Embassy of the State of Palestine in Tanzania

Embassy of the State of Palestine in Tanzania The official page of the Embassy of the State of Palestine promoting diplomatic cooperation in Tanzania, Mauritius, and Seychelles.

24/06/2026

Israel inaendelea kutekeleza mauaji ya kimbari na uhalifu mwingine mkubwa kwa kuwalenga kwa makusudi watoto wa Kipalestina

GENEVA – Mamlaka na vikosi vya usalama vya Israel vimekuwa vikiwalenga kwa makusudi watoto wa Kipalestina, jambo lililosababisha kutendeka kwa mauaji ya kimbari (genocide), uhalifu dhidi ya ubinadamu na uhalifu wa kivita katika Ukanda wa Gaza, pamoja na uhalifu wa kivita katika Ukingo wa Magharibi (West Bank). Hayo yameelezwa katika ripoti mpya iliyotolewa leo na Tume Huru ya Kimataifa ya Uchunguzi ya Umoja wa Mataifa kuhusu Ardhi ya Palestina Inayokaliwa kwa Mabavu, ikiwemo Jerusalem Mashariki, na Israel.

Tume hiyo, ambayo mwaka jana ilihitimisha kuwa Israel ilifanya mauaji ya kimbari dhidi ya kundi la Wapalestina katika Ukanda wa Gaza, imebaini kuwa ukubwa na mfumo wa operesheni za kijeshi za Israel umeendelea kwa kiwango kikubwa, na kusababisha idadi isiyokuwa na mfano ya watoto wa Kipalestina kuuawa, kujeruhiwa na kupata majeraha makubwa ya kisaikolojia.

Tume hiyo imesisitiza tena kuwa kuwalenga watoto kwa makusudi ni mojawapo ya vipengele muhimu vinavyothibitisha dhamira ya mauaji ya kimbari ya mamlaka na vikosi vya usalama vya Israel, kwa lengo la kuangamiza, kwa ujumla au kwa sehemu, kundi la Wapalestina huko Gaza.

Fuatilia taarifa hii: https://www.facebook.com/share/p/18tx9weGVj/

Israel inaendelea kutekeleza mauaji ya kimbari na uhalifu mwingine mkubwa kwa kuwalenga kwa makusudi watoto wa Kipalesti...
24/06/2026

Israel inaendelea kutekeleza mauaji ya kimbari na uhalifu mwingine mkubwa kwa kuwalenga kwa makusudi watoto wa Kipalestina

GENEVA – Mamlaka na vikosi vya usalama vya Israel vimekuwa vikiwalenga kwa makusudi watoto wa Kipalestina, jambo lililosababisha kutendeka kwa mauaji ya kimbari (genocide), uhalifu dhidi ya ubinadamu na uhalifu wa kivita katika Ukanda wa Gaza, pamoja na uhalifu wa kivita katika Ukingo wa Magharibi (West Bank). Hayo yameelezwa katika ripoti mpya iliyotolewa leo na Tume Huru ya Kimataifa ya Uchunguzi ya Umoja wa Mataifa kuhusu Ardhi ya Palestina Inayokaliwa kwa Mabavu, ikiwemo Jerusalem Mashariki, na Israel.

Tume hiyo, ambayo mwaka jana ilihitimisha kuwa Israel ilifanya mauaji ya kimbari dhidi ya kundi la Wapalestina katika Ukanda wa Gaza, imebaini kuwa ukubwa na mfumo wa operesheni za kijeshi za Israel umeendelea kwa kiwango kikubwa, na kusababisha idadi isiyokuwa na mfano ya watoto wa Kipalestina kuuawa, kujeruhiwa na kupata majeraha makubwa ya kisaikolojia.

Tume hiyo imesisitiza tena kuwa kuwalenga watoto kwa makusudi ni mojawapo ya vipengele muhimu vinavyothibitisha dhamira ya mauaji ya kimbari ya mamlaka na vikosi vya usalama vya Israel, kwa lengo la kuangamiza, kwa ujumla au kwa sehemu, kundi la Wapalestina huko Gaza.

"Ushahidi unaonyesha kuwa watoto wa Kipalestina wamelengwa na kuuawa kwa makusudi na vikosi vya usalama vya Israel," alisema Mwenyekiti wa Tume hiyo, Srinivasan Muralidhar. "Hata baada ya usitishaji mapigano wa Oktoba 2025, watoto wanaendelea kuuawa na kujeruhiwa vibaya, huku Israel ikiendelea kupuuza makubaliano ya usitishaji mapigano na wajibu wake wa kuwalinda watoto wa Kipalestina chini ya sheria za kimataifa."

