Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete - JKCI

Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete  - JKCI JKCI is a government National Specialized & University Teaching Hospital offering Cardiovascular care

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Afya na Jamhuri ya Watu wa China waanza majadiliano ya kin...
01/09/2026

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Afya na Jamhuri ya Watu wa China waanza majadiliano ya kina yaliyolenga kukamilisha upatikanaji wa hati ya makubaliano ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Hospitali mpya ya moyo nchini.

Hatua hiyo imefikiwa baada ya wataalamu kutoka Wizara ya Afya, Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na Jamhuri ya Watu wa China kukutana na kupitia vipengele mbalimbali vya makubaliano vinavyohusu ujenzi wa hospitali hiyo pamoja na maeneo mengine ya ushirikiano katika sekta ya afya.
Akizungumza wakati wa kikao hicho Mkurugenzi wa Idara ya Tiba kutoka Wizara ya Afya Dkt. Hamad Nyembea alisema majadiliano hayo yanalenga kuhakikisha kuwa pande zote mbili zinafikia uelewa wa pamoja kuhusu vipengele vya makubaliano kabla ya hatua ya kusaini hati.

“Tumekutana na wataalamu wenzetu kutoka Jamhuri ya Watu wa China kupitia na kujadili baadhi ya vipengele vya hati ya makubaliano ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Hospitali mpya ya moyo pamoja na miradi mingine iliyopo chini ya Sekta ya Afya, tunaamini kwamba kupitia majadiliano haya tutakamilisha taratibu za makubaliano na kuanza utekelezaji”, alisema Dkt. Nyembea.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Angela Muhozya alisema JKCI itatoa ushirikiano wa kutosha kwa wataalamu kutoka Jamhuri ya Watu wa China wakati wote wa kutekeleza mradi huo.

“Tutahakikisha kabla ya yote tunawatambulisha katika mazingira yetu, taratibu na mifumo yetu pamoja na kuhakikisha kuwa wanafanya kazi kwa karibu na wataalamu wetu ili lengo tulilokusudia liweze kufanikiwa”, alisema Dkt. Angela.

Naye Mshauri wa Masuala ya Uchumi na Biashara katika Ubalozi wa China nchini Tanzania Chu Kun alisema Jamhuri ya Watu wa China inafahamu umuhimu wa ushirikiano uliopo baina ya nchi hizo mbili.
“Tumeshaanza kupitia baadhi ya vipengele vya makubaliano tukiwa na lengo moja la kuwezesha ujenzi wa hospitali hii mpya ya moyo hapa Tanzania ili kuwasaidia wagonjwa wa moyo kupata huduma hapa nchini”, alisema Chu.

Kwa mara ya kwanza watalamu wa upasuaji wa moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na mwenzao kut...
01/09/2026

Kwa mara ya kwanza watalamu wa upasuaji wa moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na mwenzao kutoka Mradi wa Little Heart wa Shirika la Muntada lililopo nchini Uingereza Dkt. Ahmet Sasmazel wamemfanyia upasuaji wa moyo mtoto aliyezaliwa na mishipa miwili mikubwa ya damu inayotoka kwenye moyo kupishana (Nikaidoh Operation).

Upasuaji huo umefanyika kwa njia ya kufungua kifua kwa mtoto mwenye umri wa miaka miwili na mwezi mmoja kwa mafanikio makubwa.

Akizungumza na mwandishi wa habari hii leo jijini Dar es Salaam Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Thabit Ramadhani alisema upasuaji huu ni wa kwanza kufanyika JKCI na Afrika Mashariki na Kati.

“Tumefanya upasuaji huu kwa umakini mkubwa, na sasa mtoto anaendelea vizuri, ameshatolewa katika chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalumu (ICU) na kupelekwa katika chumba cha ungalizi wa watoto (PICU)”, alisema Dkt. Thabit.

Kwa upande wake Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo kutoka Mradi wa Little Heart wa Shirika la Muntada lililopo nchini Uingereza Dkt. Ahmet Sasmazel alisema mafanikio ya upasuaji huo yametokana na ushirikiano wa karibu uliokuwa ukifanywa na watalaamu wa JKCI.

Naye mama wa mtoto aliyefanyiwa upasuaji huo Witness Kibuga alisema mtoto wake aligundulika kuwa na tatizo la moyo akiwa na umri wa miezi saba na kuanza kuudhuria kliniki ya matibabu ya moyo hadi sasa alipofanyiwa upasuaji huo.

31/08/2026

Jumla ya watu 1,005 wamepatiwa huduma za uchunguzi na matibabu ya magonjwa yasiyoambukiza ikiwemo magonjwa ya moyo na macho wakati wa kambi maalumu ya matibabu iliyomalizika jana mkoani Arusha

Kambi hiyo maalumu ilikuwa ikifanywa na wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete – Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (JKCI–ALMC) na kudhaminiwa na GSM Foundation kwa lengo la kuwafikia wananchi wa Kanda ya Kaskazini na kusogeza huduma hizo karibu na wananchi.

