NemcTanzania

NemcTanzania Karibu katika ukurasa rasmi wa Baraza la Taifa la Hifadhi ya Mazingira (NEMC). Pamoja tulinde na kutunza mazingira kwa maendeleo endelevu.

UCHUMI MZUNGUUKO NI NGUZO MUHIMU YA UTUNZAJI WA MAZINGIRA 🤝
12/06/2026

UCHUMI MZUNGUUKO NI NGUZO MUHIMU YA UTUNZAJI WA MAZINGIRA 🤝

TUPANDE MTI NA TUUTUNZE🤝
10/06/2026

TUPANDE MTI NA TUUTUNZE🤝

KUKIJANISHA TANZANIA NI WAJIBU WETU SOTE🤝
09/06/2026

KUKIJANISHA TANZANIA NI WAJIBU WETU SOTE🤝

NEMC YASHIRIKI KILELE CHA MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI.Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira ...
06/06/2026

NEMC YASHIRIKI KILELE CHA MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI.

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeshiriki kilele Cha Maadhimisho ya siku ya Mazingira Duniani yaliyofanyika tarehe 5 Juni 2026 katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete (JKCC) Jijini Dodoma yenye kaulimbiu isemayo Dira 2050- Tushirikiane kukijanisha Tanzania

Mgeni rasmi katika Maadhimisho hayo alikuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.Emmanuel Nchimbi ambapo pamoja na mambo mengine akizindua mikakati wa Kitaifa wa kukijanisha Tanzania.

Maadhimisho hayo pia yalitanguliwa na Maonesho ya wiki nzima yenye kutoka elimu ya Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira kwa wadau mbalimbali ambapo NEMC k**a mdau wa Mazingira ametekeleza Dira hii kwa vitendo.

NEMC YAMTAMBUA JACKLINE ELIABI KWA WASILISHO BORA LA UCHUMI MZUNGUKO KATIKA KILELE CHA MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZINGIRA ...
06/06/2026

NEMC YAMTAMBUA JACKLINE ELIABI KWA WASILISHO BORA LA UCHUMI MZUNGUKO KATIKA KILELE CHA MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limemtambua mwanafunzi wa Darasa la Sita, Jackline Eliabi wa Shule ya Msingi Manyinga, Wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro, kwa uwasilishaji wake bora wa dhana ya Uchumi Mzunguko katika kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani.

Jackline alipata pongezi na kutunukiwa zawadi baada ya kuwasilisha kwa umahiri dhana hiyo muhimu inayohamasisha matumizi endelevu ya rasilimali, upunguzaji wa taka na uhifadhi wa mazingira. Uwasilishaji wake ulionesha uelewa mkubwa wa masuala ya mazingira na mchango wa wanafunzi katika kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa kutunza mazingira kwa maendeleo endelevu.

Zawadi hiyo ilitolewa na Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Dkt. Immaculate Sware Semesi, ikiwa ni kutambua mchango wa wanafunzi katika kusukuma gurudumu la uhifadhi na usimamizi wa mazingira nchini. Dkt. Semesi alieleza kuwa wanafunzi ni wadau muhimu katika juhudi za kulinda mazingira na kwamba wao ndio mabalozi wa baadaye wa mazingira watakaosaidia kuendeleza agenda ya maendeleo endelevu kwa manufaa ya taifa na vizazi vijavyo.

Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Mhe. Edward Mpogolo, akitoa tuzo kwa Shule za Mkoa wa Dar es Salaam zinazofanya vizuri katika u...
06/06/2026

Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Mhe. Edward Mpogolo, akitoa tuzo kwa Shule za Mkoa wa Dar es Salaam zinazofanya vizuri katika uhifadhi na usimamizi wa Mazingira, katika Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani Juni 5, 2026 zilizoandaliwa ma NEMC kwa kushirikiana ma KPMG ikiwa ni jitihada za kuhamasisha wanafunzi, walimu na jamii kwa ujumla kuendeleza utamaduni wa kutunza mazingira.