Majeraha makubwa ya mwili na akili, mshtuko mkubwa wa kisaikolojia, kuwa yatima, kutenganishwa na familia, ulemavu, kuhama makazi mara kwa mara, njaa, pamoja na kusambaratika kwa mifumo ya elimu na afya, vimeharibu kabisa utoto wa watoto wa Gaza na vitaendelea kuwaathiri katika maisha yao yote.

Watoto wa Kipalestina wamek**atwa na kufungwa, ambapo wamepitia mateso na aina nyingine za ukatili mkubwa katika magereza na vituo vya mahabusu vya Israel, huku familia zao zikikosa taarifa kuhusu walipo. Aidha, vikosi vya usalama vya Israel vimetumia ukatili wa kingono dhidi ya watoto k**a sehemu ya kuwaaibisha na kuwanyanyasa kwa pamoja, katika mfumo wa muda mrefu wa ukaliaji wa mabavu na uhasama wenye misingi ya ukabila, jinsia na vizazi.

Mashambulizi ya Israel dhidi ya vituo vya huduma za watoto wachanga na wajawazito huko Gaza yameathiri moja kwa moja maisha ya watoto wanaozaliwa na mustakabali wa uzazi wa Wapalestina. Hali hiyo imesababisha kuongezeka kwa mimba kuharibika, kasoro za kuzaliwa na matatizo ya muda mrefu kwa watoto wachanga, jambo linaloharibu maisha ya watoto wa Kipalestina na kuathiri mwendelezo wa kizazi cha Wapalestina.

Njaa iliyosababishwa na Israel kupitia mzingiro na kuzuia misaada pia imechangia vifo vya watoto wa Kipalestina na kuathiri vibaya afya ya wengine wengi. Watoto hao wamekosa lishe muhimu, huku wakikabiliwa na ongezeko la magonjwa kutokana na kupungua kwa chanjo, uhaba wa chakula na uharibifu wa huduma za afya.

Wakati huohuo, kubomolewa na kuharibiwa kwa vituo vya kulelea yatima na taasisi za elimu katika Gaza na Ukingo wa Magharibi, ikiwemo Jerusalem Mashariki, kumekwamisha maendeleo ya watoto katika nyanja za kiakili, kijamii na kihisia, pamoja na kudhoofisha misingi ya jamii ya Kipalestina.

"Hata k**a mabomu na risasi vitakoma Gaza na Ukingo wa Magharibi, watoto wa Kipalestina hawatarejea katika hali ya kawaida kwa muda mfupi," alisema Muralidhar. "Uharibifu uliotokea katika afya yao, elimu yao na maendeleo yao hauwezi kurekebishwa."

Watoto wa Kipalestina wamepata madhara makubwa ya kisaikolojia baada ya kupokonywa hisia ya usalama na matumaini ya maisha ya baadaye. Madhara hayo ya kiakili yanaendelea kutoka kizazi hadi kizazi, yakizalisha hali ya kipekee ya "akili iliyotawaliwa na ukaliaji wa mabavu", ambapo uhuru wa kucheza, kuota ndoto, kuwa na matumaini na kujenga utambulisho wao umeendelea kudhoofishwa.

Kwa kuwalenga watoto, Israel inaendelea kudhoofisha msingi wa jamii ya Kipalestina, kupunguza nguvu ya idadi ya watu wake na uwezo wa Wapalestina kuendelea kuwepo k**a taifa na kutumia haki yao ya kujiamulia mustakabali wao.

"Ulinzi, malezi na uhai wa watoto wa Kipalestina haviwezi kutenganishwa na haki ya watu wa Palestina ya kujitawala," alisema Muralidhar. "Kwa kuwalenga watoto, Israel inashambulia uwezo wenyewe wa watu wa Palestina kuendelea kuwepo na kuamua mustakabali wao."

Tume hiyo imeitaka Israel kusitisha mara moja ukiukwaji wa haki na uhalifu unaowalenga watoto wa Kipalestina. Pia imeitaka Israel kukomesha uwepo wake unaoendelea katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu, ikiwemo Jerusalem Mashariki, kwa kuzingatia maoni ya ushauri ya Mahak**a ya Kimataifa ya Haki (ICJ).

