Mediawireexpress

Mediawireexpress Your News Hub for Uncovering Africa's untold narratives , one video at a time .

19/09/2026

Mkuu wa Wilaya ya Serengeti mkoani Mara, Mhe. Angellina Marco Lubela, ameongoza mazishi ya Mkami Nyaimwamu Kisogiro, mama mzazi wa Diwani wa Kinyerezi na Naibu Meya wa Jiji la Dar es Salaam, John Ryoba Mrema, huku akitoa rai kwa wananchi wa wilaya hiyo kujiandaa mapema kukabiliana na uwezekano wa mvua kubwa zinazotarajiwa kunyesha mwishoni mwa Oktoba 2026.

Mkami Nyaimwamu Kisogiro alifariki dunia Septemba 15, 2026, akiwa na umri wa miaka 62, na amezikwa katika Wilaya ya Serengeti, mkoani Mara, ambako mazishi yake yamehudhuriwa na viongozi, ndugu, jamaa na wananchi.

Akizungumza katika mazishi hayo, Mhe. Lubela amewataka wananchi kuchukua tahadhari na kuanza maandalizi mapema, hasa katika maeneo yanayoweza kukumbwa na mafuriko kutokana na mvua kubwa.

Amesema watafiti wa hali ya hewa wameeleza uwezekano wa kuwepo kwa mvua nyingi katika kipindi kijacho, hivyo wananchi wanapaswa kutumia muda uliopo kufanya maandalizi yatakayosaidia kupunguza madhara yanayoweza kujitokeza.

“Kwa hiyo, natoa rai kwa wananchi wetu tuendelee kuchukua tahadhari. Kwenye maeneo tunayoishi, tuhakikishe tunazibua mitaro ili maji yapite kwa urahisi,” amesema.

Mkuu huyo wa Wilaya pia amewataka wananchi wenye ndugu au familia zinazoishi katika maeneo ya mabondeni kuwashauri kuhama mapema kwenda maeneo salama, badala ya kusubiri hali ya mvua kuwa mbaya.

Amesema hatua za mapema ni muhimu katika kulinda maisha ya wananchi na mali zao, hasa iwapo mvua hizo zitasababisha ongezeko la maji na mafuriko katika maeneo hatarishi.

Mbali na tahadhari za miundombinu na makazi, Mhe. Lubela amewataka wananchi kujiandaa kwa upande wa mahitaji ya msingi, ikiwemo kutunza akiba ya chakula ili kukabiliana na changamoto zinazoweza kujitokeza wakati wa dharura.

“Kama una ndugu yako anayeishi bondeni, mshauri ahame mapema. La mwisho kabisa, tutunzeni vyakula wananchi wenzangu, kwani mvua hizi na dharura zitakuwepo,” amesema.

18/09/2026

Shirika la Reli Tanzania (TRC) limefanya kikao cha kwanza na mshauri mwelekezi Kampuni ya SYSTRA kutoka Ufaransa, inayotarajiwa kufanya upembuzi yakinifu wa mradi wa reli za mjini (Monorail) jijini Dar es Salaam ambapo limesema sekta binfasi ndiyo itakayotekeleza mradi huo.

Kikao hicho kilichofanyika Septemba 17, 2026 jijini Dar Es Salaam, ni kiashiria cha kuanza matayarisho ya mradi huo unaolenga kuboresha usafiri wa umma na kupunguza msongamano wa magari katika jiji hilo la biashara.

Akizungumza na waandishi wa habari Mkurugenzi Mkuu wa TRC, Mhandisi Machibya Shiwa, amesema, sekta binafsi imepewa takribani asilimia 70 katika utekelezaji wa dira 2025, hivyo hiyo ni fursa kutekeleza mradi huo.

“Natoa wito kwa sekta binafsi kujitokeza kuchangamkia fursa hiyo kufuatia nafasi kubwa waliyonayo ya kuongeza uwekezaji nchini, kufuatia Serikali kuendelea kuweka mazingira wezeshi ya kisheria, kisera na kitaasisi ili kuvutia uwekezaji wa ndani na nje ya nchi’’, amesema Shiwa.

Mradi huo wa ujenzi wa reli moja unalenga kukabiliana na ongezeko la mahitaji ya usafiri linalotokana na ukuaji wa Jiji la Dar es Salaam ambapo kufikia 2030 linatarajiwa kuwa na watu milioni kumi 10.

