02/06/2026
NJIANI KUELEKEA MOROCCO
Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini, Mhe. Ester Amos Bulaya, akiwa pamoja na Mhe.Haji Manara ndani ya ndege kuelekea nchini Morocco kwa ajili ya kutoa hamasa kwa timu ya vijana ya Tanzania chini ya umri wa miaka 17, Serengeti Boys, ambayo itashuka dimbani kesho kucheza mchezo wa fainali.
Mhe. Bulaya ni miongoni mwa wabunge waliochaguliwa kuiunga mkono na kuitia moyo timu ya Serengeti Boys katika fainali itakayozikutanisha Tanzania na Senegal, ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha vijana wetu kufanya vizuri na kuendelea kuipeperusha vyema bendera ya taifa katika mashindano hayo.
Ofisi ya Mbunge wa jimbo la Bunda Mjini inawatakia kila la heri Serengeti Boys katika mchezo huo muhimu wa fainali.
Imetolewa na:
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Bunda Mjini