Ofisi ya Mbunge Jimbo la Bunda Mjini

Ofisi ya Mbunge Jimbo la Bunda Mjini Ukurasa rasmi ya Ofisi ya Mbunge Jimbo la Bunda mjini- Kituo cha cha taarifa ,huduma na shughuli za maendeleo kwa wananchi.

SALAMU ZA RAMBIRAMBIMbunge wa Jimbo la Bunda Mjini, Mhe. Ester Amos Bulaya, amepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za k...
16/07/2026

SALAMU ZA RAMBIRAMBI

Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini, Mhe. Ester Amos Bulaya, amepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha Ndugu Benjamin Mataluma, aliyekuwa Katibu wa Vijana wa Kata ya Balili.

Mhe. Bulaya, anatoa pole za dhati kwa familia ya marehemu, ndugu, jamaa, marafiki, viongozi wa CCM Kata ya Balili, pamoja na vijana wote walioguswa na msiba huu mzito.

Ametambua mchango wa marehemu Benjamin Mataluma katika kuwatumikia vijana na kushiriki shughuli mbalimbali za maendeleo na ujenzi wa chama katika Kata ya Balili.

Katika kipindi hiki kigumu, Mhe. Bulaya anawaombea familia na wote walioguswa na msiba huu Mwenyezi Mungu awape nguvu, faraja na uvumilivu wa kuhimili majonzi haya makubwa.

"Bwana ametoa, Bwana ametwaa, jina la Bwana lihimidiwe."

Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi. Amina.

Imetolewa na
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Bunda Mjini

25/06/2026
KATIBU WA MBUNGE WA JIMBO LA BUNDA MJINI AKUTANA NA VIONGOZI WA UMOJA WA WAJASIRIAMALI WILAYA YA BUNDAKatibu wa Mbunge w...
19/06/2026

KATIBU WA MBUNGE WA JIMBO LA BUNDA MJINI AKUTANA NA VIONGOZI WA UMOJA WA WAJASIRIAMALI WILAYA YA BUNDA

Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini amekutana na viongozi wa Umoja wa Wajasiriamali Wilaya ya Bunda kwa lengo la kusikiliza changamoto mbalimbali zinazowakabili wajasiriamali ndani ya Jimbo la Bunda Mjini.

Kikao hicho kimefanyika kufuatia maelekezo ya Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini Mhe. Ester Bulaya, ikiwa ni sehemu ya kuendelea kusogeza karibu uongozi kwa wananchi na kutafuta suluhisho la changamoto zinazogusa shughuli za kiuchumi kwa wananchi.

Viongozi wa wajasiriamali walipata nafasi ya kueleza changamoto mbalimbali pamoja na kutoa mapendekezo ya namna ya kuboresha mazingira ya biashara na uwezeshaji wa wajasiriamali ndani ya jimbo.

Ofisi ya Mbunge imeeleza kuendelea kushirikiana na makundi mbalimbali ya kijamii na kiuchumi ili kuhakikisha wananchi wa Bunda Mjini wanapata fursa bora za maendeleo na kukuza uchumi wao.

Imetolewa na:
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Bunda Mjini

MBUNGE WA JIMBO LA BUNDA MJINI MHE. ESTER AMOS BULAYA AENDELEA KUGUSA JAMII, AJENGA CHOO SOKO LA MANYAMANYAMAMbunge wa J...
19/06/2026

MBUNGE WA JIMBO LA BUNDA MJINI MHE. ESTER AMOS BULAYA AENDELEA KUGUSA JAMII, AJENGA CHOO SOKO LA MANYAMANYAMA

Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini Mhe. Ester Bulaya ameendelea kuonyesha dhamira yake ya kuboresha huduma za kijamii kwa wananchi kupitia utekelezaji wa miradi yenye manufaa ya moja kwa moja kwa jamii.

Safari hii, Mbunge huyo amejenga choo katika Soko la Manyamanyama ikiwa ni hatua ya kuboresha mazingira ya wafanyabiashara na wananchi wanaotumia soko hilo kila siku.

