TPATZ Main functions of TPA is to promote the use, development & management of Ports and their hinterlands.

The Tanzania Ports Authority (TPA) was established by the Ports Act No. 17 of 2004 as landlord port authority. It operates a system of ports serving the Tanzania hinterland and the land-linked countries of Zambia, Democratic Republic of Congo (DRC), Burundi, Rwanda, Malawi, Uganda and Zimbabwe. The Authority performs the role of landlord and operator with the main functions of promoting the use, development and management of the ports and their hinterlands, entering contracts for the purpose of delegating the powers of the Authority through licensing and concessions for port services. The TPA manages a diverse system of sea and inland waterways on Tanzania's Mainland. Dar es Salaam, Tanga, and Mtwara are the major seaports; Kilwa, Lindi, Mafia, Pangani, and Bagamoyo are the smaller seaports; and Lake Victoria, Tanganyika, and Nyasa are the lake ports.

18/09/2026
Baraza Dogo la Majadiliano (JIC) la Bandari za Ziwa Victoria limesisitiza umuhimu wa ushirikiano, bidii na mawasiliano b...
18/09/2026

Baraza Dogo la Majadiliano (JIC) la Bandari za Ziwa Victoria limesisitiza umuhimu wa ushirikiano, bidii na mawasiliano bora miongoni mwa wafanyakazi katika kuongeza tija na ufanisi wa utendaji kazi wa Mamlaka.

Msisitizo huo umetolewa na Mwenyekiti wa Baraza hilo, Bi. Rosemary Ndesamburo, ambaye pia ni Meneja wa Bandari za Ziwa Victoria, wakati wa Kikao cha 62 cha Baraza Dogo la Majadiliano (JIC) kilichofanyika tarehe 16 na 17 Septemba 2026.

Kikao hicho kimejadili masuala mbalimbali yanayohusu utendaji na maendeleo ya Bandari za Ziwa Victoria, ikiwemo mafanikio yaliyopatikana, pamoja na masuala yanayohusu maslahi na ustawi wa wafanyakazi, kwa lengo la kuimarisha mazingira ya kazi na utekelezaji wa majukumu ya Mamlaka.

Akizungumza katika kikao hicho, Bi. Ndesamburo amewasisitiza wajumbe kufanya kazi kwa bidii, ushirikiano na upendo, huku wakizingatia wajibu wao katika kuhakikisha mijadala na maamuzi ya Baraza yanakuwa na mchango chanya katika kuongeza tija na ufanisi wa utendaji kazi.

Amesema JIC linaendelea kuwa jukwaa muhimu la mawasiliano, ushirikiano na uelewano mahali pa kazi, linalowezesha kujadili masuala mbalimbali ya wafanyakazi na taasisi kwa pamoja, hatua inayolenga kuimarisha ustawi wa wafanyakazi na kufanikisha malengo ya Mamlaka.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya, Bw. Abdallah Mitawi, tarehe 17 Septemba 2026 amefanya ziara katika Mamlaka ya Usimamizi ...
18/09/2026

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya, Bw. Abdallah Mitawi, tarehe 17 Septemba 2026 amefanya ziara katika Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), ikiwa na lengo la kufahamu kwa kina shughuli zinazotekelezwa na Mamlaka hiyo pamoja na mchango wa bandari katika kukuza biashara, usafirishaji na uchumi wa Taifa.

Katika ziara hiyo, Bw. Mitawi amepokelewa na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Mha. Dkt. Baraka Mdima, kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa TPA.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Bw. Mitawi ameipongeza Menejimenti ya TPA kwa mafanikio yaliyopatikana katika kuhudumia shehena na kuongeza mapato kupitia bandari zinazosimamiwa na Mamlaka hiyo.

Amesema mafanikio hayo yanadhihirisha umuhimu wa kuendelea kuboresha ufanisi wa huduma za bandari, kuimarisha matumizi ya teknolojia na ubunifu, pamoja na kuweka mazingira rafiki kwa wafanyabiashara na wadau wa sekta ya usafirishaji.

Kwa upande wake, Mha. Dkt. Baraka Mdima amemshukuru Naibu Katibu Mkuu kwa kutembelea TPA na kueleza kuwa Mamlaka itaendelea kutekeleza kwa ufanisi maelekezo na mipango ya Serikali katika kuboresha huduma za bandari na kuongeza mchango wake katika uchumi wa Taifa.

Dkt. Mdima amesema TPA itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wa sekta ya usafirishaji na biashara, wakiwemo wadau kutoka Sekta Binafsi, katika kuongeza ufanisi na tija katika sekta ya bandari, kuboresha huduma za kuhudumia na kushughulikia mizigo, pamoja na kuimarisha ushindani wa bandari za Tanzania.

