna Sekiboko, amesema mafanikio katika sekta ya elimu yanahitaji ushiriki wa wadau wote, wakiwemo wazazi, walimu, wanafunzi na viongozi wa jamii.

Amesema maboresho yanayoendelea katika mifumo ya uongozi na utawala yanalenga kuongeza ufanisi wa utoaji wa huduma za elimu na kuimarisha matokeo ya kujifunza kwa wanafunzi.

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Elimu Tanzania (TET), Dkt. Aneth Komba, amesema shindano la Taifa la Stadi za Ufundishaji ...
06/06/2026

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Elimu Tanzania (TET), Dkt. Aneth Komba, amesema shindano la Taifa la Stadi za Ufundishaji la mwaka 2026 ni la nne kwa walimu wa elimu ya awali na msingi na la pili kwa walimu wa elimu ya sekondari, likihusisha halmashauri zote 184 za Tanzania Bara.

Ameyasema hayo leo Juni 6, 2026 katika hafla ya tuzo ya Taifa ya stadi za ufundishaji kwa walimu wa Awali, Msingi na Sekondari lililofanyika katika ukumbi wa maktaba mpya UDSM.

Amesema kwa upande wa elimu ya awali, shindano hilo limejikita katika kuimarisha umahiri wa ufundishaji wa stadi za kusoma, hususan sauti za herufi ambazo zimekuwa changamoto kwa baadhi ya wanafunzi katika kuzitamka na kuzitumia kwa usahihi katika kuunda silabi na maneno.

“Lengo la shindano hili ni kusaidia kutatua changamoto za ufundishaji na ujifunzaji wa stadi za Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (K*K) ili kuhakikisha wanafunzi wanazimudu stadi hizo muhimu wanapofikia Darasa la Tatu." Amesema

Ameeleza kuwa maandalizi ya shindano hilo yalihusisha uchambuzi wa matokeo ya wanafunzi kupitia taarifa za Baraza la Mitihani la Tanzania pamoja na maeneo mapya yaliyoingizwa katika mtaala ili kubaini maeneo yanayohitaji kupewa kipaumbele.

Kwa mujibu wa Dkt. Komba, walimu walitakiwa kuandaa andalio la somo, kujirekodi wakifundisha kwa muda wa dakika 10 hadi 15 na kupakia video pamoja na andalio hilo katika mfumo wa kidijitali wa National Teaching Skills Competition System kwa ajili ya tathmini.

Jumla ya walimu 3,153 walijisajili katika mfumo huo, huku walimu 1,263 sawa na asilimia 40 wakifanikiwa kupakia video zao kwa ajili ya tathmini katika ngazi ya halmashauri.

Amesema tathmini ilifanyika katika ngazi tatu ambazo ni halmashauri, mkoa na taifa kwa kuzingatia vigezo mbalimbali ikiwemo ubora wa maudhui, mtiririko wa somo, matumizi ya mbinu shirikishi, matumizi ya TEHAMA, matumizi ya zana za kufundishia, ukuzaji wa stadi za karne ya 21 na matumizi ya upimaji endelevu katika mchakato wa ufundishaji na ujifunzaji.

Katika mchujo wa shindano hilo, video 751 zilifanikiwa kuingia ngazi ya mkoa kutoka video 1,263 zilizotathminiwa katika ngazi ya halmashauri. Kati ya hizo, video 232 zilichaguliwa kuingia ngazi ya taifa.

PROF. SHEMDOE AWATAKA WALIMU KUONGEZA UBUNIFU KATIKA UFUNDISHAJI-Walimu 35 walioshinda tuzo za ufundishaji kupatiwa viwa...
06/06/2026

PROF. SHEMDOE AWATAKA WALIMU KUONGEZA UBUNIFU KATIKA UFUNDISHAJI

-Walimu 35 walioshinda tuzo za ufundishaji kupatiwa viwanja

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Prof. Riziki Shemdoe ametoa wito kwa walimu nchini kuendelea kufanya kazi kwa bidii, kujituma na kutumia mbinu bunifu za ufundishaji ili kuimarisha ubora wa elimu na kuchangia maendeleo ya taifa, huku akielekeza halmashauri kuwapa viwanja karibu kwenye maeneo yao ya kazi walimu 35 walioibuka washindi katika Shindano la Taifa la Stadi za Ufundishaji k**a sehemu ya motisha.