Jumla ya watu 1,005 wamepatiwa huduma za uchunguzi na matibabu ya magonjwa yasiyoambukiza ikiwemo magonjwa ya moyo na ma...
31/08/2026

Jumla ya watu 1,005 wamepatiwa huduma za uchunguzi na matibabu ya magonjwa yasiyoambukiza ikiwemo magonjwa ya moyo na macho wakati wa kambi maalumu ya matibabu iliyomalizika jana mkoani Arusha

Kambi hiyo maalumu ilikuwa ikifanywa na wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete – Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (JKCI–ALMC) na kudhaminiwa na GSM Foundation kwa lengo la kuwafikia wananchi wa Kanda ya Kaskazini na kusogeza huduma hizo karibu na wananchi.

Akizingumza wakati wa kufunga kambi hiyo Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete – Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (JKCI–ALMC) Dkt. Godwin Kivuyo alisema idadi ya wagonjwa waliopatiwa huduma imevuka lengo lililowekwa hatua inayoonesha mwitikio mkubwa wa wananchi kutumia fursa zilizopo kupata huduma za afya.

“Kambi hii imekuwa na siku tano ambazo tulikuwa tumedhamiria kuona wagonjwa elfu moja angalau wagonjwa kati ya 150 hadi 200 kwa siku, mpaka leo tumeweza kuona wagonjwa 1,005 hivyo kufikia lengo tulilojiwekea”, alisema Dkt. Kivuyo.

Dkt. Kivuyo alisema kupitia kambi hiyo wataalamu wa JKCI – ALMC wameweza kufanya vipimo zaidi ya 800 kuchunguza magonjwa ya moyo na macho.

Kwa upande wake Mratibu kutoka GSM Foundation Julius Ndyakoha alisema GSM kufadhili kambi hiyo ni sehemu ya kurudisha kwa jamii, kuunga mkono jitihada zinazofanywa na JKCI pamoja na Serikali katika kuboresha upatikanaji wa huduma za afya nchini.

Vyombo vya habari, wadau na watu binafsi waombwa kuwasiliana na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) pale wanapofuatwa ...
31/08/2026

Vyombo vya habari, wadau na watu binafsi waombwa kuwasiliana na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) pale wanapofuatwa na wagonjwa au familia zinazohitaji msaada wa matibabu ya moyo ili kupata taarifa sahihi kuhusu hali ya mgonjwa, mahitaji ya matibabu na taratibu zinazopaswa kufuatwa kabla ya kuanza kutafuta msaada kwa niaba ya wagonjwa hao

29/08/2026

Wananchi wa mkoa wa Arusha wameipongeza Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete – Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (JKCI-ALMC) kwa kushirikiana na Kampuni ya GSM Foundation kuendesha kambi maalumu ya uchunguzi na matibabu ya magonjwa yasiyoambukiza mkoani humo.
Pongezi hizo zimetolewa na wananchi waliojitokeza kufanya uchunguzi wa afya katika kambi hiyo inayofanyika katika viwanja vya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete–Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (JKCI–ALMC) iliyopo jijini Arusha.
Wananchi hao walisema kupitia kambi hiyo wameweza kupata fursa ya kufanya uchunguzi wa afya, kujua namba zao pamoja na ushauri kutoka kwa watalamu wa afya bila
Aisha Juma mkazi wa Arusha alisema mbali na wananchi kupata huduma za afya na ushauri kutoka kwa wataalamu wa JKCI-ALMC wataalamu hao pia wamekuwa wakiwasaidia wanaichi hao kupata huduma nyingine za jamii k**a vile kuwapa viburudisho, kuwasaidia kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine wale wasiojiweza na kuchukua mawasiliano yao kwaajili ya ufuatiliaji wa hali zao.
“Afya ni bora kuliko pesa, watu wakilijua hili wataona umuhimu wa kufanya uchunguzi wa afya kuliko kuhangaika na kutafuta pesa kwasababu pesa tunazozitafuta hapo baadaye zinaweza kutumika hadi kuisha kwa kutafuta huduma za afya”, alisema Aisha
Naye mkazi wa Arusha mjini John Matemu alisema amefika katika Hospitali hiyo mara baada ya kupata taarifa hivyo akaona ni muhimu kufika na kufanya uchunguzi wa aya ya macho yake kutokana na alivyokuwa akijisikia.
“Huduma ni nzuri na tunazipata kwa wakati, watu wengi wakipata taarifa ya kambi za matibabu wanahofia muda kutokana na idadi kubwa ya wanaohitaji huduma hizi, lakini hapa wameweka utaratibu mzuri ambao unarahisisha upatikanaji wa huduma kwa wakati”, alisema John

Wananchi wa mkoa wa Arusha wameipongeza Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete – Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (JK...
29/08/2026

Wananchi wa mkoa wa Arusha wameipongeza Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete – Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (JKCI-ALMC) kwa kushirikiana na Kampuni ya GSM Foundation kuendesha kambi maalumu ya uchunguzi na matibabu ya magonjwa yasiyoambukiza mkoani humo.

