Chama Cha Mapinduzi Ccm Tawi La Napoli-Italy

Chama Cha Mapinduzi Ccm Tawi La Napoli-Italy The Chama Cha Mapinduzi CCM


( Revolution Party) is the dominant ruling party in Tanzania CCM CHAMA MAKINI KINACHOFANYA MAAMUZI KWA VIKAO RASMI

▪️DKT.MIGIRO AIMARISHA USHIRIKIANO KIMATAIFA NA MABALOZI WA CUBA, VIETNAM, NA UNKatibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)...
16/05/2026

▪️DKT.MIGIRO AIMARISHA USHIRIKIANO KIMATAIFA NA MABALOZI WA CUBA, VIETNAM, NA UN

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi, Dkt. Asha-Rose Migiro, kwa nyakati tofauti amekutana na kufanya mazungumzo na mabalozi wawili wanaoziwakilisha nchi zao katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mazungumzo hayo yamefanyika katika ofisi ndogo ya makao makuu CCM, Lumumba, jijini Dar es salaam.
Mabalozi hao ni Mheshimiwa Yordenis Despaigne Vera, Balozi wa Jamhuri ya Cuba na Mheshimiwa Vu Thanh Huyen, Balozi wa Jamhuri ya Kisoshalisti ya Viet Nam, wote wenye makaazi yao nchini Tanzania.

Mazungumzo hayo yalijikita katika kuendeleza na kuimarisha ushirikiano wa kihistoria kati ya CCM na vyama rafiki vya CPC–Cuba na CPV–Viet Nam, hususan katika maeneo ya uongozi, mshik**ano wa vyama vya siasa na maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwa manufaa ya wananchi wa nchi hizi mbili.

Katika hatua nyingine, Katibu Mkuu wa CCM, Dkt Migiro, alifanya mazungumzo na Mheshimiwa Susan Ngongi Namondo, Mwakilishi Mkaazi wa Umoja wa Mataifa nchini Tanzania, ambapo walijadiliana vipaumbele vya maendeleo ya jamii katika utekelezaji wa baadhi ya maeneo yaliyomo katika Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2025–2030 ambayo yanawiana na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, na Malengo ya Maendeleo ya Kimataifa (SDGs).

TAARIFA KWA UMMA
07/05/2026

TAARIFA KWA UMMA

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan afunga...
26/04/2026

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan afunga Kongamano la Muungano lililoandaliwa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Tunguu, Zanzibar

SALAMU ZA RAMBIRAMBI Chama Cha Mapinduzi kimepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Itilim...
20/03/2026

SALAMU ZA RAMBIRAMBI

Chama Cha Mapinduzi kimepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Itilima, mkoani Simiyu Ndg. Mhuli Ngeleja kilichotokea tarehe 18/03/2026 .

Katika kipindi chote cha uhai wake, marehemu alikuwa kiongozi shupavu, mwadilifu na aliyejitolea kwa dhati kukitumikia Chama.
Alitoa mchango mkubwa katika kuimarisha uhai wa Chama, kudumisha umoja na kusukuma mbele gurudumu la maendeleo ya kijamii na kiuchumi katika eneo lake.

Wana-Itilima na wana-CCM Wote tutamkumbuka sana kwa uchapakazi na uzalendo wake.
Chama Cha Mapinduzi kinatoa pole za dhati kwa familia ya marehemu, ndugu, jamaa na marafiki, pamoja na wanachama wote wa CCM Wilaya ya Itilima na Mkoa wa Simiyu kwa msiba huu mkubwa.
Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi. Amina.

21/02/2026

Celebrating our 10th year on Facebook. Thank you for your continuing support. We could never have made it without you. 🙏🤗🎉

Chama Cha Mapinduzi Ccm Mamasamiamitanotena Ccm Scandinavia Ccm Algeria

21/02/2026

“Rais Dkt. Samia Amewafikia Watu Wenye Ulemavu.”

Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Ndg. Rabia Abdalla Hamid ameyasema hayo alipowatembelea Watu Wenye Ulemavu, kwenye ofisi yao Buguruni, wilaya ya Ilala, jijini Dar es Salaam, leo tarehe 21 Februari 2026.

na Utu, Tunasonga Mbele #
KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI

Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCMTaifa (NEC), Idara ya Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa (SUKI), Ndg. Rabia Abdalla...
28/01/2026

Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM

Taifa (NEC), Idara ya Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa (SUKI), Ndg. Rabia Abdalla Hamid Leo tarehe 28 Januarı 2026, amekutana na Bw. Jack Fenwick, Katibu wa Pili -

Masuala ya Siasa kutoka Ubalozi wa Uingereza nchini. Bw. Jack amefika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, Dar es Salaam kwa ajili ya kujitambulisha na kujadili masuala mbalimbali ya ushirikiano.