“Kuanza kwa mchakato huu ni hatua muhimu katika maandalizi ya kujenga mfumo wa kisasa wa usafiri wa Mijini. Upembuzi yakinifu utatupatia msingi wa kitaalamu wa kubaini namna bora ya kutekeleza mradi kwa kuzingatia mahitaji ya wananchi na ukuaji wa jiji la Dar es Salaam," amesema Shiwa.

Reli hiyo inatarajiwa kupunguza muda na gharama za safari pamoja na msongamano wa magari na kuwawezesha wananchi kufika kwa urahisi kwenye maeneo ya kazi, biashara na huduma.

Kwa mujibu wa Mhandisi Shiwa, kiuchumi mradi huo utaongeza ufanisi wa biashara, kufungua fursa za ajira na uwekezaji na kuongeza thamani ya maeneo yanayohudumiwa na reli na kupunguza hasara zinazotokana na muda unaopotea katika foleni.

16/09/2026

Dada mkubwa wa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu, Mchungaji Rose Masesa, amekanusha madai yaliyotolewa na Mwanaharakati Mange Kimambi kwamba familia ya Lissu imenunuliwa na inatumia vibaya fedha za chama, akisema tuhuma hizo hazina ukweli wowote.

Akizungumza nje ya Mahak**a Kuu, Masjala Ndogo ya Dar es Salaam leo Jumatano, Septemba 16, 2026, Mchungaji Masesa amesema amekuwa akimsoma Mange Kimambi kupitia mitandao ya kijamii na wakati mwingine amekuwa akikubaliana na harakati zake, lakini ameshangazwa kuona familia yao ikiingizwa katika tuhuma ambazo, kwa mujibu wake, hazina msingi.

Amesema yeye binafsi ameacha Kanisa na familia yake Songea na kufika Dar es Salaam kuonyesha mshik**ano kwa ndugu yake, akisisitiza kuwa uwepo wa familia mahak**ani si kwa sababu hawana kazi, bali ni sehemu ya kumpa Lissu moyo na kumfariji anapowaona wakati wa usikilizwaji wa kesi inayomkabili.

“Mimi namsoma Mange Kimambi tu kwenye mitandao na kuna wakati nakubaliana na harakati zake, ila nimeshangaa familia yetu kuingizwa kwenye tuhuma ambazo hazina ukweli wowote. Mimi nimeacha Kanisa Songea, nimeacha familia kuja kuonesha mshik**ano. Lissu Anapotuona Mahak**ani anasikia faraja,” amesema Mch. Masesa.

Mchungaji Masesa amesema familia ya Lissu iko pamoja, ina mshik**ano na haiwezi kununuliwa wala kumsaliti Lissu, akimtaja ndugu yake kuwa ni mtu mwaminifu, mwadilifu na anayependa nchi yake. Amesema tangu alipomfahamu hajawahi kuona tabia zinazoweza kumfanya aamini tuhuma kwamba ni mhaini au mhalifu.

Aidha, amewataka Watanzania kutokuwa wepesi kuamini kila kinachochapishwa kwenye mitandao ya kijamii bila kukichunguza na kukithibitisha, akisema kipindi hiki ni kigumu na taarifa nyingi zinaweza kutolewa. Pia amekanusha madai kwamba familia ya Lissu imekuwa ikiishi hotelini kwa kutumia fedha za CHADEMA, akisema watu wanaotajwa katika madai hayo wana familia zao na wana maisha yao.

Masesa amesema yupo pamoja na watoto na wajukuu zake kwa amani na kwamba familia ya Lissu inaendelea kusubiri maamuzi ya Mungu kuhusu mwenendo wa kesi hiyo, akisisitiza kuwa hawawezi kununuliwa kwa jambo lolote. Amewataka Watanzania kuchukulia kwa tahadhari madai yanayotolewa mtandaoni, huku akisema Mange Kimambi na watu wengine wanaohusishwa na madai hayo wanapaswa kuacha kueneza taarifa zisizothibitishwa kuhusu familia hiyo.

Kundi la EPP katika Bunge la Ulaya limemteua Mwanasheria, mwanaharakati wa haki za binadamu na mwanasiasa wa Tanzania, T...
16/09/2026

Kundi la EPP katika Bunge la Ulaya limemteua Mwanasheria, mwanaharakati wa haki za binadamu na mwanasiasa wa Tanzania, Tundu Lissu, kuwa mgombea wa Tuzo ya Sakharov ya Uhuru wa Mawazo.