Pongezi hizo zimetolewa na wananchi waliojitokeza kufanya uchunguzi wa afya katika kambi hiyo inayofanyika katika viwanja vya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete–Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (JKCI–ALMC) iliyopo jijini Arusha.
Wananchi hao walisema kupitia kambi hiyo wameweza kupata fursa ya kufanya uchunguzi wa afya, kujua namba zao pamoja na ushauri kutoka kwa watalamu wa afya bila
Aisha Juma mkazi wa Arusha alisema mbali na wananchi kupata huduma za afya na ushauri kutoka kwa wataalamu wa JKCI-ALMC wataalamu hao pia wamekuwa wakiwasaidia wanaichi hao kupata huduma nyingine za jamii k**a vile kuwapa viburudisho, kuwasaidia kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine wale wasiojiweza na kuchukua mawasiliano yao kwaajili ya ufuatiliaji wa hali zao.

“Afya ni bora kuliko pesa, watu wakilijua hili wataona umuhimu wa kufanya uchunguzi wa afya kuliko kuhangaika na kutafuta pesa kwasababu pesa tunazozitafuta hapo baadaye zinaweza kutumika hadi kuisha kwa kutafuta huduma za afya”, alisema Aisha

Naye mkazi wa Arusha mjini John Matemu alisema amefika katika Hospitali hiyo mara baada ya kupata taarifa hivyo akaona ni muhimu kufika na kufanya uchunguzi wa aya ya macho yake kutokana na alivyokuwa akijisikia.

“Huduma ni nzuri na tunazipata kwa wakati, watu wengi wakipata taarifa ya kambi za matibabu wanahofia muda kutokana na idadi kubwa ya wanaohitaji huduma hizi, lakini hapa wameweka utaratibu mzuri ambao unarahisisha upatikanaji wa huduma kwa wakati”, alisema John

Bodi ya Wadhamini, Menejimenti na wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) tunakupongeza Mhe. Deogratius Joh...
29/08/2026

Bodi ya Wadhamini, Menejimenti na wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) tunakupongeza Mhe. Deogratius John Ndejembi kwa kuteuliwa, kuthibitishwa na kuapishwa kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Tunakutakia kila la kheri katika majukumu yako mapya.

Kwa mara ya kwanza Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) imefanikiwa kumfanyia upasuaji wa moyo mtoto wa siku mbili aliy...
29/08/2026

Kwa mara ya kwanza Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) imefanikiwa kumfanyia upasuaji wa moyo mtoto wa siku mbili aliyezaliwa akiwa na tatizo la kubana kwa mshipa wa damu unaopeleka damu kwenye mapafu (Severe pulmonary valve stenosis).

Upasuaji huo wa bila kufungua kifua kwa kutumia mtambo wa Cathlab (Percutaneous balloon pulmonary valvuloplasty- PBV) umefanyika katika kambi maalumu ya siku sita iliyokuwa ikifanywa na watalaamu wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao kutoka mradi wa Little Heart wa shirika la Muntada Aid lililopo nchini Uingereza.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Angela Muhozya alisema ushirikiano huo wa kimatibabu umeleta matokeo makubwa ikiwemo kufanikiwa kumfanyia upasuaji mtoto wa siku mbili.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Muntada Aid Nayaf Sheikh alisema shirika hilo limesafiri katika mataifa mbalimbali kuwasaidia watoto wanaohitaji upasuaji wa kibingwa lakini limeona upekee wa JKCI kutokana na kuwa na miundombinu wezeshi.

“Hii ni mara yetu ya 9 kuja JKCI na mara zote ambazo tumekuwa tukija hapa tumekuwa tukipewa ushirikiano wa watalamu ambao unatuwezesha kufanya upasuaji wa kibingwa kwa kiwango kikubwa hivyo watanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla hawana haja tena ya kusafiri kwenda nje ya nchi kufuata matibabu ya kibingwa”, alisema Sheikh.

28/08/2026

Watu 200 wamepatiwa huduma za uchunguzi na matibabu ya macho kupitia kambi maalumu ya uchunguzi na matibabu ya magonjwa yasiyoambukiza yakiwemo magonjwa macho inayoendeshwa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete – Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (JKCI–ALMC) kwa kushirikiana na Kampuni ya GSM Foundation.
Akizungumza wakati wa kambi hiyo Daktari Bingwa wa Macho wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete – Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (JKCI–ALMC) John Njelango alisema watu hao wamepatiwa huduma za macho ikiwemo kufanyiwa kipimo cha presha ya macho, uchunguzi wa madhara ya kisukari kwenye macho pamoja na vipimo vya miwani.

Address

Dar Es Salaam
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete - JKCI posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete - JKCI:

Share