EGA_tanzania

EGA_tanzania e-GA inakusudia kutekeleza afua mbalimbali ili kusaidia taasisi za umma kutoa huduma mtandao kwa ufanisi. ISO 9001: 2015
CERTIFIED

Salamu za Pole
07/09/2026

Salamu za Pole

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA), Mha. Benedict Ndomba, amewataka wanafunzi wanaofanya mafunzo kwa ...
04/09/2026

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA), Mha. Benedict Ndomba, amewataka wanafunzi wanaofanya mafunzo kwa vitendo katika Kituo cha Utafiti, Ubunifu na Uendelezaji wa Jitihada za Serikali Mtandao (e-GovRIDC), kutumia ipasavyo fursa hiyo kwa kujenga maarifa, ujuzi na uwezo wa kukabiliana na mahitaji ya soko la ajira.

Mha. Ndomba ameyasema hayo jijini Dodoma wakati akizungumza na wanafunzi hao waliopata fursa ya kufanya mafunzo kwa vitendo katika kituo hicho kwa kipindi cha wiki 10.

Amesema mafunzo kwa vitendo ni sehemu muhimu katika kuwaandaa wanafunzi kwa mazingira halisi ya kazi, kwa kuwa yanawawezesha kuunganisha maarifa wanayoyapata darasani na ujuzi wa vitendo, hususan katika sekta ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA).

Kwa upande wake, Meneja wa Utawala na Rasilimali Watu wa e-GA, Jafari Maganga, amewataka wanafunzi hao kuzingatia kanuni, taratibu na maadili ya Utumishi wa Umma wakati wote wa mafunzo yao.

Naye Meneja wa e-GovRIDC, Dkt. Jaha Mvula, amesema ushiriki wa wanafunzi katika miradi hiyo unalenga kuwapatia uzoefu wa vitendo, kuwawezesha kutumia maarifa waliyoyapata katika masomo yao na kuwajengea uwezo wa kushiriki katika ubunifu na utatuzi wa changamoto za kiteknolojia.

Kwa niaba ya wanafunzi wenzake, Leticia Omari kutoka Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya (MUST), ameishukuru e-GA kwa kuwapatia fursa hiyo, akisema mafunzo hayo yatawasaidia kuongeza maarifa, ujuzi na uzoefu wa mazingira halisi ya kazi.

Kituo hicho kimepokea jumla ya wanafunzi 62 kutoka vyuo vikuu 10 kwa ajili ya mafunzo kwa vitendo ya kipindi cha wiki 10. Wanafunzi hao wamegawanywa katika makundi mbalimbali yanayoshiriki katika utekelezaji wa jumla ya miradi 14 inayohusisha maeneo tofauti ya teknolojia ya TEHAMA.

Mkurugenzi wa Usimamizi wa Huduma za TEHAMA Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) Bw. Ricco Boma, leo Septemba 01, 2026 ame...
01/09/2026

Mkurugenzi wa Usimamizi wa Huduma za TEHAMA Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) Bw. Ricco Boma, leo Septemba 01, 2026 ameshiriki kwenye mjadala unaohusu “Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali katika Kuongeza Ufanisi wa Huduma za Umma” (Leveraging Digital for Public Service Efficiency) katika Kongamano la mwaka la Ubunifu lilioandaliwa kwa ushirikiano wa Tume ya Taifa ya Mipango, Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) na Umoja wa Ulaya (European Union).

Kongamano hilo linaongozwa na kaulimbiu “Kutoka kwenye Dhamira hadi Mageuzi: Ubunifu katika Njia ya Tanzania kuelekea Ustawi Jumuishi” (From Aspirations to Transformation: Innovating Tanzania’s Path to Inclusive Prosperity), linafanyika kwa siku tano kuanzia Agosti 31 hadi Septemba 4, 2026 katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Mwl Julius Nyerere (JNICC).

29/08/2026

24/08/2026


24/08/2026


Address

Mtumba-Mtaa Wa Mtandao
Dodoma

Opening Hours

Monday 07:30 - 15:30
Tuesday 07:30 - 15:30
Wednesday 07:30 - 15:30
Thursday 07:30 - 15:30
Friday 07:30 - 15:30

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when EGA_tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to EGA_tanzania:

Shortcuts

Share