12/07/2024
Matukio mbalimbali katika picha wakati Mkurugenzi Mkuu wa PURA, Mhandisi Charles Sangweni alipotembelea banda la Mamlaka katika Maonesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) leo Julai 12, 2024 yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere, Barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam.
Mha. Sangweni pia ametembelea mabanda mengine ya taasisi za sekta ya nishati ikiwemo Wizara ya Nishati, Mamlaka ya Huduma za Udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA), Shirika la Maendeleo ya Petroli (TPDC), Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) pamoja na Mamlaka ya Udhibiti wa Utafutaji na Uchimbaji wa Mafuta na Gesi Asilia Zanzibar (ZPRA).