𝗠𝗔𝗕𝗔𝗟𝗢𝗭𝗜 𝗧𝗘𝗠𝗘𝗞𝗘 𝗡𝗔 𝗞𝗜𝗚𝗔𝗠𝗕𝗢𝗡𝗜 𝗪𝗔𝗠𝗘𝗜𝗧𝗜𝗞𝗔𝗔𝗔, 𝗗𝗞𝗧. 𝗠𝗜𝗚𝗜𝗥𝗢 𝗔𝗞𝗢𝗦𝗛𝗪𝗔Unaambiwa k**a walidhani mambo ni majimaji waambieni kuwa m...
07/01/2026

𝗠𝗔𝗕𝗔𝗟𝗢𝗭𝗜 𝗧𝗘𝗠𝗘𝗞𝗘 𝗡𝗔 𝗞𝗜𝗚𝗔𝗠𝗕𝗢𝗡𝗜 𝗪𝗔𝗠𝗘𝗜𝗧𝗜𝗞𝗔𝗔𝗔, 𝗗𝗞𝗧. 𝗠𝗜𝗚𝗜𝗥𝗢 𝗔𝗞𝗢𝗦𝗛𝗪𝗔

Unaambiwa k**a walidhani mambo ni majimaji waambieni kuwa mambo ni moto motooo🔥🔥🔥tena kwa ile sauti ya UWT yaani motoo motoooo.

Kutokea katika ukumbi huu wa PTA, Mabalozi wote kutokea Temeke na Kigamboni wamejitokeza kuujaza ukumbi huu huku wakionesha morali ya kutosha kudhiirisha kuwa ni wazima wa afya na wapo tayari kumsikiliza, kupokea na kuzingatia maelezo na maelekezo yote yatakayotolewa na Katibu Mkuu wa CCM Balozi Dkt. 𝗔𝘀𝗵𝗮-𝗿𝗼𝘀𝗲 𝗠𝗶𝗴𝗶𝗿𝗼 siku ya leo tarehe 07 Januari 2026.

#𝙎𝙝𝙞𝙣𝙖𝙇𝙖𝙠𝙤𝙇𝙞𝙣𝙖𝙠𝙪𝙞𝙩𝙖

07/01/2026

𝗗𝗞𝗧. 𝗠𝗜𝗚𝗜𝗥𝗢 𝗔𝗪𝗘𝗞𝗔 𝗪𝗔𝗭𝗜 𝗔𝗗𝗛𝗠𝗔 𝗬𝗔 𝗠𝗪𝗘𝗡𝗬𝗘𝗞𝗜𝗧𝗜 𝗗𝗞𝗧. 𝗦𝗔𝗠𝗜𝗔 𝗬𝗔 𝗞𝗨𝗧𝗔𝗞𝗔 𝗖𝗖𝗠 𝗞𝗨𝗭𝗜𝗗𝗜 𝗞𝗨𝗜𝗠𝗔𝗥𝗜𝗞𝗔

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Balozi Dkt. 𝗔𝘀𝗵𝗮-𝗿𝗼𝘀𝗲 𝗠𝗶𝗴𝗶𝗿𝗼 amebainisha kuwa makubaliano ndani ya sekretarieti kuu ya CCM ni kuanza ziara kwenye ngazi za mashina kutazamia matawi na kata kwakuwa ndizo sehemu ambazo umadhubuti na uimara wa CCM unapoanzia.

Dkt. Migiro ameyasema hayo leo tarehe 7 Januari 2026 wakati wa kuanza kwa ziara yake aliyokutana na Mabalozi wa mashina wote kutoka wilaya za Temeke na Kigamboni katika ukumbi wa PTA Jijini Dar es salaam.

Akizungumza na Mabalozi hao, Dkt. Migiro ameeleza kuwa adhma ya Mwenyekiti wa CCM ambaye ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. 𝗦𝗮𝗺𝗶𝗮 𝗦𝘂𝗹𝘂𝗵𝘂 𝗛𝗮𝘀𝘀𝗮𝗻 ya kuhakikisha CCM inazidi kupata uimara siku hadi siku na kujipambanua zaidi kwa sera na ilani zenye kugusa matakwa na matarajio ya wananchi kwa maslahi mapana ya Taifa kwa ujumla.

#𝙎𝙝𝙞𝙣𝙖𝙇𝙖𝙠𝙤𝙇𝙞𝙣𝙖𝙠𝙪𝙞𝙩𝙖

Indirizzo

Casalnuovo Di Napoli

Notifiche

Lasciando la tua email puoi essere il primo a sapere quando Chama Cha Mapinduzi Ccm Tawi La Napoli-Italy pubblica notizie e promozioni. Il tuo indirizzo email non verrà utilizzato per nessun altro scopo e potrai annullare l'iscrizione in qualsiasi momento.

Condividi