Ucsaf-Tanzania

Ucsaf-Tanzania UCSAF ilianzishwa na Serikali kwa lengo la kufanikisha huduma ya mawasiliano katika maeneo yasio na mvuto kwa watoa huduma ya mawasiliano nchini.

📌UCSAF YAUNGANISHA VIJIJI 51 MWANZA, WANANCHI 322,820 WAMENUAFAIKASerikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF)...
17/09/2026

📌UCSAF YAUNGANISHA VIJIJI 51 MWANZA, WANANCHI 322,820 WAMENUAFAIKA

Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) imefikisha huduma za mawasiliano katika vijiji 51 vya Mkoa wa Mwanza, na kuwawezesha wananchi 322,820 kupata huduma za mawasiliano katika maeneo yao.

Vijiji hivyo vimefikishiwa huduma kupitia Mradi wa Kimkakati wa Ujenzi wa Minara 758 ya Mawasiliano, ambao umekamilika na tayari umezinduliwa rasmi. Mradi huo umewezesha kufikisha huduma za mawasiliano katika vijiji 1,400 nchini, hususan maeneo ya vijijini yaliyokuwa hayajafikiwa na huduma hizo.

Kupatikana kwa huduma za mawasiliano kumewawezesha wananchi kurahisisha mawasiliano ya kila siku, kupata taarifa na kutumia huduma mbalimbali zinazotegemea mawasiliano, ikiwemo huduma za kifedha, biashara na intaneti, hivyo kuchangia shughuli za kijamii na kiuchumi katika maeneo yao.

📻 KIPINDI CHA REDIO – NURU FM IRINGAMkuu wa Kanda ya Nyanda za Juu Kusini kutoka Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF), ...
17/09/2026

📻 KIPINDI CHA REDIO – NURU FM IRINGA

Mkuu wa Kanda ya Nyanda za Juu Kusini kutoka Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF), Mhandisi Richard Sotery atashiriki katika kipindi cha Redio Nuru FM Iringa, akieleza juhudi za Serikali katika kuimarisha na kufikisha huduma za mawasiliano vijijini.

🎙️ Usikose kufuatilia kipindi hiki kupitia Nuru FM Iringa!

17/09/2026

📌KITOHAVI SASA YAUNGANISHWA: WANANCHI WAFURAHIA MAWASILIANO KOKOTE.

Wananchi wa Kijiji cha Kitohavi, Mkoa wa Lindi, wameeleza furaha yao baada ya huduma za mawasiliano kufikishwa katika eneo hilo, wakisema sasa wanaweza kuwasiliana kwa urahisi wakiwa katika maeneo mbalimbali ya kijiji.

Awali, wananchi hao walikabiliwa na changamoto ya ukosefu wa mawasiliano, hali iliyowalazimu kutafuta maeneo maalum yenye mawasiliano ili kuweza kupiga au kupokea simu.

Wamesema wakati mwingine walilazimika kuweka simu zao katika maeneo maalum na kusubiri au kuzungumza wakiwa katika eneo hilo ili kupata mawimbi, jambo lililokuwa likiwapa usumbufu na kupoteza muda.

Wananchi hao wameeleza kuwa upatikanaji wa mawasiliano umeleta mabadiliko katika maisha yao ya kila siku, ikiwemo kurahisisha mawasiliano ya kifamilia, kijamii na shughuli mbalimbali za kiuchumi.

16/09/2026

VIJIJI 151 MOROGORO VYAFIKIWA NA HUDUMA ZA MAWASILIANO

Wananchi katika vijiji 151 vya Mkoa wa Morogoro wameanza kunufaika na huduma za mawasiliano baada ya maeneo yao kufikishiwa miundombinu kupitia Mradi wa Ujenzi wa minara 758, uliotekelezwa na Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF).

Kupitia mradi huo, jumla ya wananchi 983,815 katika vijiji hivyo wamewezeshwa kupata huduma za mawasiliano, hatua inayochangia kuunganisha jamii ambazo awali zilikuwa na changamoto ya upatikanaji wa huduma hizo.

Upatikanaji wa mawasiliano umefungua fursa kwa wananchi kutumia huduma mbalimbali zinazotegemea mtandao, ikiwemo mawasiliano ya simu, huduma za kifedha kwa njia ya simu, kupata taarifa, kufanya biashara na kuwasiliana wakati wa dharura.

Aidha, uwepo wa huduma za mawasiliano unasaidia kuchochea shughuli za kiuchumi na kijamii katika maeneo ya vijijini kwa kuwawezesha wananchi kuwasiliana kwa urahisi zaidi na masoko, wateja, taasisi za Serikali na huduma nyingine muhimu.

16/09/2026

📍UCSAF YAING’ARISHA MJIMBINI KIBIASHARA KUPITIA MAWASILIANO

Shehiya ya Mjimbini, Wilaya ya Mkoani, Mkoa wa Kaskazini Pemba, imeendelea kunufaika na fursa za kiuchumi baada ya Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) kufikisha huduma za mawasiliano katika eneo hilo.