Aidha, Tume hiyo imevitambua vikosi vya kijeshi ndani ya vyombo vya usalama vya Israel vinavyohusika na mauaji na majeraha ya watoto wa Kipalestina, na kutoa mapendekezo kwa Israel pamoja na nchi zote wanachama wa Umoja wa Mataifa kuhakikisha kuwa wahusika wanawajibishwa kwa uhalifu huo.

Hatimaye, Tume imesisitiza kuwa jumuiya ya kimataifa ina wajibu wa kutekeleza majukumu yake chini ya sheria za kimataifa kwa kutaka mapigano yakome, Israel ikomeshe ukaliaji wake wa mabavu, na kuhakikisha uwajibikaji pamoja na upatikanaji wa haki kwa waathirika unakuwa sehemu muhimu ya mchakato wowote wa kisiasa, unaojengwa juu ya ushiriki wa maana wa Wapalestina, wakiwemo watoto.
....

Israel continues to commit genocide and other atrocity crimes by deliberately targeting Palestinian children

GENEVA – Israeli authorities and security forces have deliberately targeted Palestinian children resulting in genocide, crimes against humanity and war crimes in the Gaza Strip and war crimes in the West Bank, the UN Independent International Commission of Inquiry on the Occupied Palestinian Territory, including East Jerusalem, and Israel said in a new report today.

The Commission, which concluded last year that Israel had committed genocide against the Palestinian group in the Gaza Strip, found that the intense scale and systematic nature of the Israeli military operations have continued – resulting in unprecedented death, injury and trauma of Palestinian children.

The Commission reiterates that the deliberate targeting of children is one of the key elements establishing genocidal intent of the Israeli authorities and security forces to destroy the Palestinian group, in whole or in part, in Gaza.

“The evidence shows that Palestinian children have been deliberately targeted and killed by the Israeli security forces,” said Srinivasan Muralidhar, Chair of the Commission. “Even after the October 2025 ceasefire, children continue to be killed and seriously injured, with continued disregard by Israel for the ceasefire and for the protection owed to Palestinian children under international law.”

Severe physical and mental injuries, mass trauma, orphanhood, separation, disability, repeated displacements, starvation, and the collapse of education and healthcare have erased childhood and will continue to affect children in Gaza throughout their lives.

Palestinian children have been arrested and subjected to torture and other severe forms of mistreatment in Israeli prisons and detention facilities, with no information on their whereabouts. Israeli security forces have also used sexual violence against children as part of the collective shaming and oppression, entrenched within a prolonged, ethnic, gendered, and intergenerational pattern of Israeli occupation and hostilities.

Israel’s targeting of neonatal and maternity care centers in Gaza have directly harmed the survival of newborns and Palestinians’ reproductive future, including rises in miscarriages, birth defects and lasting vulnerabilities among newborns, resulting in the destruction of Palestinian newborn life and the population’s continuity. Starvation imposed by Israel through blockade and siege have further caused the death of Palestinian children and severely impacted the health of many others, depriving them of essential nutrition and increasing disease risks amid reduced immunization, food insecurity and destroyed health services.

In parallel, the dismantling and destruction of orphanages and education facilities in Gaza and the West Bank, including East Jerusalem, have obstructed children’s cognitive, social and emotional care and development and disrupted the foundations of Palestinian society.

“Even if the bombs and guns fall silent in Gaza and West Bank, Palestinian children will not simply recover overnight,” said Muralidhar. “The destruction of their health, education and development is irreversible.”

Palestinian children have suffered immense psychological harm, having been stripped of any sense of safety and future. Mental harm is an intergenerational condition, producing a distinctive “occupied psyche” in which the freedom to play, imagine, hope, and develop an identity has been eroded.

By targeting children, Israel is eroding the foundational structure of Palestinian society, weakening the demographic vitality, and overall capacity of the Palestinian people to sustain and exercise its right to determine its future as a people.

“The protection, care and survival of Palestinian children are inseparable from the Palestinian people’s right to self-determination,” said Muralidhar. “By targeting children, Israel is attacking the very capacity of the Palestinian people to exist and to determine their future.”

The Commission calls for Israel to cease committing violations and crimes against and affecting Palestinian children. The Commission further calls for the end of Israel’s continuing presence in the occupied West Bank, including East Jerusalem, in compliance with the advisory opinion of the International Court of Justice.