Lissu alinusurika jaribio la kuuawa mwaka 2017 na baadaye kurejea Tanzania, ambako aliendelea kutetea mageuzi ya kidemokrasia. Hata hivyo, amekumbana na kuk**atwa, mashtaka ya uhaini na kuzuiwa kushiriki katika uchaguzi wa urais wa mwaka 2025, huku chama chake pia kikizuiwa kushiriki katika uchaguzi huo.

Kwa mujibu wa EPP Group, kesi ya Lissu inaakisi kile kundi hilo linachokitaja kuwa kudhoofika kwa mfumo wa vyama vingi, ushindani wa kisiasa na demokrasia nchini Tanzania.

EPP imesema Lissu anawakilisha mchanganyiko wa ujasiri binafsi, msimamo wa kidemokrasia na umuhimu wa kisiasa katika mahusiano ya Ulaya na Afrika.

Kundi hilo limesema uteuzi huo unaonyesha msimamo wa Ulaya wa kuunga mkono watu wanaotetea demokrasia ya kikatiba na uhuru wa kisiasa barani Afrika na katika nchi nyingine zinazoshirikiana na Umoja wa Ulaya.

EPP pia imesema Lissu anawakilisha utetezi wa demokrasia, siasa za vyama vingi, utawala wa sheria na uhuru wa msingi, akifanya hivyo licha ya gharama kubwa binafsi alizokumbana nazo.

Tuzo ya Sakharov ya Uhuru wa Mawazo ni heshima ya juu inayotolewa na Umoja wa Ulaya kwa watu na taasisi zinazotambuliwa kwa mchango wao katika kutetea haki za binadamu na uhuru wa msingi.

Uteuzi wa Lissu sasa unamweka miongoni mwa majina yanayozingatiwa kwa tuzo hiyo, huku mchakato wa uteuzi na uamuzi wa mshindi ukiendelea ndani ya Bunge la Ulaya.

16/09/2026

Polisi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) wametumia mabomu ya machozi na kufyatua risasi za onyo kuwatawanya mamia ya watu waliokuwa wakiandamana katika mji mkuu, Kinshasa.

Waandamanaji hao walikuwa wakipinga mapendekezo ya mabadiliko ya Katiba yanayoweza kumruhusu Rais Félix Tshisekedi kugombea muhula wa tatu wa urais.

Mjadala huo umeibua wasiwasi na mvutano wa kisiasa kuhusu ukomo wa mihula ya urais nchini DRC. Kwa mujibu wa mfumo wa sasa wa Katiba, rais huchaguliwa kwa muhula wa miaka mitano na anaweza kuhudumu kwa mihula miwili.

Waandamanaji wanapinga mabadiliko yanayoweza kuondoa au kubadilisha masharti hayo, wakieleza kuwa hatua hiyo inaweza kumruhusu Tshisekedi kuwania tena urais baada ya kumaliza mihula yake inayoruhusiwa chini ya Katiba ya sasa.

Tshisekedi alichaguliwa kwa mara ya kwanza mwaka 2018 na akachaguliwa tena mwaka 2023. Mchakato wa marekebisho ya Katiba umeendelea kuwa suala lenye mjadala mkubwa wa kisiasa, huku wafuasi wa mabadiliko wakisisitiza umuhimu wa kuirekebisha Katiba na wapinzani wakihofia uwezekano wa kurefusha utawala wa rais.

Matukio ya Kinshasa yanaonyesha jinsi suala la ukomo wa mihula ya urais linavyoendelea kuwa nyeti katika siasa za DRC.

16/09/2026

Mamia ya raia nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) wameingia barabarani katika mji mkuu Kinshasa, kupinga mapendekezo ya mabadiliko ya Katiba yanayoweza kumruhusu Rais Félix Tshisekedi kugombea muhula wa tatu.

Polisi walitumia mabomu ya machozi na kufyatua risasi za onyo kuwatawanya waandamanaji, huku hali ya wasiwasi ikiongezeka katika baadhi ya maeneo ya mji huo.

Waandamanaji wanapinga mchakato huo wakidai kuwa mabadiliko ya Katiba yanaweza kubadilisha masharti ya sasa kuhusu ukomo wa mihula ya urais na hivyo kumwezesha Tshisekedi kuwania tena nafasi hiyo.