Wakazi wa Mjimbini wamesema uwepo wa mawasiliano umerahisisha shughuli za biashara, ikiwemo usafirishaji na uuzaji wa mazao ya kilimo. Aidha, wajasiriamali wadogo, akiwemo wanaojishughulisha na ushonaji, wamesema mitandao ya mawasiliano imewawezesha kupata mawazo na mitindo mbalimbali ya ushonaji kupitia mitandao ya kijamii.

Wakazi hao wameeleza kuwa mawasiliano yamekuwa chachu ya kuimarisha shughuli zao za kiuchumi, kwani sasa wanaweza kuwasiliana kwa urahisi na wateja, wafanyabiashara na masoko yaliyo mbali na eneo lao.

📌Ofisi zetu
16/09/2026

📌Ofisi zetu

15/09/2026

WAKAZI WA MTAWANGO, LINDI WAFURAHIA MANUFAA YA MAWASILIANO KATIKA AFYA, BIASHARA NA KILIMO

Wakazi wa Kijiji cha Mtawango, Wilaya ya Liwale, Mkoa wa Lindi, wanaendelea kufurahia manufaa ya huduma za mawasiliano baada ya Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) kuwezesha upatikanaji wa mawasiliano katika eneo hilo.

Wamesema upatikanaji wa mawasiliano umeleta mabadiliko katika shughuli zao za kila siku, hususan katika huduma za afya, biashara na kilimo, ambapo sasa wanaweza kuwasiliana kwa urahisi na kupata taarifa muhimu zinazohusiana na shughuli zao.

Maboresho hayo ni sehemu ya juhudi za Serikali kupitia UCSAF za kuhakikisha huduma za mawasiliano zinawafikia wananchi katika maeneo ambayo awali hayakuwa na huduma za uhakika, ili kuwawezesha kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi na kijamii.

📍UCSAF YATOA ELIMU KWA UMMA KUHUSU MIRADI YA MAWASILIANO PEMBA.Timu ya Elimu kwa Umma kutoka Mfuko wa Mawasiliano kwa Wo...
14/09/2026

📍UCSAF YATOA ELIMU KWA UMMA KUHUSU MIRADI YA MAWASILIANO PEMBA.

Timu ya Elimu kwa Umma kutoka Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) imefika katika shehia mbalimbali za Mkoa wa Kusini Pemba na Kaskazini Pemba kwa lengo la kutoa elimu kwa wananchi kuhusu miradi ya mawasiliano inayotekelezwa na Serikali kupitia UCSAF katika maeneo yao.

Elimu hiyo inalenga kuwawezesha wananchi kufahamu miradi inayotekelezwa, manufaa yake pamoja na namna miundombinu ya mawasiliano inavyosaidia kuboresha maisha ya wananchi na kuchochea shughuli za kiuchumi na kijamii katika maeneo ambayo hapo awali yalikuwa na changamoto ya upatikanaji wa huduma za mawasiliano.

Hivi sasa, Serikali inatekeleza mradi wa ujenzi wa minara 287 ya mawasiliano ya simu nchini, ambapo minara 21 inajengwa Zanzibar, katika maeneo mbalimbali ya Unguja na Pemba.

Kupitia mradi huo, Serikali inalenga kuongeza upatikanaji na ubora wa huduma za mawasiliano kwa wananchi, hususan katika maeneo ambayo hayajafikiwa kikamilifu na huduma hizo kutokana na changamoto za kijiografia au kutokuwa na mvuto wa kutosha wa uwekezaji kibiashara.

14/09/2026

📌MINARA 9 YAUNGANISHA WANANCHI 154,117 MKOANI MBEYA.

Wananchi 154,117 wameanza kupata huduma za mawasiliano katika Mkoa wa Mbeya baada ya kukamilika kwa ujenzi wa minara 9 katika vijiji 14 vilivyopo katika wilaya mbalimbali za mkoa huo.

Miundombinu hiyo imeongeza upatikanaji wa huduma za mawasiliano kwa wananchi wa maeneo hayo, ikiwemo kurahisisha mawasiliano, matumizi ya huduma za kifedha kwa njia ya simu, upatikanaji wa taarifa na kuchochea shughuli za kiuchumi na kijamii.

Hatua hiyo ni sehemu ya jitihada za Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) za kuhakikisha huduma za mawasiliano zinawafikia wananchi katika maeneo ya vijijini na maeneo ambayo hayajafikiwa kikamilifu na huduma hizo.

📍Malengo ya kuanzishwa kwa UCSAF
14/09/2026

📍Malengo ya kuanzishwa kwa UCSAF

Address

Jengo La UCSAF, S. L. P 1957, 10 Barabara Ya UCSAF, Makulu
Dodoma
41107

Opening Hours

Monday 08:00 - 16:00
Tuesday 08:00 - 16:00
Wednesday 08:00 - 16:00
Thursday 08:00 - 16:00
Friday 08:00 - 16:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Ucsaf-Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Organization

Send a message to Ucsaf-Tanzania:

Shortcuts

Share