The Commission has identified military units within the Israeli security forces responsible for killing and injuring of Palestinian children and makes recommendations to Israel and to all Member States to ensure accountability for such crimes.

The international community as a whole must uphold their international legal obligations and call for an end to the hostilities, for Israel to end its occupation and to prioritize accountability and access to justice for victims as an integral component of any political process, grounded in the meaningful participation of Palestinians, including children.

23/06/2026

MJADALA WA KITAALUMA: JE, AMANI ILIKUWA MUHIMU KWAO? 🧠🏛️🇵🇸
​Katika mjadala mzito uliofanyika Oxford Union, wataalamu na mashahidi wameibua hoja nzito zinazotilia shaka nia ya kweli ya utawala wa Israel katika kufikia amani.

​Uhalisia wa Simulizi hii:
​📍 Ushuhuda wa Kutisha: Daktari Nick Maynard, aliyewahi kuhudumu katika maeneo yaliyoathirika, ametoa ushuhuda wa kusikitisha akielezea vitendo vya ukatili anavyovishuhudia, akiviita mauaji ya kimbari na usafishaji wa kikabila.

​📍 Mtazamo wa Kihistoria: Mwanahistoria Ilan Pappe amechambua jinsi simulizi za kihistoria zinavyotumiwa kupotosha ukweli na kujenga taswira ya uongo ya "mwathiriwa" ili kuficha ubaguzi na uvamizi.

​📍 Uamuzi wa Wengi: Kwa ushindi wa kura nyingi, mjadala huu umethibitisha kuwa ulimwengu unaanza kuona na kuelewa uhalisia wa ubaguzi na dhuluma inayofanyika dhidi ya haki za binadamu.

​"Ukweli hauwezi kufichwa milele. Ni wakati wa kusimama upande sahihi wa historia." 🕊️🌍

​FREE PALESTINA 🇵🇸🇵🇸🇵🇸
Tafadhali fuatilia (Follow), shiriki (Share) na Like kurasa zetu ili kusaidia kuongeza uelewa na kusimama pamoja katika kudai haki kwa watu wa Palestina dhidi ya utawala wa ubaguzi wa rangi (Apartheid).

​Kila mmoja wetu ana nafasi ya kuwa sauti ya wasio na sauti.

22/06/2026

NANI NI GAIDI? NI WAKATI WA KUREKEBISHA LUGHA YETU 🧠🌍
​Video hii inaleta mtazamo mpya wa kihistoria kuhusu jinsi tunavyotumia maneno k**a "ugaidi" na "upinzani".

​Uhalisia wa Simulizi hii:
​📍 Mfano wa Kihistoria: Mzungumzaji anatoa mfano wa Norway wakati wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia (1940-1945). Wakati Norway ilipokaliwa kwa mabavu, watu wake walipigana kwa ajili ya uhuru wao.

​📍 Mtazamo wa "Occupier": Wale waliokuwa wakiikalia Norway walikuwa wakiwaita wapiganaji wa Norway "terrorists" (gaidi). Lakini historia inawakumbuka wapiganaji hao k**a mashujaa wa upinzani.

​📍 Wito wa Kurekebisha Lugha: Mzungumzaji anatoa wito wa "recalibrate" (kurekebisha/kuchunguza upya) lugha tunayotumia wakati tunazungumzia matukio ya sasa. Inatuhoji: Nani anayechagua nani ni gaidi na nani ni shujaa?.

​📍 Uhusiano na Sasa: Hoja kuu ni kuelewa tofauti kati ya wale wanaopigania uhuru na jinsi nchi k**a Israel inavyotumia lugha ya "ugaidi" dhidi ya Wapalestina wanaopigania haki zao.

​"Historia inatufundisha kuwa wapiganaji wa uhuru mara nyingi wameitwa magaidi na wakoloni. Je, tunapaswa kuchunguza upya nani anayeitwa gaidi?" 🕊️✊

​FREE PALESTINA 🇵🇸🇵🇸🇵🇸
​Tafadhali fuatilia (Follow), shiriki (Share) na Like kurasa zetu ili kusaidia kuongeza uelewa na kusimama pamoja katika kudai haki kwa watu wa Palestina dhidi ya utawala wa ubaguzi wa rangi (Apartheid).

​Kila mmoja wetu ana nafasi ya kuwa sauti ya wasio na sauti.