Prof. Shemdoe ametoa wito huo leo Juni 6, 2026 jijini Dar es Salaam katika hafla ya utoaji wa zawadi kwa washindi wa shindano hilo kwa walimu wa elimu ya awali, msingi na sekondari Tanzania Bara, huku akisisitiza kuwa, walimu wana mchango mkubwa katika kuwalea na kuwaandaa wanafunzi kuwa wananchi wenye maarifa, stadi na maadili mema yanayohitajika katika jamii.

Prof. Shemdoe amesema Serikali itaendelea kuthamini mchango wa walimu kwa kuweka mazingira bora ya kazi na motisha mbalimbali zinazolenga kuongeza ufanisi katika ufundishaji na ujifunzaji.

Aidha, amewataka walimu kuendelea kutumia mbinu za kisasa na bunifu katika ufundishaji ili kuwajengea wanafunzi uwezo wa kufikiri kwa kina, kubuni na kukabiliana na changamoto za dunia ya sasa.

Amesema tuzo hizo zinalenga kuhamasisha ubora, uwajibikaji, ubunifu na kujituma katika kazi za kufundisha, na kusisitiza kuwa, maendeleo ya taifa yanategemea kwa kiasi kikubwa ubora wa rasilimali watu inayozalishwa kupitia mfumo wa elimu.

Mgeni Rasmi wa shindano la Taifa la Stadi za Ufundishaji kwa walimu wa Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari Tanzania Bara...
06/06/2026

Mgeni Rasmi wa shindano la Taifa la Stadi za Ufundishaji kwa walimu wa Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari Tanzania Bara Prof. Riziki Shemdoe akiwasili katika ukumbi wa maktaba mpya UDSM, tayari kwaajili ya kushiriki hafla hiyo inayoendelea leo Juni 6, 2026.

Pia, Prof. Shemdoe ameambatana na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Daniel Mushi, Mkurugenzi Mkuu wa TET Dkt. Aneth Komba na viongozi mbalimbali wa kitaifa na mkoa.

Hafla ya shindano la Taifa la Stadi za Ufundishaji kwa walimu wa Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari Tanzania Bara juni ...
05/06/2026

Hafla ya shindano la Taifa la Stadi za Ufundishaji kwa walimu wa Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari Tanzania Bara juni 6, 2026 katika ukumbi wa maktaba mpya UDSM. Mgeni rasmi ni Waziri wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI Prof. Riziki Shemdoe.

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) Dkt. Aneth Komba amekutana na walimu teule 35 wanaotarajia kuwania tu...
05/06/2026

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) Dkt. Aneth Komba amekutana na walimu teule 35 wanaotarajia kuwania tuzo katika shindano la Taifa la Stadi za Ufundishaji inayotarajia kufanyika Juni 6, 2026 katika ukumbi wa maktaba mpya UDSM.

Hayo yamejiri leo Juni 5,2026 katika makao makuu ya ofisi za TET Jijini Dar es Salaam ambapo ameambatana na baadhi ya wajumbe wa menejimenti walioongozwa na Naibu Mkurugenzi Mkuu Dkt. Angela Katabaro pamoja na mkuu wa idara ya rasilimali watu Bw. Moses Ziota.

Dkt. Komba amesema, mpaka sasa Serikali imefanya maboresho sita katika mitaala ili kuendana na mabadiliko ya teknolojia na mahitaji wa sasa hasa katika soko la ajira na stadi za karne ya 21.

Aidha, Dkt. Komba amesema, dhamira ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuona mtoto wa Tanzania anaweza kujiajiri mwenyewe, kuajiriwa au kuajiri wengine pindi atapomaliza shule, kufutia maboresho ya Mtaala yaliyoanza kutekelezwa Januari 2024.

"Kufuatia maboresho ya Mtaala yaliyofanyika Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, anatamani kuwe na wanafunzi wanaoweza kujiajiri au kuajiriwa pindi watapomaliza elimu yao." Amesema Dkt. Komba.

Sambamba na hilo Dkt. Komba amewaomba walimu kuendelea kuwa chachu ya mabadiliko katika elimu nchini kwani tayari Serikali imeshatoa mafunzo ya Mtaala ulioboreshwa na mifumo ya TEHAMA kwa walimu wote nchini.

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Taasisiyaelimutanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share