Ziara hiyo ni sehemu ya jitihada za Wizara ya Uchukuzi na TPA za kuimarisha ushirikiano na ufuatiliaji wa utekelezaji wa mikakati ya Serikali katika kuendeleza sekta ya usafirishaji, kukuza biashara na kuimarisha nafasi ya Tanzania k**a kitovu cha biashara na usafirishaji katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.

wizara_ya_uchukuzi Msemaji Mkuu wa Serikali Maelezo News

Serikali imesema katika kuongeza ufanisi katika sekta ya Bandari nchini kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania...
17/09/2026

Serikali imesema katika kuongeza ufanisi katika sekta ya Bandari nchini kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) imetekeleza miradi mbalimbali ya kuboresha miundombinu ya uhudumiaji wa shehena ili kuongeza ufanisi katika sekta ya Uchukuzi.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Kigoma, Mhe.Dkt.Rashid Chuachua kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa huo, wakati akifungua kikao cha Wadau wa Sekta ya Usafirishaji, Ushoroba wa Kati kilichofanyika Septemba 16, 2026 Mkoani huo.

Dkt. Chuachua amesema anaamini mijadala itakayoibuka itakuja na ufumbuzi wa changamoto katika usafirishaji kupitia Ushoroba wa Kati.

Katika salamu zake za ukaribisho Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TPA Mha. Dkt. Baraka Mdima, amesema Ushoroba wa Kati ni moja kati ya mihimili muhimu ya biashara,si kwa Kigoma pekee bali kwa Taifa zima kwani umekuwa daraja la kuiunganisha Tanzania na nchi zingine katika uchukuzi wa shehena.

Aidha Dkt.Mdima amesema jumla ya shehena iliyohudumiwa na Bandari zote zinazosimamiwa na TPA kwa mwaka wa fedha uliopita, ilifikia tani milioni 39.898 ambayo ni sawa na ongezeko la asilimia 21.8 ukilinganisha na mwaka uliotangulia.

Dkt.Mdima amesema kikao cha Wadau wa Ushoroba wa Kati kimeandaliwa mahususi kabisa ili kwa pamoja tupate fursa ya kujifanyia tathimini ya tulichokifanya mwaka uliopita na kutafakari namna bora kuboresha ili kuongeza ufanisi katika sekta ya Uchukuzi nchini.

Akizungumza mapema Meneja wa Bandari za Ziwa Tanganyika Bw.Edward Mabula amesema Serikali kupitia TPA imefanya uwekezaji wa zaidi ya bilioni 100 ili kutengenza mazingira wezeshi ya kuhudumia shehena inayopita katika Bandari ya Kigoma.

Akiongea kuhusu kuongezeka kwa shehena Bw.Mabula amesema imeongezeka kutoka zaidi ya tani 200,000 mpaka kufikia tani 815,285 kwa mwaka wa fedha wa 2025/2026 na baada ya maboresho matarajio ni kufika mpaka tani milioni 2.

wizara_ya_uchukuzi Msemaji Mkuu wa Serikali Maelezo News

16/09/2026

Kikao cha siku moja kilichoandaliwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) kwa lengo la kuwakutanisha Wadau wa Usafirishaji kupitia ushoroba wa kati kimefunguliwa rasmi na Mkuu wa Wilaya ya Kigoma, Dkt. Rashid Chuachua, kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma.

Kikao hicho kinachofanyika Mjini Kigoma, kimewakutanisha wadau mbalimbali kutoka katika sekta ya Uchukuzi na Usafirishaji, wakiwemo wawakilishi wa taasisi za Serikali na sekta binafsi.

wizara_ya_uchukuzi Maelezo News Msemaji Mkuu wa Serikali

A new week brings new opportunities to connect, move cargo and power trade. At TPA, we are ready to deliver efficiency, ...
14/09/2026

A new week brings new opportunities to connect, move cargo and power trade. At TPA, we are ready to deliver efficiency, safety and world class service across all our ports.

Wishing our customers, partners and stakeholders a productive week ahead!


MondayMotivation

Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) imepongezwa kwa kukutanisha Wadau wa Bandari ya Mtwara kwa lengo kujadili...
11/09/2026

Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) imepongezwa kwa kukutanisha Wadau wa Bandari ya Mtwara kwa lengo kujadili ili kuiwezesha bandari hiyo kuendelea kuhudumia zao la korosho kuelekea masoko ya kimataifa.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Mhe. Abdallah Mwaipaya kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa huo wakati akifungua Mkutano wa Wadau wa Bandari ya Mtwara uliofanyika katika ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT), mjini Mtwara.

Aidha Mhe. Mwaipaya amesema Serikali ya awamu ya sita chini Rais Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan imeijengea Bandari ya Mtwara uwezo kwa kuimarisha miundombinu ya kuhudumia shehena ili kuongeza ufanisi zaidi.

Awali katika salamu za ukaribisho,Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TPA Mha. Dkt. Baraka Mdima kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa TPA, amesema lengo la Mkutano huo ni kujadiliana kwa uwazi changamoto,mafanikio na namna bora ya kutafuta ufumbuzi utakaoongeza ufanisi wa uhudumiaji wa shehena.