22/06/2026

HISTORIA HAISAHAU: UKWELI KUHUSU GAZA UTAWAKABILI WAHUSIKA ⚖️⏳

​Ukatili unaoendelea Gaza ni doa kubwa kwa ubinadamu. Tucker Carlson ameweka wazi mtazamo ambao wengi wanaanza kuukubali: kuwa kadiri muda unavyosonga na ukweli wa yaliyotendeka Gaza unapokuja kujulikana kikamilifu, msimamo wa dunia utabadilika.
​Pointi za Msingi:

📍 Ukweli Uliofichika: Hivi sasa, dunia bado haijapata picha kamili ya ukatili wote uliofanywa Gaza. Ukweli huu unapodhihirika, hakuna mtu atakayeweza kusimama kidete kutetea vitendo hivyo.

📍 Mwangwi wa Kihistoria: K**a ilivyokuwa kwa viongozi wa kinazi waliofikishwa kwenye vyombo vya sheria (Nuremberg) baada ya vita, ni wazi kuwa viongozi wanaohusika na maangamizi ya sasa watawajibishwa.

📍 Wito wa Haki: Ubinadamu unadai haki. Hatua za kisheria ni lazima zichukuliwe dhidi ya wote wanaohusika na ukiukwaji huu wa kutisha wa haki za binadamu.

​"Historia inatufundisha kuwa ukweli una njia ya kujitokeza, na hakuna anayeweza kukwepa mkono wa sheria baada ya uhalifu wa kivita kufichuka." 🌍🚨

​FREE PALESTINA 🇵🇸🇵🇸🇵🇸
Tafadhali (Follow), (Share) na (Like) kurasa zetu ili kueneza ukweli huu na kusimama pamoja kudai haki.

21/06/2026

LADHA ZA HISTORIA YA PALESTINA 🥘✨
​Unapoangalia chakula hiki, huenda ukaona k**a soseji za kawaida, lakini hii ni zaidi ya chakula—ni sehemu ya utamaduni na historia tajiri inayotoka katika mji wa kihistoria wa Nablus.

​Uhalisia wa Simulizi hii:
📍 Ubunifu wa Kiasili: Vyakula vya Palestina vinabeba utambulisho wa kina. Ni sanaa inayorithishwa kutoka kizazi hadi kizazi, ikiwakilisha ukarimu na upendo wa watu wa ardhi hiyo.

📍 Nablus na Utamaduni wake: Nablus inajulikana kwa vyakula vyake vya kipekee ambavyo ni alama ya ustahimilivu na utajiri wa utamaduni wa Wapalestina.

📍 Uhifadhi wa Utambulisho: Kila sahani inayotayarishwa ni ushahidi wa utamaduni unaokataa kufutika, hata katika nyakati ngumu zaidi.

​"Chakula cha Palestina si tu kitoweo, ni simulizi ya ardhi, watu, na imani yao." 🕊️🌍

​FREE PALESTINA 🇵🇸🇵🇸🇵🇸
Tafadhali fuatilia (Follow), shiriki (Share) na Like kurasa zetu ili kusaidia kuongeza uelewa na kusimama pamoja katika kudai haki kwa watu wa Palestina dhidi ya utawala wa ubaguzi wa rangi (Apartheid).

​Kila mmoja wetu ana nafasi ya kuwa sauti ya wasio na sauti.

21/06/2026

SAUTI YA UKWELI: JE, DUNIA INAANGALIA NINI? 🌍📢
​Rais wa Belarus, Aleksander Lukashenko, ametoa wito mzito kuhusu hali ya Gaza akieleza:

​📍 Uharibifu wa Sifa: Israel inakabiliwa na changamoto kubwa ya sifa mbaya duniani kutokana na operesheni zake za kijeshi Gaza.

​📍 Ulinganifu wa Historia: Lukashenko amehoji ni kwa nini ulimwengu unaendelea kuzungumzia Holocaust iliyowapata Wayahudi, wakati ambapo "wanajifanyia wenyewe" kitendo cha kikatili kwa kuua maelfu ya watu, hususan wanawake na watoto.

​📍 Wito wa Uwajibikaji: Amesema kuwa Israel inapaswa kuwa "makini zaidi" kwa sababu matendo haya yanashuhudiwa na ulimwengu mzima.

