Land Transport Regulatory Authority - LATRA

Land Transport Regulatory Authority - LATRA Official account for Land Transport Regulatory Authority (LATRA).

15/09/2026
Viongozi wa LATRA wakiongozwa na Prof. Ahmed M. Ame, Mwenyekiti wa Bodi LATRA, Septemba 11, 2026, wamefika Kizimkazi Zan...
12/09/2026

Viongozi wa LATRA wakiongozwa na Prof. Ahmed M. Ame, Mwenyekiti wa Bodi LATRA, Septemba 11, 2026, wamefika Kizimkazi Zanzibar kumfariji Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kufuatia kifo cha Mhe. Hafidh Ameir Hassan, aliyekuwa mume wake.

Pamoja na kumfariji wametumia muda huo kufanya dua ya pamoja na Mhe. Rais kumuombea marehemu.

Viongozi wa LATRA waliomtembelea Mhe. Rais ni pamoja na Mwenyekiti wa Bodi LATRA, CPA Dkt. Habibu J. Suluo Mkurugenzi Mkuu LATRA, Bw. Athumani M. Kwikima Mkurugenzi wa Huduma za Mamlaka na Bw. Salum S. Pazzy Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano LATRA.

Bw. Augustus Fungo, Afisa Huduma kwa Wateja Mkuu – LATRA, amekabidhi vyeti kwa wanafunzi kutoka Convention Social and Ec...
11/09/2026

Bw. Augustus Fungo, Afisa Huduma kwa Wateja Mkuu – LATRA, amekabidhi vyeti kwa wanafunzi kutoka Convention Social and Economic Empowerment (CSEE) walioshiriki ziara ya mafunzo kuhusu kazi na majukumu ya LATRA kupitia programu ya Mzalendo Tour Youth Connect.

Ziara hiyo imelenga kuwaongezea wanafunzi uelewa kuhusu sekta ya usafiri ardhini, matumizi ya mifumo ya teknolojia pamoja na fursa mbalimbali zilizopo katika sekta ya usafiri ardhini nchini.

Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA), tarehe 10 Septemba 2026, imekutana na Walimu na wanafunzi kutoka Taasisi is...
11/09/2026

Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA), tarehe 10 Septemba 2026, imekutana na Walimu na wanafunzi kutoka Taasisi isiyo ya serikali ya Convention Social and Economic Empowerment (CSEE), waliotembelea LATRA kwa lengo la kujifunza kuhusu kazi na majukumu yanayofanywa na LATRA kudhibiti sekta ya usafiri ardhini nchini.

Akifungua ziara hiyo, Bw. Augustus Fungo, Afisa Huduma kwa Wateja Mkuu LATRA, amewaasa wanafunzi kujifunza, kuzielewa sheria za usafirishaji na kuchangamkia fursa zinazopatikana kwenye sekta ya usafiri, huku wakiendeleza ubunifu na matumizi ya teknolojia katika kutafuta suluhisho za changamoto za usafiri, ikiwemo matumizi ya nishati safi.

Wanafunzi hao wameipongeza na kuishukuru LATRA kwa kuwapatia fursa ya kujifunza na kupata uelewa mpana kuhusu sekta ya usafiri ardhini, matumizi ya teknolojia na fursa mbalimbali zilizopo katika sekta hiyo.

Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA), tarehe 9 Septemba 2026, imekutana na Chama cha Madereva wa Taksi Mtandao Ta...
10/09/2026

Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA), tarehe 9 Septemba 2026, imekutana na Chama cha Madereva wa Taksi Mtandao Tanzania (TODA), Wamiliki wa Mifumo ya Taksi Mtandao pamoja na wadau wengine, wakiwemo kampuni zinazojihusisha na uuzaji wa magari yanayotumia nishati safi. Kikao hicho kimefanyika katika Ofisi za LATRA Mkoa wa Dar es Salaam kwa lengo la kuboresha utoaji wa huduma za Taksi Mtandao nchini na kuhakikisha huduma hiyo inapatikana kwa ufanisi wakati wa mashindano ya AFCON 2027 katika miji ya Dar es Salaam, Arusha na maeneo ya jirani.

Akifungua kikao hicho, Bw. Salum Pazzy, Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano - LATRA, amewataka wadau hao kuwa mfano wa kuigwa katika utoaji wa huduma ya Taksi Mtadao kwa wateja wao, kwa kuzingatia ubora, usalama na ufanisi wa huduma hiyo, hususan katika kipindi hiki na wakati wa mashindano ya AFCON 2027.

Kwa upande wake, Bw. Patel Ngereza, Kaimu Meneja Udhibiti Magari ya Abiria - LATRA, amewasihi wadau hao kupanua wigo wa utoaji wa huduma za Taksi Mtandao katika mikoa mingine nchini ili kuwawezesha wananchi wengi zaidi kunufaika na huduma hiyo.

Aidha, Bw. Ngereza amewataka wadau hao kuimarisha mifumo ya usalama ili kuhakikisha abiria wanapotumia huduma za Taksi Mtandao wanakuwa na uhakika na usalama wa safari zao. Vilevile, amewataka wadau kuhakikisha wanakuwa na uelewa wa pamoja kati ya Madereva na Wamiliki wa Mifumo ya Taksi Mtandao kuhusu masuala ya kamisheni pamoja na ofa zinazotolewa na wamiliki wa mifumo hiyo kwa abiria ili kuepusha migogoro inayoibuka baina yao.

Wadau waliohudhuria kikao hicho kwa pamoja wameipongeza LATRA kwa kuandaa kikao hicho, wakieleza kuwa ni hatua muhimu yenye lengo la kujenga ushirikiano na kuboresha zaidi utoaji wa huduma za Taksi Mtandao nchini.

Address

Nkrumah Street, Near Clock Tower
Dar Es Salaam
3093

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Land Transport Regulatory Authority - LATRA posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Land Transport Regulatory Authority - LATRA:

Shortcuts

Share