08/09/2026
KIPYENGA CHAPULIZWA ARUSHA, KUELEKEA SIKU YA UNYWAJI MAZIWA SHULENI
Maandalizi ya Maadhimisho ya Siku ya Unywaji Maziwa Shuleni 2026 yameanza rasmi mkoani Arusha baada ya Bodi ya Maziwa Tanzania (TDB) na wadau mbalimbali wa Tasnia ya Maziwa kukutana kwa ajili ya kujadili na kuweka mikakati ya pamoja kuelekea maadhimisho hayo yanayotarajiwa kufanyika Septemba 30, 2026.
Akifungua kikao hicho kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha Bi. Winfrida Joseph, ambaye ni Afisa Mifugo wa Mkoa, alisisitiza umuhimu wa maandalizi ya pamoja na ushirikiano wa wadau mbalimbali katika kuhakikisha maadhimisho hayo yanafikia malengo yaliyokusudiwa.
Alieleza kuwa tukio hilo ni fursa muhimu ya kuhamasisha jamii, hususan wazazi, walimu na wanafunzi, kuhusu umuhimu wa unywaji wa maziwa katika lishe, afya na ukuaji wa watoto.
Akizungumza kwa niaba ya Msajili wa Bodi ya Maziwa Tanzania, Kaimu Meneja Ufundi Maziwa, Bi. Deorinidei Mng’ong’o, alieleza kuwa TDB imejipanga kushirikiana na wadau katika kuimarisha uhamasishaji wa unywaji maziwa shuleni, huku akisisitiza umuhimu wa kuhakikisha maadhimisho hayo yanakuwa chachu ya kujenga utamaduni endelevu wa unywaji wa maziwa miongoni mwa wanafunzi.
Katika kikao hicho, Meneja Masoko wa TDB, Bw. Joseph Semu, aliwasilisha Dhana ya Maadhimisho ya Siku ya Unywaji Maziwa Shuleni 2026, huku akielezea shughuli na mikakati mbalimbali itakayotekelezwa kabla, wakati na baada ya maadhimisho hayo ili kuongeza uelewa na ushiriki wa wanafunzi, wazazi, walimu na wadau wengine katika kuendeleza unywaji wa maziwa shuleni.
Aidha, washiriki wa kikao hicho walijadili kwa pamoja maeneo muhimu ya maandalizi, ikiwemo uhamasishaji kupitia vyombo vya habari, mitandao ya kijamii, shule na majukwaa ya kijamii, pamoja na namna ya kushirikisha wadau mbalimbali ili kuongeza mwitikio na mwonekano wa maadhimisho hayo.
Siku ya Unywaji Maziwa Shuleni 2026 inatarajiwa kufanyika Septemba 30, 2026 mkoani Arusha, ikiwa ni sehemu ya juhudi za Bodi ya Maziwa Tanzania (TDB) na wadau wake katika kuhamasisha matumizi ya maziwa k**a sehemu ya lishe bora, kuimarisha afya na ukuaji wa watoto, pamoja na kuchochea utamaduni wa unywaji maziwa nchini huku ikienda sambamba na kaul