​"Ubinadamu haupimiwi kwa upande mmoja, bali kwa thamani ya kila maisha. Ni wakati wa kusimama na kutafakari kuhusu haki kwa wote." 🕊️✊

​FREE PALESTINA 🇵🇸🇵🇸🇵🇸
​Tafadhali fuatilia (Follow), shiriki (Share) na Like kurasa zetu ili kusaidia kuongeza uelewa na kusimama pamoja katika kudai haki kwa watu wa Palestina.

​Kila mmoja wetu ana nafasi ya kuwa sauti ya wasio na sauti.

21/06/2026

MTHAWAMET BATATA: LADHA YA ASILI YA KIPEKEE NA VALIEATS 🥔✨
​Tunajifunza kuandaa Mthawamet Batata, sahani pendwa ya viazi yenye ladha ya kipekee na mguso wa asili, ikitayarishwa kwa ustadi mkubwa na mpishi mahiri VALIEATS!

​Uhalisia wa Simulizi hii:
​📍 Ufundi wa VALIEATS: Mpishi huyu anatuonyesha hatua kwa hatua jinsi ya kubadilisha viazi vya kawaida kuwa kitoweo kitamu, akitumia viungo asilia na mafuta ya mzeituni.

​📍 Utajiri wa Utamaduni: Mthawamet Batata si chakula tu, bali ni urithi wa mapishi unaoakisi historia na utambulisho wa ardhi hiyo tajiri.

​📍 Urahisi na Ladha: Ni sahani inayounganisha familia, ikionesha jinsi mapishi rahisi yanavyoweza kuleta furaha na umoja jikoni.
​"Kupika ni lugha ya upendo; asante VALIEATS kwa kutukumbusha uzuri wa ladha za nyumbani." 🕊️🌍

​FREE PALESTINA 🇵🇸🇵🇸🇵🇸
Tafadhali fuatilia (Follow), shiriki (Share) na Like kurasa zetu ili kusaidia kuongeza uelewa na kusimama pamoja katika kudai haki kwa watu wa Palestina dhidi ya utawala wa ubaguzi wa rangi (Apartheid).

​Kila mmoja wetu ana nafasi ya kuwa sauti ya wasio na sauti.

20/06/2026

UHALISIA WA KUSIKITISHA: GHALA LA HAKI ZA BINADAMU LINAITA MAMLAKA YA KIMATAIFA! 🚨🇵🇸
​Volker Türk, Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, ametoa taarifa nzito na ya kushtua kuhusu hali ya Gaza.

​Uhalisia wa Simulizi hii:
​📍 Mauaji ya raia: Tangu kutangazwa kwa msimamo wa kusitisha mapigano Oktoba iliyopita, vikosi vya Israel vimeua takriban Wapalestina 1,000, wengi wao wakiwa ni raia.

​📍 Kusukumwa kwenye maeneo finyu: Mamlaka za Israel zinaendelea kuwasukuma Wapalestina kwenye maeneo madogo zaidi ya eneo hilo, hali inayozidi kuhatarisha maisha yao.

​📍 Vikwazo vya misaada: Vikwazo vimewekwa dhidi ya misaada ya kuokoa maisha, hali inayozidisha mateso ya watu walio katika hali mbaya.

​📍 Hali ya Ukingo wa Magharibi (West Bank): Hali si shwari pia Ukingo wa Magharibi, ambapo vikosi vya usalama na walowezi wanaharakisha uharibifu wa jamii na kunyakua ardhi kwa kasi ya kutisha.

​"Wito wa haki za binadamu ni wito wa ubinadamu. Dunia inapaswa kusimama kidete na kukataa maovu haya dhidi ya Wapalestina." 🕊️🌍

​FREE PALESTINA 🇵🇸🇵🇸🇵🇸
​Tafadhali fuatilia (Follow), shiriki (Share) na Like kurasa zetu ili kusaidia kuongeza uelewa na kusimama pamoja katika kudai haki kwa watu wa Palestina dhidi ya ukatili huu.

Kila mmoja wetu ana nafasi ya kuwa sauti ya wasio na sauti.

Address

612 United Nations Road
Dar Es Salaam
P.OBOX20307

Opening Hours

Monday 09:00 - 15:00
Tuesday 09:00 - 15:00
Wednesday 09:00 - 15:00
Thursday 09:00 - 15:00
Friday 09:00 - 13:30

Telephone

+255222150643

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Embassy of the State of Palestine in Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Embassy of the State of Palestine in Tanzania:

Share