06/05/2026
Taarifa ya Kikao – 5 Aprili 2026
Tarehe 5 Aprili 2026, Jumuiya ya Mbomipa ilikutana na kampuni ya Carbon Tanzania kwa lengo la kujadili masuala yanayohusu mradi wa uvunaji wa hewa ukaa ndani ya hifadhi.
Kikao kilifanyika katika hali nzuri na yenye tija, kikionyesha mwelekeo chanya wa ushirikiano. Lengo kuu la majadiliano lilikuwa kuhakikisha mradi huu unachangia maendeleo ya jumuiya pamoja na kuboresha ustawi wa wananchi wake kwa ujumla.
Kikao hicho kilihudhuriwa na wadau mbalimbali muhimu wakiwemo Shirika la STEP, Honeyguide, Muungano wa Jumuiya za Hifadhi za Jamii (CWMAC), pamoja na Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri.
Kwa pamoja, wadau walionesha dhamira ya kuendelea kushirikiana ili kufanikisha malengo ya mradi kwa manufaa ya jamii na uhifadhi endelevu wa mazingira.