Tshisekedi alichaguliwa kuwa rais mwaka 2018 na akashinda uchaguzi wa mwaka 2023. Chini ya Katiba ya sasa, rais wa DRC anaweza kuhudumu kwa mihula miwili ya miaka mitano.

Mjadala kuhusu marekebisho ya Katiba umeendelea kuwa suala nyeti katika siasa za DRC, huku wafuasi wa mabadiliko wakisisitiza umuhimu wa kufanya marekebisho ya kikatiba, wakati wapinzani wakipinga uwezekano wa kubadilisha masharti yanayohusu ukomo wa mihula ya urais.

16/09/2026

Waziri Mkuu wa Tanzania, Dkt. Mwigulu Nchemba, amesema si kila changamoto au suala linalojitokeza nchini linapaswa kukabiliwa kwa namna ileile, akitumia mfano wa kiberiti na gesi kusisitiza umuhimu wa tahadhari katika kushughulikia mambo mbalimbali.

Dkt. Nchemba alitoa kauli hiyo jana, Jumanne, Septemba 15, 2026, wakati akizungumza na wananchi wa Bariadi Mjini, mkoani Simiyu, katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Viwanja vya CCM Saba Saba.

Katika hotuba yake, Waziri Mkuu alisema: “Sio kila kiberiti nitakichukua, vingine ni vya gesi, vitakulipukia,” akisisitiza kuwa baadhi ya masuala yanahitaji utulivu, busara na namna maalum ya kuyashughulikia

16/09/2026

Mkaguzi mkuu wa Pentagon, kwa mara ya kwanza, amethibitisha rasmi kwamba mpiganaji wa siri wa F-35 aliharibiwa na "moto wa adui" wakati wa misheni ya mapigano nchini Iran, miezi kadhaa baada ya Washington kuelezea tukio hilo k**a kutua kwa dharura tu.

Katika tathmini yake rasmi ya kwanza ya hasara na usumbufu wa uendeshaji unaotokana na vita dhidi ya Iran, mkaguzi mkuu alisema Jumanne kwamba mashambulizi ya Iran yaliharibu au kuharibu mamia ya majengo na miundo katika kambi za kijeshi za Marekani kote katika eneo hilo na kuchangia uhaba wa silaha muhimu.

Kwa kuzingatia kipindi cha kuanzia Februari 28 hadi Juni 30, tathmini hiyo pia ilibainisha ndege aina ya F-35 miongoni mwa mali za kijeshi za Marekani zilizoharibiwa na ulinzi wa anga wa Iran.

16/09/2026

Picha mpya zilizopatikana na CBS News zinaonyesha uharibifu mkubwa wa majengo, magari na vifaa katika vituo kadhaa vya kijeshi vya Marekani Mashariki ya Kati, kufuatia mashambulizi ya makombora na ndege zisizo na rubani yaliyofanywa na Iran.

Kwa mujibu wa CBS News, picha hizo zilitumwa na wanajeshi wa Marekani walioko katika maeneo ya operesheni, ambao waliomba kutotajwa majina kutokana na masharti ya kijeshi yanayodhibiti utoaji wa taarifa kwa vyombo vya habari.

Moja ya picha inaonyesha uharibifu katika Prince Sultan Air Base nchini Saudi Arabia, ambapo ndege aina ya Boeing E-3 Sentry imeonekana ikiwa imeharibiwa vibaya, huku sehemu ya mkia ikiwa imekatika na mwili wa ndege ukiwa umeungua.

Picha nyingine kutoka Camp Buehring nchini Kuwait zinaonyesha majengo na mabweni yaliyoharibiwa, pamoja na magari na miundombinu mingine iliyokumbwa na mashambulizi.

CBS News imenukuu mmoja wa wanajeshi walioko kwenye operesheni akisema uharibifu katika baadhi ya vituo ni mkubwa na kwamba kiwango chake hakijawasilishwa kikamilifu kwa umma wa Marekani.

Taarifa hiyo inafuatia miezi kadhaa ya mashambulizi na mashambulizi ya kulipiza kisasi kati ya Marekani na Iran katika Mashariki ya Kati, huku vituo vya Marekani katika baadhi ya nchi za eneo hilo vikilengwa kwa makombora na drones.

CBS News imesema picha hizo ni ushahidi mpya unaoonyesha ukubwa wa athari za mashambulizi hayo kwenye miundombinu ya kijeshi ya Marekani katika eneo hilo.

Address

Samora Avenue
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mediawireexpress posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Mediawireexpress:

Shortcuts

Share