Ujenzi wa huduma hiyo unatarajiwa kusaidia kuongeza usafi wa mazingira, kulinda afya za watumiaji wa soko pamoja na kuboresha mazingira ya biashara katika eneo hilo.

Wananchi wa eneo hilo wameeleza kuwa hatua hiyo ni sehemu ya juhudi zinazoendelea za kuimarisha ustawi wa jamii na kuboresha huduma za msingi ndani ya Jimbo la Bunda Mjini.

Imetolewa na:
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Bunda Mjini

19/06/2026

BUNGENI -DODOMA

BUNGE LA KUMI NA TATU(13)
Mkutano wa Tatu - Kikao cha Hamsini na Tatu

MBUNGE WA JIMBO LA BUNDA MJINI MHE. ESTER AMOS BULAYA AULIZA SWALI BUNGENI KUHUSU UJENZI WA KITUO CHA AFYA KABASA

Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini, Mhe.Ester Amos Bulaya ameuliza swali bungeni akitaka kufahamu ni lini Serikali itajenga Kituo cha Afya katika Kata ya Kabasa ili wananchi wa eneo hilo waondokane na adha ya kutembea umbali mrefu kufuata huduma za afya.

Mhe. Bulaya amesisitiza kuwa upatikanaji wa huduma za afya karibu na wananchi ni jambo muhimu kwa kupunguza muda na gharama za kupata matibabu pamoja na kuboresha ustawi wa jamii.

Imetolewa na
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Bunda Mjini

18/06/2026

MBUNGE WA JIMBO LA BUNDA MJINI MHE. ESTER AMOS BULAYA ATOA JEZI NA MPIRA KWA TIMU YA VIJANA BITARAGURU

Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini Mhe. Ester Amos Bulaya ametoa jezi pamoja na mpira kwa timu ya vijana ya Bitaraguru iliyopo Mtaa wa Bitaraguru, Kata ya Kabasa Jimbo la Bunda Mjini.

Msaada huo ni sehemu ya jitihada za kuendelea kuhamasisha ushiriki wa vijana katika michezo, kukuza vipaji pamoja na kuimarisha mshik**ano na maendeleo ya jamii kupitia shughuli za michezo.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Katibu wa Mbunge, kwa niaba ya Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini aliwataka vijana kuendelea kutumia michezo k**a nyenzo ya kujenga afya, nidhamu na kutengeneza fursa mbalimbali za maendeleo.

Vijana wa Bitaraguru walimshukuru Mhe. Bulaya kwa mchango huo na kueleza kuwa vifaa hivyo vitasaidia kuongeza morali na kuimarisha ushiriki wao katika mashindano na shughuli za michezo ndani ya eneo lao.

Imetolewa na:
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Bunda Mjini

16/06/2026

BUNGENI - DODOMA
15.06.2026

BUNGE LA KUMI NA TATU (13)
Mkutano wa Tatu - Kikao cha Arobaini na Tisa

Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini, Mhe. Ester Amos Bulaya, ameuliza swali Bungeni akiitaka Serikali kutoa maelezo kuhusu hatua zinazochukuliwa kutatua changamoto ya ukosefu wa huduma ya maji ambayo imeendelea kulikabili Jimbo la Bunda Mjini kwa takribani Mwezi Mmoja.

Katika swali hilo, Mhe. Bulaya ameonesha wasiwasi wake kuhusu athari zinazowakumba wananchi kutokana na upatikanaji hafifu wa maji, zikiwemo shughuli za kijamii na kiuchumi kuathirika.

Aidha, ameomba Serikali kueleza sababu za changamoto hiyo pamoja na mpango wa muda mfupi na muda mrefu wa kuhakikisha wananchi wa Bunda Mjini wanapata huduma ya maji ya uhakika na endelevu.

Imetolewa na:
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Bunda Mjini

MBUNGE WA JIMBO LA BUNDA MJINI MHE. ESTER AMOS BULAYA AKAMILISHA UJENZI WA OFISI YA WALIMU NA UKARABATI WA DARASA SHULE ...
16/06/2026

MBUNGE WA JIMBO LA BUNDA MJINI MHE. ESTER AMOS BULAYA AKAMILISHA UJENZI WA OFISI YA WALIMU NA UKARABATI WA DARASA SHULE YA MSINGI KILIMANI, KATA YA NYASURA.

Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini Mhe. Ester Amos Bulaya amekamilisha ujenzi wa ofisi moja ya walimu pamoja na ukarabati wa darasa moja katika Shule ya Msingi Kilimani iliyopo Kata ya Nyasura, Halmashauri ya Mji wa Bunda.

Hatua hiyo ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za wananchi na Serikali katika kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia, kwa lengo la kuongeza ufanisi wa utoaji wa elimu pamoja na kuweka mazingira bora kwa walimu na wanafunzi.

Kukamilika kwa ofisi hiyo ya walimu kunatarajiwa kusaidia shughuli za kiutawala shuleni, huku ukarabati wa darasa ukichangia kuboresha mazingira ya ujifunzaji kwa wanafunzi wa Shule ya Msingi Kilimani.

Wananchi wa Kata ya Nyasura wameendelea kutoa pongezi kwa jitihada hizo ambazo zinaonyesha dhamira ya kuendelea kuwekeza katika sekta ya elimu ndani ya Jimbo la Bunda Mjini.

Imetolewa na:
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Bunda Mjini

16/06/2026

BUNGENI - DODOMA
16.06.2026

BUNGE LA KUMI NA TATU (13)
Mkutano wa Tatu - Kikao cha Hamsini

Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini Mhe.Ester Bulaya aliuza swali bungeni akitaka kufahamu mpango wa Serikali wa kukarabati Kituo cha Afya cha Manyamanyama kilichopo Bunda Mjini kutokana na uchakavu wa majengo na umuhimu wake katika kutoa huduma kwa wananchi wa maeneo ya jirani.

Akijibu swali hilo bungeni, Naibu Waziri wa TAMISEMI, Dkt. Jafar R. Seif alisema kuwa Serikali ilitenga fedha za ukarabati wa vituo vya Afya 364 na kituo cha Afya Manyamanyama kimejumuishwa katika mpango huo wa ukarabati.

Serikali imeeleza kuwa ukarabati wa Kituo cha Afya Manyamanyama upo ndani ya mpango wa utekelezaji wa fedha zilizotengwa kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya afya.

Imetolewa na
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Bunda Mjini

KATIBU WA MBUNGE WA JIMBO LA BUNDA MJINI AFUATILIA ZOEZI LA UKARABATI WA MIUNDOMBINU YA MAJIKatibu wa Mbunge wa Jimbo la...
16/06/2026

KATIBU WA MBUNGE WA JIMBO LA BUNDA MJINI AFUATILIA ZOEZI LA UKARABATI WA MIUNDOMBINU YA MAJI

Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini ndugu Hussein, M. Ruge amefanya ziara ya kufuatilia zoezi la ukarabati wa miundombinu ya maji inayosababisha changamoto kubwa ya upatikanaji wa huduma ya maji kwa wananchi wa Jimbo la Bunda Mjini.

Ziara hiyo imefanyika kwa maelekezo ya Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini, Mhe. Ester Bulaya, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kuhakikisha changamoto ya ukosefu wa maji inapatiwa ufumbuzi wa haraka na wananchi wanaendelea kupata huduma muhimu kwa wakati.

Katika ufuatiliaji huo, Katibu wa Mbunge amesisitiza umuhimu wa kuongeza kasi ya utekelezaji wa kazi za ukarabati ili kuhakikisha huduma ya maji inarejea ndani ya muda mfupi na kupunguza adha inayowakabili wananchi.

Ofisi ya Mbunge imeeleza kuwa itaendelea kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa kazi hiyo hadi pale huduma ya maji itakaporejea katika hali ya kawaida kwa manufaa ya wakazi wa Bunda Mjini.

Imetolewa na
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Bunda Mjini

Address

250
Bunda
818196

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Ofisi ya Mbunge Jimbo la Bunda Mjini posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share