Naye Meneja wa Bandari ya Mtwara Bw. Ferdinand Nyathi ameeleza ufanisi na utayari wa Bandari hiyo katika msimu mpya wa korosho kwa kuongeza vifaa vya kuhudumia meli k**a Gottwald na Folklift.

wizara_ya_uchukuzi Msemaji Young Muzlim Maelezo News

Serikali imeshauriwa kuongeza maeneo zaidi yanayozunguka Mradi wa Usanifu na Ujenzi wa Bandari ya Kisiwa/Mgao Mkoani Mtw...
11/09/2026

Serikali imeshauriwa kuongeza maeneo zaidi yanayozunguka Mradi wa Usanifu na Ujenzi wa Bandari ya Kisiwa/Mgao Mkoani Mtwara ili kuweka nafasi ya upanuzi wa Bandari hiyo siku zijazo na kuepusha gharama kubwa za fidia na ununuzi wa ardhi zitakazoweza kujitokeza wakati wa utekelezaji wa miradi mikubwa ya baadaye.

Ushauri huo umetolewa tarehe 9 Septemba, 2026 na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Mhe. Selemani Kakoso (Mb) wakati Kamati hiyo ilipotembelea na kukagua maendeleo ya utekelezaji wa Mradi wa Bandari ya Kisiwa/Mgao.

Mhe. Kakoso amesema uzoefu unaonesha kuwa kuchukua maeneo madogo wakati wa kuanzisha miradi mikubwa huweza kuongeza gharama pale inapohitajika kupanua miradi hiyo baadaye, hivyo Serikali inapaswa kuwa na mtazamo wa muda mrefu kwa kuhakikisha maeneo muhimu yanayozunguka mradi yanahifadhiwa mapema.

Aidha, Kamati hiyo imesisitiza umuhimu wa kuanza kwa wakati ujenzi wa barabara ya kiunganishi cha lami itakayounganisha Bandari ya Kisiwa/Mgao na Mtwara ili kuhakikisha miundombinu ya usafiri na usafirishaji inaenda sambamba na maendeleo ya Bandari na kuwezesha shughuli za Bandari kuanza mara tu baada ya kukamilika kwa mradi.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Uchukuzi, Mhe. David Kihenzile ameihakikishia Kamati hiyo kuwa Serikali itatekeleza maelekezo yote yaliyotolewa na kuendelea kusimamia kwa karibu utekelezaji wa miradi ya Sekta ya Uchukuzi inayotekelezwa Mkoani Mtwara ili ikamilike kwa wakati na kwa viwango vinavyokusudiwa.

Naye Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TPA Mhandisi Dkt. Baraka Mdima, kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa TPA amesema Mradi wa Ujenzi wa Bandari ya Kisiwa/Mgao unatekelezwa kwa gharama ya Shilingi Bilioni 435 na unalenga kuongeza uwezo wa Bandari ya Mtwara kuhudumia mizigo mikubwa ikiwemo kupitia upanuzi wa miundombinu ya Bandari na kuongeza uwezo wa kuhudumia meli kubwa.

Amesema mradi huo kwa sasa umefikia asilimia 48 ya utekelezaji na unatarajiwa kukamilika Septemba, 2028 hatua inayotarajiwa kuimarisha nafasi ya Bandari ya Mtwara katika kuhudumia biashara na usafirishaji wa mizigo ndani na nje ya Tanzania.

Baraza Kuu la Wafanyakazi (MWC) la  Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) tarehe 9 Septemba 2026 limefanya kika...
10/09/2026

Baraza Kuu la Wafanyakazi (MWC) la Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) tarehe 9 Septemba 2026 limefanya kikao chake cha 40 mjini Morogoro.

Kikao hicho kimelenga kupokea na kujadili taarifa ya utekelezaji wa Bajeti kwa mwaka wa Fedha 2025/2026 pamoja na mpango wa Bajeti iliyoidhinishwa na Wizara ya Uchukuzi kwa Mwaka wa Fedha 2026/ 2027.

Pamoja na mambo mengine Baraza hilo pia limemuaga aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi (DOWUTA) Tawi la Makao Makuu aliyemaliza muda wa utumishi kisheria Bw. Benjamin Kihanga

Kikao hicho kimeongozwa na Naibu Mkurugenzi Mkuu (TPA) Dkt. Baraka R. Mdima kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu Bw. Plasduce M. Mbossa.

Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) inawatakia Wanafunzi wote wa Darasa la Saba kote Nchini, kila la kheri ka...
09/09/2026

Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) inawatakia Wanafunzi wote wa Darasa la Saba kote Nchini, kila la kheri katika Mitihani yao ya kumaliza Elimu ya Msingi.

Address

P. O. Box 9184 DSM
Dar Es Salaam
255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when TPATZ posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share