NEMC YATAMBUA SHULE BORA ZA UHIFADHI WA MAZINGIRA: SIKU YA MAZINGIRA DUNIANIBaraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa M...
05/06/2026

NEMC YATAMBUA SHULE BORA ZA UHIFADHI WA MAZINGIRA: SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI

Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limetoa tuzo na vyeti kwa Shule za Ssingi zinazofanya vizuri kwenye uhifadhi wa mazingira katika Mkoa wa Dar es Salaam, wakati wa sherehe za kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yaliyofanyika Kimkoa Juni 5, 2026 katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam, yakiongozwa na kauli mbiu isemayo, “Dira 2050: Tuwajibike Kukijanisha Tanzania.”

Akizungumza katika kilele cha maadhimisho hayo, Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Mhe. Edward Mpogolo, amewataka wananchi kushiriki kikamilifu katika uhifadhi wa mazingira ili kuunga mkono maendeleo endelevu ya Taifa. “Tunahitaji kuongeza juhudi za pamoja katika kulinda mazingira yetu, kwani mafanikio ya Dira 2050 yanategemea namna tunavyohifadhi rasilimali za mazingira na kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabianchi,” amesema.

Kaimu Meneja wa Kanda ya Ilala, Bi. Zainab Kuhanwa, ametoa salamu za Baraza Kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, na kuongeza kuwa NEMC kwa kushirikiana na KPMG Advisory Limited iliandaa mashindano ya shule za msingi ili kutambua na kuthamini juhudi za uhifadhi wa mazingira, sambamba na kuhamasisha wanafunzi kuwa mabalozi wa mazingira katika jamii.

Ameeleza kuwa shule washindi zilipatikana baada ya tathmini iliyozingatia vigezo mbalimbali vya usimamizi wa mazingira ikiwemo uwepo wa Klabu za Mazingira, upandaji wa miti, usimamizi wa taka na usafi wa mazingira. Amesema utoaji wa tuzo na vyeti hivyo unalenga kuhamasisha Shule na Wadau wengine kuendelea kushiriki katika kulinda mazingira kwa maendeleo endelevu.

DKT. NCHIMBI AZURU BANDA LA NEMC MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANIMakamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzan...
05/06/2026

DKT. NCHIMBI AZURU BANDA LA NEMC MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. Emmanuel Nchimbi ametembelea Banda la NEMC Leo ikiwa ni siku ya kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yanayoadhimishwa kila tarehe 5, Mei ya Kila mwaka ambapo alipata fursa ya kujionea shughuli mbalimbali zinazotekelezwa na Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) katika kuhifadhi na kusimamia mazingira nchini.

Maadhimisho ya mwaka huu yamefanyika chini ya kaulimbiu isemayo *“Dira 2050: Tuwajibike Kukijanisha Tanzania,”* ikihamasisha ushiriki wa wadau wote katika kutunza mazingira, kupambana na uharibifu wa mazingira na kuendeleza matumizi endelevu ya rasilimali asilia kwa maendeleo ya Taifa na ustawi wa vizazi vijavyo.

05/06/2026
MWENYEKITI WA BODI YA NEMC AKIMBIA KILOMITA 5Mwenyekiti wa Bodi ya Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira ...
05/06/2026

MWENYEKITI WA BODI YA NEMC AKIMBIA KILOMITA 5

Mwenyekiti wa Bodi ya Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Mhandisi Mwanasha Tumbo, ameshiriki mbio za kilomita 5 zilizofanyika katika maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani.

Mbio hizo zililenga kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa uhifadhi wa mazingira na kuendeleza afya kupitia shughuli za michezo.

Tukio hilo liliwakutanisha viongozi wa Serikali, wadau wa mazingira na wananchi mbalimbali, likibeba ujumbe wa pamoja wa kulinda mazingira kwa maendeleo endelevu na ustawi wa vizazi vya sasa na vijavyo.

Address

Regent Street
Dar Es Salaam
00000

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 16:00
Wednesday 08:00 - 16:00
Thursday 09:00 - 16:00
Friday 08:00 - 16:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when NemcTanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share